< Daniel 9 >
1 En la première année du règne de Darius, fils d'Assuérus, de la race des Mèdes, qui régna sur l'empire des Chaldéens,
Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario mwana wa Ahasuero (mzaliwa wa Umedi), ambaye alifanywa mtawala juu ya ufalme wa Babeli,
2 Moi, Daniel, je compris, au moyen des livres, le nombre des années que la parole du Seigneur avait fait connaître à Jérémie le prophète, sur le temps que devait durer la désolation de Jérusalem, et qui devait être de soixante-dix années.
katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, mimi Danieli nilielewa kutokana na Maandiko, kulingana na neno la Bwana alilopewa nabii Yeremia, kwamba ukiwa wa Yerusalemu ungetimizwa kwa miaka sabini.
3 Et je tournai mon visage vers le Seigneur mon Dieu, pour l'implorer et le prier, en jeûnant, et revêtu d'un cilice.
Kwa hiyo nikamgeukia Bwana Mungu na kumsihi katika maombi na dua, katika kufunga, na kuvaa nguo ya gunia na kujipaka majivu.
4 Et je fis ma prière au Seigneur mon Dieu, et je lui rendis gloire, et je dis: Seigneur, Dieu grand et admirable, qui gardez votre alliance, et réservez votre miséricorde en faveur de ceux qui vous aiment et observent vos commandements;
Nikamwomba Bwana Mungu wangu na kutubu: “Ee Bwana, Mungu mkuu na unayetisha, anayeshika agano lake la upendo kwao wanaompenda na kutii maagizo yake,
5 Nous avons péché; nous avons commis l'injustice et l'iniquité; nous nous sommes retirés de vous; nous avons dévié de vos ordonnances et de vos jugements,
tumetenda dhambi na kufanya mabaya. Tumekuwa waovu na tumeasi; tumegeuka mbali na maagizo yako na sheria zako.
6 Et nous n'avons point écouté vos serviteurs les prophètes, qui, en votre nom, parlaient à nos rois, à nos princes, à nos pères et à tout le peuple de la terre.
Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, wakuu wetu, baba zetu, na watu wote wa nchi.
7 À vous, Seigneur, est la justice; à nous la honte au visage, comme aujourd'hui à tout homme de Juda, à tout habitant de Jérusalem, à tout Israël, soit près d'ici, soit au loin, en toute région où vous les avez dispersés à cause des prévarications qu'ils ont commises.
“Bwana, wewe ni mwenye haki, lakini siku hii ya leo tumefunikwa na aibu: tukiwa wanaume wa Yuda, na watu wa Yerusalemu, na Israeli yote, wote walio karibu na walio mbali, katika nchi zote ulikotutawanya kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako.
8 En vous, Seigneur, est notre justice; à nous la honte au visage, à nous, à nos rois, à nos princes et à nos pères; car nous avons tous péchés contre vous.
Ee Bwana, sisi na wafalme wetu, wakuu wetu na baba zetu tumefunikwa na aibu kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
9 À vous, Seigneur notre Dieu, les miséricordes et le pardon; car nous nous sommes retirés de vous,
Bwana Mungu wetu ni mwenye rehema na anayesamehe, hata ingawa tumefanya uasi dhidi yake.
10 Et nous n'avons point écouté la voix du Seigneur notre Dieu, pour marcher dans les lois qu'il nous a données, face à face, par les mains de ses serviteurs les prophètes.
Hatukumtii Bwana Mungu wetu wala kuzishika sheria alizotupa kupitia kwa watumishi wake manabii.
11 Tout Israël a transgressé votre loi; il s'est détourné tout entier, pour ne pas entendre votre parole. Et votre malédiction est tombée sur nous, ainsi que l'imprécation écrite dans la loi de Moise, serviteur de Dieu, parce que nous avons péché contre vous.
Israeli yote imekosea sheria yako na kugeuka mbali, nao wamekataa kukutii. “Kwa hiyo laana na viapo vya hukumu vilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, mtumishi wa Mungu, vimemiminwa juu yetu, kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
12 Et Dieu a confirmé ses paroles prononcées contre nous et contre les juges qui nous jugeaient, et qui ont amené sur nous de si grands maux, que jamais rien sous le ciel n'advint comme ce qui est advenu à Jérusalem;
Umetimiza maneno uliyosema dhidi yetu na dhidi ya watawala wetu, kwa kuleta maafa makubwa juu yetu. Chini ya mbingu yote kamwe hapajatendeka kitu kama kile kilichotendeka kwa Yerusalemu.
13 Comme il est écrit en la loi de Moïse: Tous ces maux sont arrivés sur nous, et nous n'avons point prié devant la face du Seigneur notre Dieu, pour qu'il nous retirât de nos iniquités, et nous fit comprendre toute sa vérité.
Kama vile ilivyoandikwa katika sheria ya Mose, misiba hii yote imekuja juu yetu, lakini hatujaomba fadhili kwa Bwana Mungu wetu kwa kugeuka kutoka dhambi zetu na kuwa wasikivu katika kweli yake.
14 Mais le Seigneur a veillé sur nous, et il a amené sur nous ces maux, parce que le Seigneur notre Dieu est juste en toutes ses œuvres, et que nous n'avions point écouté sa voix.
Bwana hakusita kuleta maafa juu yetu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mwenye haki katika kila afanyalo; lakini hata hivyo hatujamtii.
15 Et maintenant, Seigneur notre Dieu, qui par votre main puissante avez délivré votre peuple de la terre d'Égypte, et qui vous êtes fait alors un nom comme aujourd'hui, nous avons péché, nous avons commis l'iniquité!
“Sasa, Ee Bwana Mungu wetu, ambaye uliwatoa watu wako Misri kwa mkono wenye nguvu, na ambaye umejifanyia Jina linalodumu mpaka leo, tumetenda dhambi, tumefanya mabaya.
16 Seigneur, votre miséricorde est pour tous; que votre indignation et votre colère se détourne de votre ville de Jérusalem et de votre montagne sainte; car nous avons péché, et à cause de nos iniquités et de celles de nos pères, Jérusalem et votre peuple sont devenus un sujet d'opprobre pour tous ceux qui nous entourent.
Ee Bwana, wewe kwa kadiri ya matendo yako ya haki, ondoa hasira yako na ghadhabu yako juu ya Yerusalemu, mji wako, mlima wako mtakatifu. Dhambi zetu na maovu ya baba zetu yameifanya Yerusalemu na watu wako kitu cha kudharauliwa kwa wale wote wanaotuzunguka.
17 Et maintenant, Seigneur notre Dieu, écoutez la prière de votre serviteur et ses supplications; faites briller votre face dans votre sanctuaire délaissé; faites-le pour vous, Seigneur!
“Basi Mungu wetu, sasa sikia maombi na dua ya mtumishi wako. Ee Bwana, kwa ajili yako angalia kwa huruma ukiwa wa mahali pako patakatifu.
18 Inclinez votre oreille, Seigneur mon Dieu, et exaucez-nous; ouvrez les yeux, et voyez notre anéantissement et celui de la cité à laquelle était donné votre nom; car ce n'est point dans l'attente de vos jugements que nous jetons devant vous notre cri de pitié, mais en vue de vos abondantes miséricordes, O Seigneur.
Ee Mungu, tega sikio na ukasikie; fumbua macho yako ukaone ukiwa wa mji ule wenye Jina lako. Hatukutolei maombi yetu kwa sababu sisi tuna haki, bali kwa sababu ya rehema zako nyingi.
19 Exaucez-moi, Seigneur; apaisez-vous, Seigneur; aimez-moi, Seigneur: ne différez pas, ô mon Dieu, pour l'amour de vous-même; car cette cité et ce peuple sont ceux à qui a été donné votre nom.
Ee Bwana, sikiliza! Ee Bwana, samehe! Ee Bwana, sikia na ukatende! Kwa ajili yako, Ee Mungu wangu, usikawie, kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa Jina lako.”
20 Et comme je parlais encore, comme je priais, et que je confessais mes péchés et les péchés d'Israël, mon peuple; comme je jetais en face du Seigneur mon Dieu mon cri de pitié pour la montagne sainte;
Basi, nilipokuwa bado nikinena na kuomba, nikiungama dhambi yangu na dhambi ya watu wangu Israeli, na nikifanya maombi yangu kwa Bwana Mungu wangu kwa ajili ya mlima wake mtakatifu,
21 Tandis que je parlais encore, voilà que l'homme Gabriel, qui m'était apparu au commencement de ma vision, vint en volant, et me toucha vers l'heure du sacrifice du soir.
wakati nilipokuwa bado katika maombi, Gabrieli, yule mtu niliyekuwa nimemwona katika maono hapo awali, alinijia kwa kasi karibu wakati wa kutoa dhabihu ya jioni.
22 Et il m'ouvrit l'intelligence, et il me parla et me dit: Daniel, je suis venu pour t'apporter l'intelligence.
Akanielimisha na kuniambia, “Danieli, sasa nimekuja kukupa akili na ufahamu.
23 Au commencement de ta prière, un ordre m'est venu, et je suis venu pour t'instruire; car tu es l'homme des désirs, dit-il. Réfléchis donc à ma parole et comprends ta vision.
Mara ulipoanza kuomba, jibu lilitolewa, ambalo nimekuja kukupasha habari, kwa maana wewe unapendwa sana. Kwa hiyo, tafakari ujumbe huu na uelewe maono haya:
24 Soixante-dix semaines ont été assignées à ton peuple et à la cité sainte, pour que le péché soit à sa fin, que les péchés soient abolis, que les iniquités soient effacées et expiées, que l'éternelle justice soit ramenée, que le sceau soit mis à la vision et au prophète, et que le Saint des saints soit marqué de l'onction.
“Majuma sabini yameamriwa kwa ajili ya watu wako na kwa ajili ya mji wako mtakatifu, ili kumaliza makosa, kukomesha dhambi, kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri maono na unabii, na pia kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu sana.
25 Sache donc et comprends qu'à partir de l'ordre qui sera donné de parler et de rebâtir Jérusalem, jusqu'au roi Christ, il y aura sept semaines et soixante-deux semaines; et l'ancien temps reviendra, les places et les remparts seront relevés, et les temps accomplis.
“Ujue na kuelewa hili: Tangu kutolewa kwa amri ya kuutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu mpaka kuja kwa Mpakwa mafuta, aliye mtawala, kutakuwako majuma saba na majuma sitini na mawili. Barabara zitajengwa tena pamoja na mahandaki, lakini katika wakati wa taabu.
26 Et après les soixante-deux semaines le Christ sera mis à mort, et il n'y aura pas en lui de sujet de condamnation; et il détruira la ville et le sanctuaire, à l'aide d'un chef qui surviendra; et ils disparaîtront dans un cataclysme, et à la fin de la guerre, qui sera abrégée, il livrera la ville aux désolations.
Baada ya majuma sitini na mawili, Mpakwa Mafuta atakatiliwa mbali, wala hatabaki na kitu. Watu wa mtawala atakayekuja watauharibu mji pamoja na mahali patakatifu. Mwisho utakuja kama mafuriko: Vita vitaendelea mpaka mwisho, nao ukiwa umeamriwa.
27 Et durant une semaine il confirmera l'alliance avec plusieurs. Et au milieu de la semaine la victime et les libations me seront ôtées, et l'abomination de la désolation sera sur le temple, et la désolation aura sa fin à la consommation des temps.
Mtawala huyo atathibitisha agano na watu wengi kwa juma moja. Katikati ya juma hilo atakomesha dhabihu na sadaka. Mahali pa dhabihu katika Hekalu atasimamisha chukizo la uharibifu, hadi mwisho ulioamriwa utakapomiminwa juu yake yeye aletaye uharibifu.”