< Amos 8 >

1 Ceci est la vision que m'a envoyé le Seigneur Dieu; voilà un vase d'oiseleur à la glu.
Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
2 Et le Seigneur me dit: Que vois-tu, Amos? et je dis: Un vase d'oiseleur à la glu; et le Seigneur me dit: La fin de Mon peuple d'Israël est arrivée; Je ne continuerai plus de Me montrer à lui.
Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
3 Et en ce jour-là les lambris du temple pousseront des cris de douleur, dit le Seigneur. Une multitude d'hommes tomberont en tous lieux; et J'étendrai sur eux le silence.
Bwana Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
4 Écoutez donc ces choses, vous qui le matin opprimez l'indigent, et qui foulez aux pieds les pauvres de la terre,
Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
5 disant: Quand donc le mois sera-t-il écoulé pour que nous vendions? Quand finira le sabbat pour que nous ouvrions nos greniers, que nous fassions petite mesure, que nous augmentions les poids et faussions le balance;
mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
6 pour que nous achetions le pauvre à prix d'argent; l'indigent pour des sandales, et que nous trafiquions sur toutes les denrées?
mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
7 Le Seigneur fait serment de punir l'orgueil de Jacob: Nulle de vos œuvres, en Ma victoire, ne sera oubliée.
Bwana ameapa kwake mwenyewe, aliye Kiburi cha Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
8 Et n'est-ce pas à cause de ces choses que la terre sera troublée, que tous ceux qui l'habitent seront dans la douleur; et que la destruction montera comme le fleuve d'Égypte, et descendra comme lui?
“Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
9 En ce jour-là ceci arrivera, dit le Seigneur Maître: Le soleil se couchera à Midi, et sur la terre, la lumière fera place aux ténèbres,
“Katika siku ile,” asema Bwana Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
10 et Je changerai vos fêtes en deuil, et tous vos cantiques en lamentations; et je ceindrai vos reins de cilices, et toute tête deviendra chauve; et Israël pleurera, comme on pleure un bien-aimé, et ceux qui l'accompagneront souffriront comme en un jour de douleurs.
Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
11 Voilà que ces jours arrivent, dit le Seigneur, et J'enverrai la famine sur la terre, non la disette de pain et d'eau, mais la soif d'entendre la parole du Seigneur.
“Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana.
12 Et d'une mer à l'autre les hommes seront agités, et du nord au levant ils courront, cherchant la parole du Seigneur, et ils ne la trouveront pas.
Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Bwana, lakini hawatalipata.
13 En ce jour-là, les vierges les plus belles et les jeunes hommes tomberont de soif.
“Katika siku ile “wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
14 Ceux qui jurent par la propitiation de Samarie, et disent: Vive ton Dieu, Dan! vive ton Dieu, Bersabée! ceux-là tomberont et ne se relèveront plus.
Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”

< Amos 8 >