< 2 Samuel 23 >

1 Voici les dernières paroles de David, du fidèle David, fils de Jessé, de l'homme fidèle que le Seigneur a suscité pour être le christ du Dieu de Jacob, et dont les psaumes ont été agréables au Seigneur.
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
2 L'Esprit du Seigneur m'a parlé, sa parole est sur ma langue.
“Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
3 Le Dieu d'Israël parle. Le gardien d'Israël me propose une parabole: J'ai fait, dit-il, cette question aux hommes: Comment vous affermirez-vous dans la crainte de l'oint du Seigneur?
Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
4 Qu'au sein de la lumière matinale de Dieu, ajoute-t-il, l'on voie se lever le soleil. La splendeur du Seigneur ne s'efface point; elle naît comme l'herbe des champs naît de la pluie.
yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
5 Ainsi n'est point ma maison devant le Tout-Puissant; mais il a fait avec moi une alliance perpétuelle, toujours efficace, et, en tout temps, observée; et c'est là tout mon salut; tout mon désir est en elle, et les méchants ne fleuriront pas.
“Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
6 Tous sont comme l'épine méprisée que l'on ne prend pas avec la main.
Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
7 L'homme ne se fatiguera pas à son sujet. On y emploiera le fer et le bois de la lance, et elle sera brûlée; eux aussi seront brûlés dans leur opprobre.
Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
8 Voici les noms des hommes vaillants de David: Isboseth le Chananéen, chef de la première triade; Adinon l'Asonien, qui, un jour, tira l'épée contre huit cents hommes à la fois.
Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
9 Après lui, Eléanan, fils de son oncle paternel, fils de Dudi, de l'un des trois vaillants qui accompagnaient David. Un jour, Dudi insulta les Philistins; ils se réunirent pour livrer bataille, Israël s'avança.
Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
10 Et lui se leva, et tailla en pièces les Philistins jusqu'à ce que sa main fût fatiguée; et sa main ne put se détacher de son glaive. Et le Seigneur, ce jour-là, sauva son peuple d'un grand péril; l'armée revint vers Dudi, et elle n'eut plus qu'à dépouiller les morts.
lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
11 Après Eléanan, Samaïa, fils d'Asa, l'Aruchéen. Les Philistins s'étaient rassemblés dans Théria; et il y avait là un champ de lentilles, et devant eux l'armée d'Israël s'était enfuie.
Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
12 Et il demeura comme une colonne au milieu du champ, et il le reprit, et il tailla en pièces les Philistins. Et le Seigneur sauva son peuple d'un grand péril.
Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
13 Les trois premiers des trente avaient rejoint jadis en Cason David à la caverne d'Odollam, et les Philistins en armes étaient campés dans le val des Géants.
Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
14 David se tenait dans sa forteresse, et les Philistins avaient un poste à Bethléem.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
15 Et David eut un désir, et il dit: Qui m'apportera à boire de l'eau de la citerne qui est sous la porte de Bethléem? Or, en ce temps-là, le gros des Philistins était à Bethléem.
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
16 Aussitôt, les trois vaillants s'ouvrirent un passage à travers le camp des Philistins, et ils puisèrent de l'eau dans la citerne sous la porte de Bethléem, et ils l'emportèrent, et ils la présentèrent à David; mais il ne voulut pas la boire, et il en fit une libation au Seigneur.
Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
17 Et il dit: Dieu me préserve d'en rien faire; je croirais boire le sang des hommes qui ont exposé leur vie. Et il ne voulut point boire. Voilà ce qu'avaient fait les trois vaillants.
Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
18 Il y avait encore Abessa, frère de Joab, fils de Sarvia, chef d'une seconde triade; seul, il avait levé sa javeline contre trois cents qui périrent; et il s'était fait un nom parmi les trois.
Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
19 Et, dans sa triade, il fut illustre, et il en devint le chef; mais il n'alla pas si loin que ceux de la première triade.
Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
20 Et il y avait Banaïas de Cabeséel, fils de Joad, homme distingué aussi par ses actions; seul, il tua deux fils d'Ariel de Moab; ce fut lui qui descendit dans une citerne, un jour de neige, et qui y tua un lion.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
21 Il tua encore un Égyptien de grande taille, et l'Égyptien tenait une javeline haute comme une échelle; il l'attaqua n'ayant qu'un bâton; il la lui arracha, et s'en servit pour le tuer.
Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
22 Voilà ce que fit Banaïas, et il avait un nom dans la seconde triade.
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
23 Et, dans sa triade, il fut illustre; mais il n'alla pas si loin que ceux de la première triade. David le fit son conseiller. Voici les noms des autres hommes vaillants du roi David:
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
24 Asaël, frère de Joab, l'un des trente; Eléanan, fils de Dudi, de Bethléem, oncle paternel du premier.
Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
25 Séma le Rhudéen;
Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
26 Sellès le Celothi; Iras, fils d'Isca, de Thecoé;
Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
27 Abiézer l'Anothite, des fils de l'Anothite;
Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
28 Ellon l'Aoïte; Noré le Netophatite;
Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
29 Esthai, fils de Riba, de Gabaeth; Ephratéen, fils de Benjamin; Asmoth le Bardiamite;
Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
30 Emasa le Salabonite; Jonathan, fils d'Asan;
Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
31 Samnan l'Arodite; Amnan, fils d'Araï le Saraürite;
Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
32 Aliphaleth, fils d'Asbite, fils de Machachachi; Héliab, fils d'Achitophel le Gélonite;
Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
33 Asaraï du Carmel, fils d'Uréoërchi;
mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
34 Gaal, fils de Nathan; Bonni, fils de Galaadi; Héli l'Ammanite;
Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
35 Adroï des torrents;
Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
36 Gadabiel, fils de l'Arabothaïte;
Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
37 Geloré de Béthoron, qui portait les armes de Joab, fils de Sarvia;
Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
38 Iras l'Ethéréen; Gérab l'Ethénéen;
Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
39 Urie l'Hettéen: en tout trente-sept.
na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.

< 2 Samuel 23 >