< Ecclésiaste 11 >

1 Laisse aller ton pain au cours de l'eau; car après bien des jours tu le retrouveras.
Tupa mkate wako juu ya maji, kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.
2 Distribues-en à sept, même à huit personnes; car tu ignores ce qu'il doit y avoir de maux sur la terre.
Wape sehemu watu saba, naam hata wanane, kwa maana hujui ni baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
3 Lorsque les nuées sont pleines, elles fondent en pluie sur la terre; et si un arbre tombe au midi ou au nord, il restera là où il sera tombé.
Kama mawingu yamejaa maji, hunyesha mvua juu ya nchi. Kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, mahali ulipoangukia, hapo ndipo utakapolala.
4 Celui qui observe le vent ne sèmera pas; et celui qui regarde aux nuages ne moissonnera pas.
Yeyote atazamaye upepo hatapanda, yeyote aangaliaye mawingu hatavuna.
5 Car nul ne sait quelle est la voie du vent; comme les os cachés dans les entrailles de la femme grosse, de même te sont cachées les œuvres que Dieu a faites et toutes celle qu'Il fera encore.
Kama vile usivyofahamu njia ya upepo, au jinsi mwili uumbwavyo ndani ya tumbo la mama, vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu, Muumba wa vitu vyote.
6 Sème ton grain dès l'aurore, et que ta main ne s'arrête pas le soir; car tu ignores de celui-ci ou de celui-là lequel doit lever; s'ils lèvent tous les deux à la fois, c'est bien.
Panda mbegu yako asubuhi, nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee, kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa, kwamba ni hii au ni ile, au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.
7 La lumière est douce, et il est bon aux yeux de voir le soleil.
Nuru ni tamu, tena inafurahisha macho kuona jua.
8 L'homme qui doit vivre beaucoup d'années trouvera en toutes de la joie, et il se souviendra des jours de ténèbres, car ils seront nombreux: tout ce qui est passé est vanité.
Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani, na aifurahie yote. Lakini na akumbuke siku za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.
9 Jeune homme, réjouis-toi en ta jeunesse; que, durant les jours de ta jeunesse, ton cœur te réjouisse; marche avec innocence dans les voies de ton cœur, et non seulement ce que tes yeux auront vu. Mais sache par-dessus tout ce que le Seigneur t'appellera devant Sa justice.
Furahi ewe kijana, wakati ungali kijana, moyo wako na ukupe furaha katika siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na chochote macho yako yaonayo, lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote Mungu atakuleta hukumuni.
10 Éloigne de ton cœur la colère, et bannis de ta chair la méchanceté; car la jeunesse et la folie sont vanité.
Kwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako, kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.

< Ecclésiaste 11 >