< Daniel 11 >

1 Je suis celui qui, en la première année du règne de Cyrus, se tint près de lui pour le fortifier et l'affermir.
Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
2 Et maintenant je te ferai connaître la vérité: trois rois règneront encore sur la Perse; le quatrième prospèrera et les surpassera tous en richesses; et lorsqu'il sera en possession de ses richesses, il fera la guerre à tous les royaumes des Hellènes.
“Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
3 Et un roi puissant s'élèvera, et il sera maître d'un grand empire, et il fera ce qu'il voudra.
Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
4 Et, au moment où son empire sera affermi, il sera brisé et partagé aux quatre vents du ciel; et il ne passera point à ses descendants, et il ne gardera point sa puissance selon ses désirs; car sa royauté lui sera arrachée; puis elle passera à d'autres après lui.
Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
5 Et le roi du midi se fortifiera; mais l'un de ces princes prévaudra contre lui, et il dominera sur un grand royaume.
“Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
6 Et quelques années après ils s'uniront; et la fille du roi du midi ira trouver le roi de l'aquilon pour faire alliance avec lui; mais elle ne retirera pas de là un bras puissant; et la race du vainqueur ne se maintiendra pas; et elle-même sera livrée avec ceux qui la conduisaient, et la jeune fille, et celui qui la fortifiait en ces temps.
Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
7 Mais un rejeton de la fleur de sa racine s'élèvera bientôt après; et il s'avancera à la tête d'une armée, et il entrera dans les forteresses du roi de l'aquilon; il combattra contre elles, et il s'en rendra maître.
“Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
8 Et il transportera en Égypte, avec les captifs, leurs dieux et leurs statues de fonte et leurs objets précieux d'argent et d'or; et lui-même subsistera plus longtemps que le roi de l'aquilon.
Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
9 Celui-ci à son tour entrera dans le royaume du roi du midi, puis il retournera en sa propre terre.
Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
10 Et ses fils parmi maintes nations rassembleront une grande multitude; et l'un d'eux se mettra en campagne; et en sa marche il s'avancera comme un torrent débordé; il passera, il campera et rassemblera, ses forces pour le combat.
Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
11 Et le roi du midi s'effarouchera, et il s'avancera pour combattre le roi de l'aquilon; et il lèvera une grande armée, et une grande multitude d'ennemis lui sera livrée.
“Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
12 Et il prendra captive cette multitude, et son cœur s'enorgueillira, et il massacrera des myriades d'ennemis; mais il n'en sera pas plus puissant.
Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
13 Car le roi de l'aquilon reviendra, et il conduira des troupes en plus grand nombre que la première fois; et à la fin des temps et des années une armée envahissante arrivera avec une grande force et de grands approvisionnements.
Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
14 Et en ce temps-là plusieurs se soulèveront contre le roi du midi, et des fils de ton peuple s'élèveront comme un fléau pour accomplir une vision; mais ils manqueront de force.
“Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
15 Car le roi de l'aquilon s'avancera; il élèvera des terrasses; il prendra des villes fortes; et les bras du roi du midi soutiendront le choc, et ses troupes d'élite se lèveront; mais ils ne seront pas de force à résister.
Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
16 Et le roi de l'aquilon, après l'avoir ainsi envahi, fera tout ce qu'il voudra, et nul ne tiendra devant lui. Et il s'arrêtera en la terre de Sabé; et il la détruira de sa main.
Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
17 Et il tournera son visage pour entrer en forces dans le royaume du midi, et toutes choses prospèreront devant lui; il donnera au roi ennemi une fille des femmes pour le perdre; mais il n'y réussira point, et elle ne sera pas à lui.
Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
18 Alors il tournera son visage contre les îles, et il en prendra plusieurs; et il arrêtera d'abord les princes de son opprobre; mais son opprobre retombera sur lui.
Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
19 Et il retournera son visage vers la force de sa terre; mais il sera affaibli, et il tombera, et on ne le retrouvera plus.
Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
20 Et de sa racine s'élèvera un rejeton qui sera comme un plant sur le trône qu'il occupait avec gloire. Et en ces jours-là il sera encore brisé, mais non en face, non dans un combat.
“Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
21 Un autre prendra sa place, qui sera méprisé; on ne lui aura point accordé les honneurs de la royauté; mais il viendra avec ruse, et à force d'artifices il se rendra maître du royaume,
“Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
22 Et les bras de son adversaire seront énervés devant sa face; ils seront brisés, ainsi que le chef de l'alliance.
Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
23 Et après leur traité, il trompera encore celui-ci; il s'avancera, et prévaudra sur lui avec un petit nombre de troupes.
Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
24 Il viendra en des régions paisibles et opulentes; et il fera ce que n'ont fait ni ses pères ni les pères de ses pères; il emportera leur butin, leurs dépouilles, leurs richesses, et il concevra de mauvais desseins contre l'Égypte; mais cela n'aura qu'un temps.
Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
25 Et sa force et son cœur s'élèveront avec une grande force contre le roi du midi; et le roi du midi soutiendra aussi la guerre avec une force très grande et très redoutable; mais ses armées ne tiendront pas, parce que de mauvais desseins auront été formés contre lui.
“Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
26 On mangera avec lui; puis on le brisera, et son ennemi engloutira ses armées, et les morts tomberont en foule.
Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
27 Et les deux rois, le cœur plein de perversité, assis à la même table, se diront des mensonges; mais cela ne réussira pas, parce que leur fin arrivera au temps marqué.
Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
28 Et le roi de l'aquilon retournera en sa terre avec de grandes richesses; et son cœur sera opposé à l'alliance sainte, et il fera de grandes choses, et il rentrera dans son royaume.
Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
29 Il reviendra au temps marqué, et marchera contre le midi; mais cette dernière invasion ne sera pas comme la première.
“Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
30 Les Citians, sortis de leurs pays, marcheront contre lui; et par eux il sera abaissé, et il battra en retraite; il s'irritera contre l'alliance sainte, et agira contre elle; puis il se remettra en campagne, et s'entendra avec ceux qui auront abandonné l'alliance sainte.
Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
31 Et des rejetons de lui s'élèveront, et ils profaneront le sanctuaire de la Toute-Puissance, et ils feront cesser le sacrifice perpétuel, et ils le remplaceront par l'abomination de la désolation.
“Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
32 Et les impies feront alliance entre eux pour faire le mal; mais un peuple connaissant son Dieu prévaudra et agira vaillamment.
Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
33 Et les sages du peuple comprendront beaucoup de choses; toutefois ils seront affaiblis par le glaive, par le feu, par la captivité, et par un pillage qui durera bien des jours.
“Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
34 Et dans leur détresse ils recevront un faible secours; mais plusieurs se joindront à eux avec des vues perfides,
Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
35 Et parmi les sages quelques-uns auront beaucoup à souffrir pour être purifiés, élus et manifestés aux derniers jours; car ces choses doivent s'accomplir au temps marqué.
Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
36 Et le roi fera selon sa volonté; il s'élèvera, et il se glorifiera contre toute divinité, et il parlera un langage superbe, et il prospèrera jusqu'à ce que la colère de Dieu s'accomplisse; car cela doit finir ainsi.
“Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
37 Et il ne reconnaîtra aucun des dieux de ses pères; il sera épris des femmes, et ne reconnaîtra aucun dieu; car il se croira plus grand qu'eux tous.
Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
38 Et il honorera le dieu Maozim en son temple, et il le glorifiera en lui offrant de l'or, de l'argent, des pierres précieuses et des choses de prix, ce dieu que ses pères ne connaissaient pas.
Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
39 Et il donnera place dans les forteresses de refuge à un dieu étranger; il multipliera ses honneurs; il lui assujettira beaucoup d'hommes, et il partagera la terre pour en faire des présents.
Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
40 Et au temps marqué il sera aux prises avec le roi du midi; et le roi de l'aquilon conduira contre lui une multitude de chars, de cavaliers, de vaisseaux, et il envahira sa terre, et il la traversera, et il la foulera aux pieds.
“Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
41 Et il entrera dans la terre de Sébaïm, et beaucoup succomberont. Et voici ceux qui échapperont à sa main: Édom, Moab et la principauté des fils d'Ammon.
Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
42 Et il étendra son bras sur la terre de Palestine, et l'Égypte ne sera pas sauvée.
Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
43 Et il se rendra maître des lieux où sont cachés l'or et l'argent et tout ce qu'il y a de précieux en Égypte, en Libye et en Éthiopie, et dans leurs forteresses.
Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
44 Puis des rumeurs, des nouvelles pressantes, de l'orient et du nord, le troubleront; et il viendra plein de colère pour exterminer beaucoup d'ennemis.
Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
45 Et il dressera les tentes de son palais entre les mers, sur la montagne sainte de Sébaïn, et il y viendra jusqu'à sa fin, et nul ne pourra le sauver.
Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.

< Daniel 11 >