< 2 Samuel 7 >

1 Après que le roi se fut établi en sa demeure, et que le Seigneur lui eut donné l'héritage de tous les ennemis qui l'entouraient, ceci arriva:
Baada ya mfalme kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, naye Bwana akiwa amemstarehesha pande zote mbali na adui zake,
2 Le roi dit à Nathan le prophète: Voilà que j'habite une maison de cèdre, tandis que l'arche du Seigneur repose au milieu d'un tabernacle. De son manteau royal.
akamwambia nabii Nathani, “Mimi hapa, ninaishi katika jumba la kifalme la mierezi, wakati Sanduku la Mungu limebaki katika hema.”
3 Nathan répondit au roi: Tout ce qui est en ton cœur, va, et fais-le, parce que le Seigneur est avec toi.
Nathani akamjibu mfalme, “Lolote ulilo nalo moyoni, endelea ukalifanye, kwa maana Bwana yu pamoja nawe.”
4 Mais cette nuit même, la parole du Seigneur vint à Nathan, et lui dit:
Usiku ule neno la Bwana likamjia Nathani, kusema:
5 Va, et dis à mon serviteur David: Voici ce que dit le Seigneur: Tu ne me bâtiras point un temple pour que je l'habite,
“Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ewe ndiwe wa kunijengea mimi nyumba ili nikae ndani yake?
6 Parce que je n'ai point résidé dans un temple depuis que j'ai tiré de l'Égypte les fils d'Israël jusqu'à ce jour, et qu'en marchant je me tenais abrité sous un tabernacle.
Sijakaa ndani ya nyumba tangu siku niliyowaleta Waisraeli kutoka Misri hadi leo. Nimekuwa nikitembea kutoka mahali pamoja hadi mahali pengine ndani ya hema kama makao yangu.
7 En quelque lieu que j'aie passé, avec tout Israël, ai-je jamais dit, à celle des tribus que j'avais chargée de prendre 'soin de tout le peuple: Pourquoi ne m'avez-vous point bâti une maison de cèdre?
Popote nilipotembea pamoja na Waisraeli wote, je, nimewahi kumwambia kiongozi wao yeyote niliyemwamuru kuwachunga watu wangu Israeli, “Kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?”’
8 Dis encore à mon serviteur David: Voici ce que dit le Seigneur tout- puissant: Je t'ai tiré des bergeries pour que tu sois roi de mon peuple Israël.
“Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikutoa wewe kutoka machungani na kutoka kuandama kundi la kondoo na mbuzi ili kuwaongoza watu wangu Israeli.
9 Je t'ai accompagné partout où tu as marché, j'ai exterminé devant toi tous tes ennemis, et je t'ai rendu célèbre autant que les plus renommés des grands de la terre.
Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
10 Et j'adopterai un lieu pour mon peuple Israël; je l'y fixerai, et il s'y abritera; chacun aura sa demeure, et il ne sentira plus d'inquiétudes, et le fils de l'iniquité ne l'affligera plus comme il a fait dès le commencement,
Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali niwapande humo ili kwamba wawe na nyumbani kwao wenyewe wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
11 Depuis les temps où j'ai donné des juges à mon peuple. Et je t'affranchirai de tous tes ennemis, et le Seigneur te fera savoir qu'il te formera une maison.
na kama walivyofanya tangu mwanzo wakati nilipowaweka viongozi juu ya watu wangu Israeli. Pia nitawapa raha mbele ya adui zenu wote. “‘Bwana akuambia kwamba Bwana mwenyewe atakujengea nyumba.
12 Et quand tes jours seront remplis, quand tu te seras endormi avec tes pères, j'élèverai après toi ta race, j'élèverai celui qui sera issu de ton sang, et je préparerai son règne.
Siku zako zitakapokwisha nawe ulale pamoja na baba zako, nitainua mzao wako aingie mahali pako, ambaye atatoka viunoni mwako, nami nitauimarisha ufalme wake.
13 Celui-là bâtira un temple en mon nom; je dresserai son trône pour toujours.
Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, nami nitaimarisha kiti cha enzi cha ufalme wake milele.
14 Je serai pour lui un père, et il sera pour moi un fils; et, si une iniquité provient de lui, je le châtierai avec la verge qui châtie les hommes; je lui porterai les coups que l'on porte aux fils des hommes.
Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Atakapokosea nitamwadhibu kwa fimbo ya wanadamu, kwa adhabu ya kupigwa na wanadamu.
15 Mais je ne lui retirerai point ma miséricorde, comme je l'ai retirée à ceux qui se sont éloignés de moi.
Lakini upendo wangu kamwe hautaondolewa kwake, kama nilivyouondoa kwa Sauli, niliyemwondoa atoke mbele yako.
16 Et sa maison sera une maison sûre, et, devant moi, sa royauté subsistera à jamais; et son trône sera toujours debout.
Nyumba yako na ufalme wako utadumu milele mbele zangu, kiti chako cha enzi kitafanywa imara milele.’”
17 Ainsi, Nathan répéta à David toutes les paroles que lui-même avait ouïes en sa vision.
Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
18 Alors, le roi David entra devant le Seigneur, et il dit: Qui suis-je, Seigneur, mon Seigneur, et qui est ma maison, pour que vous m'aimiez à ce point?
Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Ee Bwana Mwenyezi, mimi ni nani, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
19 J'étais bien petit devant vous, Seigneur, mon Seigneur, et vous m'avez parlé de la maison de votre serviteur pour un avenir lointain; Seigneur, mon Seigneur, les hommes ont-ils une telle loi?
Naam, kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Bwana Mwenyezi, wewe umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Je, hii ndiyo njia yako ya kawaida ya kushughulika na mwanadamu, Ee Bwana Mwenyezi?
20 Et que pourrait David vous dire encore? Vous connaissez maintenant votre serviteur, ô Seigneur! mon Seigneur.
“Je, Daudi aweza kukuambia nini zaidi? Kwa maana unamjua mtumishi wako, Ee Bwana Mwenyezi.
21 Vous avez agi pour l'amour de votre serviteur, et selon votre cœur vous avez opéré ces grandes choses afin que votre serviteur les connaisse,
Kwa ajili ya neno lako na kwa mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa na kulifanya lijulikane na lifahamike kwa mtumishi wako.
22 Et qu'il vous glorifie, mon Seigneur; car nul ne vous ressemble, nul que vous n'est Dieu parmi tous ceux dont nos oreilles ont entendu parler.
“Tazama jinsi ulivyo mkuu, Ee Bwana Mwenyezi! Hakuna mwingine kama wewe, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe,
23 Et quelle autre nation sur la terre est comme le peuple d'Israël, que vous avez guidé, racheté et fait votre peuple, pour qu'il divulgue votre nom, pour qu'il agisse avec éclat et grandeur, de telle sorte que vous chassiez les nations et leurs tabernacles devant le peuple que vous avez tiré de l'Égypte afin qu'il soit à vous?
Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli, taifa pekee duniani ambalo Mungu alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe, na kujifanyia jina mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa na miungu yao mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
24 Car, vous avez préparé pour vous-même le peuple d'Israël; il sera votre peuple à jamais; et vous, Seigneur, vous êtes son Dieu.
Umeimarisha watu wako Israeli hasa kama watu wako mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana, umekuwa Mungu wao.
25 Et maintenant, mon Seigneur, confirmez la parole que vous avez dite concernant votre serviteur et sa maison, Seigneur tout-puissant, Dieu d'Israël; maintenant donc, comme vous avez dit:
“Basi sasa, Bwana, ukaitimize ahadi uliyosema kuhusu mtumishi wako na nyumba yake milele. Fanya kama ulivyoahidi,
26 Que votre nom soit glorifié à jamais.
ili kwamba jina lako litukuke milele. Ndipo watu watasema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ni Mungu juu ya Israeli!’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itakuwa imara mbele zako.
27 Seigneur tout-puissant, Dieu d'Israël, vous avez révélé vos desseins à votre serviteur, disant: Je te bâtirai une maison. A cause de cela votre serviteur a trouvé dans son cœur cette prière qu'il vous adresse.
“Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, umelifunua hili kwa mtumishi wako, ukisema, ‘Nitakujengea nyumba.’ Hivyo mtumishi wako amepata ujasiri kukuletea dua hii.
28 Et maintenant, Seigneur, mon Seigneur, vous êtes Dieu, et vos paroles seront vraies, c'est vous qui avez dit ces excellentes paroles concernant votre serviteur.
Ee Bwana Mwenyezi, wewe ndiwe Mungu! Maneno yako ndiyo kweli, nawe umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
29 Commencez donc; et bénissez la maison de votre serviteur pour qu'elle subsiste toujours devant vous, car Seigneur, mon Seigneur, vous l'avez promis; ainsi la maison de votre serviteur sera bénie, et bénie pour exister à jamais.
Sasa naomba uwe radhi kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu mbele zako milele, kwa maana wewe, Ee Bwana Mwenyezi, umesema, na kwa baraka zako nyumba ya mtumishi wako itaendelea kubarikiwa milele.”

< 2 Samuel 7 >