< Amos 3 >

1 Écoutez cette parole qu'a dite le Seigneur contre vous, ô maison d'Israël, et contre toute ta famille que J'ai ramené de la terre d'Égypte, disant:
Sikilizeni neno hili alilosema Bwana dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:
2 Hormis vous, Je n'ai connu aucune des tribus de la terre; et, à cause de cela, Je tirerai vengeance de vos péchés contre vous.
“Ni ninyi tu niliowachagua kati ya jamaa zote za dunia; kwa hiyo nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi zenu zote.”
3 Deux hommes peuvent-ils marcher d'accord en toutes choses, s'ils ne se connaissent l'un l'autre?
Je, watu wawili hutembea pamoja wasipokubaliana kufanya hivyo?
4 Le lion rugira-t-il en sa forêt, s'il n'a quelque proie? Le lionceau donnera-t-il de la voix en son antre, s'il n'a rien ravi?
Je, simba hunguruma katika kichaka wakati hana mawindo? Aweza kuvuma katika pango wakati ambao hajakamata chochote?
5 L'oiseau tombera-t-il à terre sans oiseleur? Détendra-t-on le filet avant qu'il ait rien pris?
Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini ambapo hajategewa chambo? Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini wakati ambapo hakuna chochote cha kunasa?
6 Sonnera-t-on de la trompette dans la ville sans que le peuple tremble, et y surviendra-t-il calamité qui ne soit envoyée par le Seigneur.
Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari, watu hawatetemeki? Mji upatwapo na maafa, je, si Bwana amesababisha?
7 Or le Seigneur ne fera rien qu'Il n'ait révélé Ses instructions à Ses serviteurs les prophètes.
Hakika Bwana Mwenyezi hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
8 Le lion rugira, et qui n'en sera pas épouvanté? Le Seigneur Dieu a parlé: qui ne prophétisera point?
Simba amenguruma: je, ni nani ambaye hataogopa? Bwana Mwenyezi ametamka: je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?
9 Faites des proclamations dans les villes des Assyriens, et dans les villes d'Égypte, et dites: Réunissez-vous en la montagne de Samarie, et voyez toutes les choses étranges qui se font au milieu d'elles, et l'oppression qui est en elles.
Tangazeni katika ngome za Ashdodi na katika ngome za Misri: “Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria; angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake, na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”
10 Elle n'a point connu ce qui allait arriver contre ses habitants, et ils thésaurisent en leurs maisons l'iniquité et la misère.
Bwana asema: “Hawajui kutenda lililo jema, wale ambao hujilundikia nyara na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”
11 À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur Dieu: Autour de toi, Tyr, on fera de ton territoire un désert; et ta puissance t'échappera, et tes champs seront dévastés.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Adui ataizingira nchi; ataangusha chini ngome zenu na kuteka nyara maboma yenu.”
12 Voici ce que dit le Seigneur: Tels, par le berger, sont arrachés de la gueule du lion deux jambes ou un lambeau d'oreille; tels seront arrachés les fils d'Israël qui demeureront en Samarie en face de la tribu du Jacob, et emmenés à Damas.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba vipande viwili tu vya mfupa wa mguu au kipande cha sikio, hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa, wale wakaao Samaria kwenye kingo za vitanda vyao, na katika Dameski kwenye viti vyao vya fahari.”
13 Prêtres, écoutez, et portez votre témoignage en la maison de Jacob, dit le Seigneur tout-puissant
“Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
14 Le jour où Je punirai sur lui-même les impiétés d'Israël, je tirerai vengeance des autels de Béthel. Et les cornes de l'autel seront abattues et tomberont à terre.
“Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake, nitaharibu madhabahu za Betheli; pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali na kuanguka chini.
15 Je renverserai et Je foulerai aux pieds la maison entourée de colonnes sur la maison d'été; et les maisons d'ivoire périront, et bien d'autres maisons seront enveloppées dans leur ruine, dit le Seigneur.
Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika, pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi; nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,” asema Bwana.

< Amos 3 >