< Deutéronome 5 >

1 Et Moïse convoqua tout Israël, et il dit: Ecoute, Israël, les jugements et les ordonnances que je vais te faire entendre aujourd'hui: retiens-les, et veille à les mettre en pratique.
Mose akawaita Israeli wote, akawaambia: Ee Israeli, sikilizeni amri na sheria ninazowatangazia leo. Jifunzeni, na mwe na hakika kuzifuata.
2 Le Seigneur votre Dieu a fait alliance avec vous en Horeb.
Bwana Mungu wetu alifanya Agano nasi katika mlima wa Horebu.
3 Ce n'est point avec vos pères que le Seigneur a fait cette alliance, mais avec vous, vous tous assemblés ici, vivant encore.
Si kwamba Bwana alifanya Agano na baba zetu, bali alifanya nasi, nasi sote ambao tuko hai hapa leo.
4 Le Seigneur vous a parlé face à face en la montagne, au milieu du feu.
Bwana alisema nanyi uso kwa uso kutoka moto juu ya mlima.
5 Et moi, en ce temps-là, je me tenais entre le Seigneur et vous, pour vous rapporter les paroles du Seigneur; car vous étiez épouvantés à l'aspect du feu, et vous ne montiez point sur la montagne; et le Seigneur a dit:
(Wakati huo nilisimama kati ya Bwana na ninyi kuwatangazia neno la Bwana, kwa sababu mliogopa ule moto, nanyi hamkupanda mlimani.) Naye Mungu alisema:
6 Je suis le Seigneur ton Dieu qui t'ai fait sortir de la terre d'Egypte, de la maison de servitude.
“Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
7 Tu n'auras point d'autres dieux devant ma face.
Usiwe na miungu mingine ila mimi.
8 Tu ne te feras point d'idoles, ni d'images d'aucune chose existant dans le ciel, sur la terre, sous la terre et dans les eaux.
Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji.
9 Tu ne les adoreras point, tu ne les serviras point; car je suis le Seigneur ton Dieu, Dieu jaloux, vengeant sur les enfants les péchés des pères, jusqu'à la troisième ou à la quatrième génération de ceux qui me haïssent,
Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
10 Et faisant miséricorde, pendant des milliers de générations, à ceux qui m'aiment et qui observent mes commandements.
lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
11 Tu ne prendras pas en vain le nom du Seigneur ton Dieu; car le Seigneur ton Dieu ne regardera point comme pur celui qui aura pris son nom en vain.
Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
12 Sois attentif le jour du sabbat a le sanctifier, comme te l'a prescrit le Seigneur ton Dieu.
Adhimisha siku ya Sabato na kuiweka takatifu, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza.
13 Pendant six jours, travaille et fais tous tes ouvrages.
Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote.
14 Mais le septième jour est le sabbat du Seigneur ton Dieu; tu ne feras aucune œuvre en ce jour-là, ni toi, ni ton fils, ni ta fille, ni ton serviteur, ni ta servante, ni ton bœuf, ni ton âne, ni aucune de tes bêtes, ni le prosélyte demeurant avec toi; ton serviteur, ta servante, ton âne, se reposeront comme toi.
Lakini siku ya Saba ni Sabato kwa Bwana, Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wa kiume au mtumishi wa kike, wala ngʼombe wako, punda wako au mnyama wako yeyote, wala mgeni aliyeko malangoni mwako, ili kwamba mtumishi wako wa kiume na wa kike wapate kupumzika kama wewe.
15 Souviens-toi que tu étais esclave en Egypte, et que le Seigneur Dieu t'en a fait sortir par une main puissante, par un bras très-haut; c'est pourquoi le Seigneur ton Dieu te commande d'observer le jour du sabbat et de le sanctifier.
Kumbuka mlikuwa watumwa huko Misri, na Bwana Mungu wenu aliwatoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa. Kwa hiyo Bwana Mungu wako amekuagiza kuiadhimisha siku ya Sabato.
16 Honore ton père et ta mère, comme te l'a prescrit le Seigneur ton Dieu, afin que tu sois heureux, et que tu vives longtemps sur la terre que te donne le Seigneur ton Dieu.
Waheshimu baba yako na mama yako, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza, ili siku zako zipate kuwa nyingi na kufanikiwa katika nchi Bwana Mungu wako anayokupa.
17 Tu ne seras pas adultère.
Usiue.
18 Tu ne tueras point.
Usizini.
19 Tu ne voleras point.
Usiibe.
20 Tu ne porteras pas de faux témoignage contre ton prochain.
Usimshuhudie jirani yako uongo.
21 Tu ne convoiteras pas la femme de ton prochain; tu ne convoiteras pas la maison de ton prochain, ni son champ, ni son serviteur, ni sa servante, ni son bœuf, ni son âne, ni aucune de ses bêtes, ni rien de ce qui est à ton prochain.
Usitamani mke wa jirani yako. Usitamani nyumba ya jirani yako au shamba lake, mtumishi wake wa kiume au wa kike, ngʼombe au punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.”
22 Telles sont les paroles que le Seigneur a dites en la montagne, devant toute votre synagogue, au milieu du feu; alentour, il y avait obscurité, ténèbres, tempête, grands éclats de tonnerre; et il n'y a rien ajouté, et il a gravé ces paroles sur deux tables de pierre, et il me les a données.
Hizi ndizo amri alizozitangaza Bwana kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lenu lote huko mlimani kutoka kwenye moto, wingu na giza nene, wala hakuongeza chochote zaidi. Kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe, naye akanipa mimi.
23 Et, pendant que vous écoutiez la voix qui sortait du feu, la montagne était enflammée; alors, vous vîntes à moi, vous tous, vous princes de vos tribus, avec vos anciens;
Mliposikia sauti kutoka kwenye giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto, viongozi wenu wote wa makabila yenu na wazee wenu walinijia mimi.
24 Vous dites: Voilà que le Seigneur notre Dieu nous a montré sa gloire, et nous avons entendu sa voix du milieu du feu; nous savons aujourd'hui que le Seigneur Dieu peut parler à un homme, et celui-ci vivre encore.
Nanyi mkasema, “Bwana Mungu wetu ametuonyesha utukufu na enzi yake, nasi tumesikia sauti yake kutoka kwenye moto. Leo tumeona kwamba mwanadamu anaweza kuishi hata kama Mungu akizungumza naye.
25 Maintenant, prends garde que nous ne mourions; car ce grand feu va nous dévorer, si nous continuons d'écouter la voix du Seigneur notre Dieu, et nous périrons.
Lakini sasa, kwa nini tufe? Moto huu mkubwa utatuteketeza sisi na tutakufa kama tukiendelea kusikia sauti ya Bwana Mungu wetu zaidi.
26 En effet, quelle chair aura entendu, comme nous, la voix du Dieu vivant, parlant du milieu du feu, et vivra encore?
Ni mtu yupi mwenye mwili ambaye amewahi kuisikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza kutoka kwenye moto, kama sisi tulivyoisikia, naye akaishi?
27 Approche-toi donc seul, écoute tout ce que dira le Seigneur notre Dieu, et tu nous répèteras tout ce que t'aura dit le Seigneur notre Dieu, et nous le saurons, et nous obéirons.
Sogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”
28 Et le Seigneur ouït la rumeur de vos discours pendant que vous me parliez, et il me dit: j'ai ouï la rumeur des discours de ce peuple, j'ai entendu tout ce qu'il t'a dit; et, en tout, il a bien parlé.
Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri.
29 Puissent leurs cœurs ne point changer, afin qu'ils me craignent et observent mes commandements; alors, ils prospèreront, eux et leurs fils, à jamais!
Laiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!
30 Va, et dis-leur: Retournez sous vos tentes.
“Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao.
31 Cependant, demeure auprès de moi, et je te dirai les commandements, les jugements et les ordonnances que tu auras à leur enseigner, afin qu'ils les mettent en pratique dans la terre que je leur donne pour héritage.
Lakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”
32 Soyez donc attentifs à vous conduire comme l'a prescrit le Seigneur votre Dieu; ne vous écartez ni à droite ni à gauche,
Hivyo kuweni waangalifu kuyafanya yale Bwana Mungu wenu aliyowaagiza; msigeuke upande wa kuume wala wa kushoto.
33 En toute voie ou le Seigneur votre Dieu vous a prescrit de marcher, si vous voulez qu'il vous donne prospérité et repos; et vous vivrez de longs jours en la terre qui sera votre héritage.
Fuateni yale yote ambayo Bwana Mungu wenu aliwaagiza, ili mpate kuishi, kustawi na kuziongeza siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.

< Deutéronome 5 >