< 2 Samuel 20 >

1 Et il y avait là, parmi les hommes inculpés, un homme pervers; il se nommait Sabé, fils de Bochori, de la famille de Jémini; il sonna du cor, et il dit: Nos champs ne dépendent point de David; nous ne tenons pas notre héritage du fils de Jessé. Israël, que chacun de nous retourne sous sa tente.
Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
2 Et tous ceux d'Israël qui suivaient David s'en allèrent avec Sabé, fils de Bochori; et ceux de Juda se serrèrent autour de leur roi, depuis le Jourdain jusqu'à Jérusalem.
Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
3 Et le roi rentra en sa demeure à Jérusalem; là, il prit ses dix concubines qu'il avait laissées pour garder le palais, les fit renfermer et les pourrit; mais il ne s'approcha plus d'elles, et elles furent recluses jusqu'au jour de leur mort, vivant comme des veuves.
Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
4 Après cela, le roi dit à Amessaï: Fais-moi venir dans trois jours les hommes de Juda, et reviens ici.
Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
5 Et Amessaï partit pour convoquer Juda; mais il tarda plus que ne le lui avait prescrit David.
Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
6 Et David dit à Abessa: Maintenant Sabé, fils de Bochori, va nous faire plus de mal qu'Absalon; prends donc avec toi les serviteurs de ton maître, et poursuis-le, avant qu'il ait trouvé quelque ville forte, car alors il obscurcirait nos yeux.
Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
7 Et Abessa sortit pour le poursuivre avec les hommes de Joab, et Chéléthi, et Phéléthi et tous les vaillants; tous sortirent de Jérusalem afin de poursuivre Sabé, fils de Bochori.
Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
8 Ils étaient vers la grande pierre que l'on voit en Gabaon, quand Amessaï arriva devant l'armée. Joab avait une casaque sur son vêtement, et par-dessus la ceinture, une dague dont le fourreau était attaché le long de sa hanche; cette dague n'était pas plutôt tirée qu'elle frappait.
Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
9 Et Joab dit à Amessaï: Es-tu en bonne santé, mon frère? En même temps, de la main droite, il lui prit la barbe pour l'embrasser.
Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
10 Amessaï ne prit point garde à la dague que Joab tenait à la main; celui- ci le frappa au ventre; les entrailles se répandirent à terre, et il ne lui porta pas un second coup, car il était mort; puis Joab, avec son frère Abessa, se mit à la poursuite de Sabé, fils de Bochori.
Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
11 Cependant, un serviteur de Joab s'arrêtant près du corps d'Amessaï, dit: Qui veut Joab; qui est pour David, et veut suivre Joab?
Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
12 Et Amessaï, baigné dans son sang, gisait au milieu du chemin, quand un homme, voyant que toute l'armée s'arrêtait, traîna le corps dans un champ voisin, et le couvrit d'un manteau, parce qu'il avait remarqué que chacun s'arrêtait auprès de lui.
Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
13 Aussitôt qu'il l'eut retiré du chemin, tout Israël passa, et se mit avec Joab à la poursuite de Sabé, fils de Bochori.
Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
14 Celui-ci, à travers toutes les tribus d'Israël, atteignit Abel et Bethmacha; à ce moment, tous ceux de Charrhi étaient rassemblés, et ils le suivirent.
Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
15 On le rejoignit, on l'assiégea dans Abel et Permacha; on l'entoura de terrasses qu'on poussa jusqu'aux remparts; et toute l'armée de Joab se préparait à les saper.
Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
16 Quand une femme expérimentée cria du haut de la muraille: Écoutez, écoutez, dites à Joab qu'il approche, j'ai à lui parler.
mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
17 Il s'approcha d'elle, et la femme dit: Es-tu Joab? Je le suis, dit-il; et elle reprit: Écoute un mot de ta servante. Il répliqua: Je t'écoute.
Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
18 Alors, elle dit: Il y avait un proverbe chez nos pères; lorsque parmi les fidèles d'Israël, un de leurs desseins venait à manquer, on disait: Il faut consulter et consulter à Abel ou à Dan. Maintenant tes hommes consultent et consultent en Abel, après avoir, eux aussi, défailli.
Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
19 Or, Abel te répond: Je suis pacifique parmi les appuis d'Israël, et toi, tu cherches à faire périr une ville et une métropole d'Israël; pourquoi veux- tu jeter dans l'abîme l'héritage du Seigneur?
Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
20 Et Joab prit la parole, et il dit: Dieu me soit propice, qu'il me soit propice, je ne veux ni abîmer, ni détruire.
Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
21 Ce n'est point de cela qu'il s'agit, mais un homme des montagnes d'Ephraïm qui se nomme Sabé, fils de Bochori, a levé la main contre le roi David. Livrez-moi celui-là seul, et je m'éloignerai soudain de la ville. Et la femme dit à Joab: Voilà que sa tète va tomber devant toi du haut de la muraille.
Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
22 Aussitôt, la femme entra à l'assemblée du peuple, et elle parla sagement à toute la ville. On trancha la tête de Sabé, fils de Bochori, et on la jeta devant Joab; celui-ci fit sonner du cor; l'armée se dispersa, chacun retourna en sa demeure. Et Joab revint à Jérusalem auprès du roi.
Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
23 Joab commandait toute l'armée d'Israël; Banaïas, fils de Joiada, avait sous ses ordres Chéléthi et Phéléthi.
Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
24 Adoniram était intendant des impôts, et Josaphath, fils d'Achilud, garde des actes publics.
Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
25 Susa était scribe, Sadoc et Abiathar, prêtres.
Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
26 Iras, fils d'Iarin, était prêtre de David.
na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.

< 2 Samuel 20 >