< Amos 7 >

1 Ceci est la vision que m'a envoyé le Seigneur Dieu; voilà une nuée de sauterelles qui vient de l'orient, et voilà de grandes sauterelles sur les champs du roi Gog.
Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
2 Et quand elles eurent achevé de dévorer l'herbe de la terre, je dis: Seigneur, Seigneur, sois miséricordieux. Qui relèvera Jacob? car il est réduit à rien.
Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
3 Seigneur, repens-Toi pour cela. Et cela ne sera point, dit le Seigneur.
Kwa hiyo Bwana akaghairi. Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”
4 Ceci est la vision que m'a envoyé le Seigneur: Voilà que le Seigneur appela le châtiment par la flamme, et le feu dévora une grande part de l'abîme, et il consuma l'héritage du Seigneur. Ceci est la vision que m'a envoyé le Seigneur
Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
5 Je dis: Seigneur, cesse donc; qui relèvera Jacob, car il est réduit à rien?
Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
6 Seigneur, repens-Toi pour cela. Et cela ne sera point, dit le Seigneur.
Kwa hiyo Bwana akaghairi. Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
7 Ceci est la vision que m'a envoyé le Seigneur: Voilà que le Seigneur Se tient debout sur un mur de diamant, et Il avait un diamant à la main.
Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
8 Et le Seigneur me dit: Que vois-tu, Amos? et je dis; Un diamant; et le Seigneur me dit: Voilà que Je mets un diamant sur un diamant entre Moi et Mon peuple d'Israël; Je ne continuerai plus de Me montrer à lui.
Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
9 Mais les autels de la division seront effacés; et les fêtes d'Israël seront délaissées; et Je Me lèverai avec le glaive contre la maison de Jéroboam.
“Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
10 Or Amasias, prêtre de Béthel, envoya au roi d'Israël Jéroboam, disant: Amos fait des complots contre toi, au milieu de la maison d'Israël; la terre ne pourrait pas souffrir toutes ses paroles.
Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
11 Car voilà ce que dit Amos: Jéroboam périra par le glaive, et Israël sera emmené captif hors de sa terre.
Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
12 Et Amasias dit à Amos: Ô Voyant, pars, retire-toi dans la terre de Juda; c'est là que tu vivras, et là que tu prophétiseras.
Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
13 Tu ne continueras plus de prophétiser en Béthel; c'est la ville sainte du roi, et la demeure royale.
Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
14 Et Amos répondit, et dit à Amasias: Je n'étais point prophète, ni fils de prophète, mais chevrier; et je cueillais des mûres.
Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
15 Et le Seigneur m'a pris au milieu de mon troupeau, et le Seigneur m'a dit: Pars et prophétise à Mon peuple Israël.
Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
16 Et maintenant écoute la parole du Seigneur: Tu dis: Ne prophétise point sur Israël, et n'ameute pas la foule contre la maison de Jacob.
Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema, “‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’
17 À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: Ta femme se prostituera dans la ville, et tes fils et tes filles périront par le glaive, et tes champs seront partagés au cordeau, et tu mourras en une terre impure, et Israël sera emmené captif hors de sa terre.
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”

< Amos 7 >