< 2 Samuel 8 >
1 Il advint, après cela, que David battit les Philistins, et qu'il les mit en fuite. Et David leur imposa un tribut.
Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
2 Ensuite, David vainquit Moab; il fit coucher les captifs à terre, et il les fit mesurer par séries; il y en eu deux séries que l'on mit à mort et deux qui eurent la vie sauve. Moab resta asservi à David, et il lui paya un tribut.
Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
3 David vainquit aussi Adraazar, fils de Rhaab, roi de Suba, qui s'était mis en campagne pour se rendre maître des rives de l'Euphrate.
Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
4 David lui prit mille chars, sept mille cavaliers et vingt mille piétons. Il énerva les attelages de tous les chars, sauf une centaine qu'il garda pour lui.
Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
5 Alors, les Syriens de Damas s'avancèrent pour porter secours à Adraazar, roi de Suba, et David tua aux Syriens vingt-deux mille hommes.
Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
6 Puis, il mit une garnison dans la Syrie de Damas; le Syrien lui fut asservi, et il lui paya un tribut. Ainsi, le Seigneur protégea David partout où il porta ses armes.
Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
7 Et David prit les bracelets d'or que portaient les serviteurs d'Adraazar, roi de Suba, et il les consacra dans Jérusalem. Sésac, roi d'Égypte, s'en empara lorsqu'il entra à Jérusalem, au temps de Roboam, fils de Salomon.
Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
8 David recueillit, à Métébac et dans les principales villes d'Adraazar, une prodigieuse quantité d'airain, dont Salomon se servit pour fabriquer la mer d'airain, les colonnes, les piscines et tous les vases du temple.
Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
9 Thu, roi d'Hémath, ayant appris que David avait taillé en pièces toute l'armée d'Adraazar,
Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
10 Envoya vers David son fils Jedduram pour lui demander la paix et le féliciter de sa victoire sur Adraazar, car il était son ennemi. Et Jedduram apporta au roi David des vases d'argent, des vases d'or et des vases d'airain.
akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
11 Et le roi David les consacra au Seigneur; comme il consacra l'argent et l'or de toutes les villes conquises,
Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
12 Tant de l'Idumée, que de Moab, des fils d'Ammon, des Philistins, d'Amalec et d'Adraazar, fils de Rhaab, roi de Suba.
yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
13 David s'était donc fait un grand renom, et, à son retour, il écrasa Gébélem à l'Idumée qui avait levé dix-huit mille hommes.
Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
14 Et il mit des garnisons dans l'Idumée entière, et tous les Iduméens furent asservis au roi. Ainsi, le Seigneur en toutes ses guerres avait protégé David.
Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
15 David régna sur tout Israël, et il rendit bonne justice à tout son peuple.
Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
16 Et Joab, fils de Sarvia, commandait l'armée; Josaphat, fils d'Achilud, recueillait les actes publics.
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
17 Sadoc, fils d'Achitob, et Achimélech, fils d'Abiathar, étaient prêtres, et Sasa, scribe.
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
18 Banaïas, fils de Joad, était conseiller; Chéléthi, Phéléthi, et les fils de David étaient maîtres du palais.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.