< 2 Samuel 2 >

1 Après cela, David consulta le Seigneur, disant: Irai-je en l'une des villes de Juda? Et le Seigneur lui répondit: Va. Et David demanda: Où irai- je? A Hébron, reprit le Seigneur.
Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
2 Et David partit pour Hébron, avec ses deux femmes Achinoam la Jezraélite et Abigaïl, femme de Nabal du Carmel,
Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
3 Et avec ses hommes, chacun emmenant sa famille; ainsi, ils habitèrent les villes d'Hébron.
Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
4 Alors, des hommes de la Judée vinrent, et ils sacrèrent David pour qu'il régnât sur la tribu de Juda; ces hommes lui apprirent que ceux de Jabès-Galaad avaient inhumé Saül.
Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
5 Et David envoya des messagers aux chefs de Jabès-Galaad, et il leur dit: Bénis soyez-vous par le Seigneur, parce que vous avez été miséricordieux envers votre maître, envers Saül l'oint du Seigneur, et que vous l'avez inhumé, lui et son fils Jonathan.
akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
6 Que le Seigneur vous traite selon sa miséricorde et sa vérité; pour moi, j'en userai bien avec vous, parce que vous avez bien agi.
Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
7 Et maintenant que vos mains soient fortes; soyez vaillants vous-mêmes; car votre maître Saül n'est plus, et la maison de Juda m'a sacré, afin que je règne sur elle.
Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
8 Mais, Abner, fils de Ner, général de Saül, prit Isboseth, fils de Saül, et il l'emmena du camp de Manaam,
Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
9 Et il le fit reconnaître roi par la contrée de Galaad, par Thasiri, par Jezraël, par Ephrahn, par Benjamin, par tout Israël.
Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
10 Isboseth, fils de Saül, avait quarante ans lorsqu'il devint roi d'Israël; il régna deux ans, hormis sur la maison de Juda, qui obéissait à David.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
11 Et David régna à Hébron sur la maison de Juda, sept ans et demi.
Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
12 Cependant, Abner, fils de Ner, et les serviteurs d'Isboseth, fils de Saül, s'en allèrent de Manaam en Gabaon.
Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
13 De son côté, Joab, fils de Sarvia, avec la troupe de David, sortit d'Hébron, et il arriva en même temps qu'eux vers la fontaine de Gabaon; ils campèrent les uns en deçà, les autres au delà de la fontaine.
Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
14 Et Abner dit à Joab: Que ces jeunes gens se lèvent et qu'ils viennent jouer devant nous; à quoi Joab répondit: Qu'ils se lèvent.
Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
15 Et douze des serviteurs d'Isboseth, fils de Saül, tous de la tribu de Benjamin, se portèrent à la rencontre de douze serviteurs de David.
Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
16 Et chacun saisit d'une main la tête de celui qui lui faisait face, puis, de l'autre main, il lui enfonça dans le flanc son épée, et ils tombèrent tous en même temps. Et l'on appela ce lieu qui est en Gabaon, le Champ des Traîtres.
Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
17 Ce jour-là, il y eut une terrible bataille; Abner et les hommes d'Israël échouèrent devant les serviteurs de David.
Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
18 Il se trouvait là trois fils de Sarvia, Joab, Abessa et Asaël; or, Asaël avait les pieds légers comme un daim libre dans les champs.
Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
19 Et Asaël se lança à la poursuite d'Abner; il s'attacha à ses pas, sans s'écarter à droite ni à gauche.
Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
20 Abner regardant derrière lui, s'écria: N'es-tu pas Asaël? l'autre reprit: Je le suis.
Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
21 Abner lui dit: Détourne-toi à droite ou à gauche, attaque l'un des jeunes serviteurs, et prends pour toi ses armes. Mais Asaël refusa de s'écarter ni à droite ni à guiche.
Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
22 Abner continua de lui parler, disant: Éloigne-toi donc de moi, de peur que d'un coup je ne t'étende à terre; comment alors oserais-je lever les yeux devant Joab?
Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
23 Où en veux-tu venir? Retourne vers Joab, ton frère. Mais il ne voulut pas s'éloigner, et Abner le frappa du bas de sa javeline au ventre, la pointe ressortit par les reins. Asaël tomba, et il mourut en s'affaissant sur lui-même; tous ceux qui arrivèrent au lieu où il était mort s'arrêtèrent autour de lui.
Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
24 Et Joab et Abessa s'élancèrent à la poursuite d'Abner; le soleil se couchait alors; et ils allèrent jusqu'à la colline d'Amma, qui est en face d'Haï, où monte le chemin du désert de Gabaon.
Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
25 Mais les fils de Benjamin, s'étant ralliés auprès de la troupe d'Abner, ne formaient plus qu'un seul corps; ils se rangèrent sur la crête d'une colline.
Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
26 Et Abner appela Joab, et il lui dit: Est-ce que l'épée dévorera sans relâche? Ne sais-tu pas qu'elle peut devenir amère à la fin? Qu'attends-tu donc pour ordonner aux tiens de ne plus poursuivre nos frères?
Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
27 Et Joab répondit: Vive le Seigneur! si tu n'avais parlé, aucun des nôtres qui, depuis le matin, poursuivent leurs frères, ne se fût arrêté.
Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
28 Et Joab sonna de la trompette, et toute l'armée s'arrêta; elle ne poursuivit plus Israël, et le combat finit.
Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
29 Partis le soir même, Abner et ses hommes marchèrent toute la nuit; ils traversèrent le Jourdain, le côtoyèrent et rentrèrent dans leur camp.
Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
30 Joab revint sur ses pas, laissant partir Abner; il rassembla tout le peuple, et il vit que des serviteurs de David, il manquait dix-neuf hommes outre Asaël.
Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
31 Et les serviteurs de David avaient tué trois cent soixante des fils de Benjamin, qui accompagnaient Abner.
Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
32 Et ils emportèrent le corps d'Asaël pour l'ensevelir à Bethléem, dans le sépulcre de son père; Joab et ses hommes marchèrent aussi toute la nuit; le jour paraissait quand ils arrivèrent à Hébron.
Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.

< 2 Samuel 2 >