< Deutéronome 16 >

1 Observe le mois des blés nouveaux, et tu feras la Pâque du Seigneur ton Dieu, parce que dans le mois des blés nouveaux, tu es sorti nuitamment de l'Egypte.
Shikeni mwezi wa Abibu, na kuiadhimisha Pasaka ya Bwana Mungu wenu, kwa sababu katika mwezi wa Abibu, Mungu aliwatoa Misri usiku.
2 Tu sacrifieras, pour la Pâque du Seigneur ton Dieu, des bœufs, des brebis et des chèvres, au lieu seul que le Seigneur ton Dieu aura choisi afin que son nom y soit invoqué.
Mtatoa dhabihu ya Pasaka ya mnyama kwa Bwana Mungu wenu kutoka kundi lenu la mbuzi na kondoo au la ngʼombe, mahali pale ambapo Bwana atapachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake.
3 Avec la victime, tu ne mangeras pas de pain levé; pendant sept jours, avec ses chairs, tu mangeras des azymes, pain de la mortification, parce qu'à la hâte vous êtes sortis de l'Egypte, et parce qu'il faut vous souvenir du jour de votre sortie d'Egypte, tous les jours de votre vie.
Msile nyama hiyo pamoja na mikate iliyotiwa chachu, lakini kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, mikate ya kujitesa, kwa sababu mliondoka Misri kwa haraka, ili kwamba siku zote za maisha yenu mpate kukumbuka wakati wenu wa kuondoka Misri.
4 On ne verra pas chez toi de pain levé, en tout ton territoire, pendant sept jours; rien ne restera des chairs des victimes que tu auras sacrifiées sur le soir du premier jour.
Chachu isionekane katika mali zenu katika nchi yenu yote kwa siku saba. Nyama yoyote ya dhabihu mtakayotoa jioni ya siku ya kwanza isibakizwe mpaka asubuhi.
5 Tu ne pourras sacrifier la Pâque dans aucune des villes que le Seigneur ton Dieu te donne;
Kamwe msitoe dhabihu ya Pasaka katika mji wowote ambao Bwana Mungu wenu amewapa,
6 Mais au lieu seul que le Seigneur ton Dieu aura choisi pour que son nom y soit invoqué; tu sacrifieras la Pâque sur le soir, au coucher du soleil, vers l'heure où tu es sorti de l'Egypte.
isipokuwa mahali atakapopachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake. Hapo ndipo lazima mtoe dhabihu ya Pasaka jioni, jua litakapotua, iwe kumbukumbu yenu ya kutoka Misri.
7 Tu feras bouillir ou rôtir les chairs, et tu les mangeras au lieu seul qu'aura choisi le Seigneur ton Dieu, et, le lendemain matin, pars, retourne en tes demeures.
Okeni na mle mahali pale ambapo Bwana Mungu wenu atakapopachagua, kisha asubuhi mrudi kwenye mahema yenu.
8 Tu mangeras des azymes pendant six jours; le septième jour, pour finir, sera la fête du Seigneur ton Dieu; tu ne feras ce jour-là aucune œuvre, sauf toutes les choses que l'on fait à cause d'un mort.
Kwa siku sita mtakula mikate isiyotiwa chachu na siku ya saba fanyeni kusanyiko kwa ajili ya Bwana Mungu wenu na msifanye kazi.
9 Tu compteras en toi-même sept semaines, à partir du jour ou ta faux commencera la moisson.
Mhesabu majuma saba tangu wakati mnapoanza kuchukua mundu kuvuna nafaka.
10 Tu célèbreras ensuite la fête des semaines du Seigneur ton Dieu, selon tes facultés, selon ce que t'aura donné le Seigneur ton Dieu.
Kisha msherehekee Sikukuu ya Majuma kwa Bwana Mungu wenu kwa kutoa sadaka ya hiari kwa kadiri ya baraka ambayo Bwana Mungu wenu amewapa.
11 Tu te réjouiras devant le Seigneur ton Dieu, toi et ton fils, et ta fille, et ton serviteur, et la servante, et le lévite, et le prosélyte, et l'orphelin, et la veuve, qui se trouvent parmi vous, au lieu seul que le Seigneur aura choisi pour que son nom y soit invoqué.
Shangilieni mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua kama makao ya Jina lake, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi walio katika miji yenu, na wageni, yatima na wajane waishio miongoni mwenu.
12 Et tu te souviendras que tu as été esclave en la terre d'Egypte, et tu observeras et exécuteras les commandements.
Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa kule Misri na mfuate amri hizi kwa uangalifu.
13 Tu célèbreras la fête des tabernacles pendant sept jours, lorsque tu auras recueilli, tant sur l'aire que dans le pressoir, les fruits de tes champs.
Adhimisheni sikukuu ya vibanda kwa siku saba baada ya kukusanya mazao yenu ya nafaka na kukamua zabibu.
14 Tu te réjouiras, en cette fête, toi, et ton fils, et ta fille, et ton serviteur, et ta servante, et le lévite, et le prosélyte, et l'orphelin, et la veuve, qui se trouveront dans tes villes.
Mfurahie sikukuu yenu, ninyi, wana wenu, binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi, wageni, yatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.
15 Tu célèbreras cette fête pendant sept jours en l'honneur du Seigneur ton Dieu, au lieu seul qu'aura choisi le Seigneur, et le Seigneur te bénira en toutes tes récoltes, en toutes œuvres de tes mains, et tu seras plein de joie.
Kwa siku saba mtaiadhimisha sikukuu ya Bwana Mungu wenu katika mahali atakapopachagua Bwana. Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki katika mavuno yenu na katika kazi zote za mikono yenu na furaha yenu itakamilika.
16 Trois fois par an, tout mâle parmi vous se présentera devant le Seigneur votre Dieu, au lieu seul qu'aura choisi le Seigneur, pour la fête des azymes, pour la tête des semaines et pour la fête des tabernacles; nul ne se présentera les mains vides devant le Seigneur.
Wanaume wenu wote lazima wajitokeze mara tatu kwa mwaka mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua: kwa ajili ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma, na Sikukuu ya Vibanda. Hakuna mtu atakayejitokeza mbele za Bwana mikono mitupu:
17 Chacun de vous offrira selon ses facultés, et selon que le Seigneur l'aura béni.
Kila mmoja wenu ni lazima alete zawadi kulingana na jinsi ambavyo Bwana Mungu wenu alivyowabariki.
18 Tu institueras pour toi des juges et des scribes dans les villes que le Seigneur te donne par tribus; ils jugeront le peuple, et rendront des jugements équitables.
Wateue waamuzi na maafisa kwa kila kabila lenu katika kila mji ambao Bwana Mungu wenu anawapa, nao watawaamua watu kwa usawa.
19 Ils ne feront point pencher la justice, ils ne feront point acception des personnes, ils n'accepteront point de présents; car les présents aveuglent le sage, et ôtent aux justes leur intelligence.
Msipotoshe haki wala msifanye upendeleo. Msikubali rushwa kwa sababu rushwa hupofusha macho ya wenye busara na kugeuza maneno ya wenye haki.
20 Vous vous efforcerez de rendre justice selon l'équité, afin que vous viviez et que vous entriez en la terre que le Seigneur vous donne, pour qu'elle soit votre héritage.
Mfuate haki na haki peke yake, ili mweze kuishi na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa.
21 Tu ne planteras point de bois sacré; tu ne planteras aucun autre arbre auprès de l'autel de ton Dieu.
Msisimamishe nguzo yoyote ya Ashera kando ya madhabahu mliyomjengea Bwana Mungu wenu,
22 Tu ne t'érigeras point de colonnes; le Seigneur ton Dieu les exècre.
wala msisimamishe jiwe la kuabudu, kwa maana Bwana Mungu wenu anavichukia vitu hivi.

< Deutéronome 16 >