< 2 Samuel 13 >
1 Voici ce qui advint ensuite: Absalon, fils de David, avait une sœur extrêmement belle; elle se nommait Thamar, et Amnon, fils de David, l'aimait.
Ikawa baada ya hayo kwamba Amnoni mwana wa Daudi, akamtamani sana Tamari dada yake wa kambo aliyekuwa mzuri, alikuwa tumbo moja na Absalome, mwana wingine wa Daudi.
2 Amnon souffrait au point de dépérir, à cause de Thamar sa sœur; car elle était vierge, et il lui semblait téméraire de rien tenter auprès d'elle.
Amnoni akasononeka sana kiasi cha kuugua kwa ajili ya Tamari dada yake. Tamari alikuwa bikra, na hivyo ilionekana haiwezekani Amnoni kufanya neno lolote kwake.
3 Amnon avait un compagnon nommé Jonadab, fils de Samaa, frère de David; or, Jonadab était un homme très rusé.
Lakini Amnoni alikuwa na rafiki jina lake Yehonadabu mwana wa Shama, nduguye Daudi.
4 Il dit donc à Amnon: Qu'as-tu, ô fils du roi! pour que tu t'affaiblisses ainsi de jour en jour? Ne me le confieras-tu point? Amnon lui répondit: J'aime Thamar, la sœur de mon frère Absalon.
Yehonadabu alikuwa mtu mwelevu sana. Akamwambia Amnoni, “Kwa nini, mwana wa mfalme, unadhoofika kila siku? Kwa nini uniambii? Ndipo Amnoni akamjibu, “Nampenda Tamari, dada yake Absalome ndugu yangu.”
5 Jonadab lui dit: Mets-toi au lit, et fais-toi malade; ton père viendra te voir, et tu lui diras: Que Thamar, ma sœur, vienne; qu'elle me coupe mes bouchées, qu'elle prépare sous mes yeux des aliments, afin que je la voie faire, et que je mange de sa main.
Ndipo Yehonadabu akamwambia, “Lala kitandani mwako na ujifanye kuwa mgonjwa. Wakati baba yako atakapo kuja kukuona, mwambie, Tafadhari mtume dada yangu Tamari aandaye chakula mbele yangu, ili kwamba nikione na kula kutoka mkononi mwake?”
6 Amnon se mit au lit, et se fit malade; son père l'alla voir, et Amnon lui dit: Que Thamar, ma sœur, vienne auprès de moi; qu'elle fasse cuire devant moi deux petits gâteaux, et je mangerai de sa main.
Hivyo Amnoni akalala na kujifanya kuwa mgonjwa. Mfalme alipokuja kumwona, Amnoni akamwambia mfalme, “Tafadhari mtume Tamari dada yangu aandaye chakula kwa ajili ya ugonjwa wangu mbele yangu ili kwamba nikile kutoka mkononi mwake.
7 Et David chercha Thamar dans la maison, et il lui dit Va-t'en chez ton frère, et prépare-lui à manger.
Ndipo Daudi katika kasri lake akatuma neno kwa Tamari, kusema, “Nenda katika nyumba ya nduguyo Amnoni na umwandalie chakula. Hivyo
8 Et Thamar alla à la maison d'Amnon, son frère, quand il était couché. Elle prit de la pâte, la pétrit, et en fit sous ses yeux de petits gâteaux qu'elle mit cuire.
Tamari akaenda katika nyumba ya Amnoni nduguye alipokuwa amelala. Akachukua donge na kulifinyanga na kuandaa mkate mbele zake, kisha akauoka.
9 Ensuite, elle prit la poêle, et elle la vida devant lui; mais il ne voulut pas manger, et il dit: Que l'on fasse sortir tous les hommes qui sont debout ici. Tout le monde s'en alla.
Akachukua kikaangio na kumpa mkate, lakini akakataa kula. Kisha Amnoni akawambia waliokuwepo, “Kila mtu na aondoke.” Hivyo kila mmoja akaondoka.
10 Et Amnon dit à Thamar: Apporte-moi auprès de mon lit ma nourriture, et je mangerai de ta main; Thamar prit donc les gâteaux qu'elle avait préparés, et elle les porta à son frère Amnon vers son lit.
Amnoni akamwambia Tamari, “Lete chakula chumbani kwangu nikile katika mkono wako.” Tamari akachukua mkate aliokuwa ameuandaa, na kuuleta katika chumba cha Amnoni kaka yake.
11 Elle l'engagea à manger, et il la saisit, et il lui dit: Viens, dors avec moi, ma sœur.
Alipoleta chakula kwake, Amnoni akamshikilia na kumwambia, “Njoo, ulale nami, dada yangu.”
12 Et elle lui dit: Mon frère, ne m'avilis pas; car pareille chose ne doit pas se faire en Israël; ne fais pas cette folie.
Yeye akamjibu, “Hapana, kaka yangu, usinilazimishe, kwani hakuna jambo kama hili linapaswa kufanyika katika Israeli. Usifanye jambo la aibu kiasi hiki!
13 Comment supporterais-je mon opprobre? Et toi, tu passerais pour un insensé en Israël. Parle plutôt à mon père; il ne m'éloignera pas de toi.
Nitakwenda wapi ili nijiepushe na aibu ambayo jambo hili litaileta juu ya maisha yangu? Na tendo hili litakuonesha kuwa mpumbavu usiye na aibu katika Israeli yote. Tafadhari, ninakuomba uongee na mfalme. Yeye atakuruhusu unioe.”
14 Mais Amnon ne voulut rien entendre; il fut plus fort qu'elle; il l'humilia, et il dormit avec elle.
Lakini Amnoni hakuweza kumsikiliza. Kwa kuwa alikuwa zaidi akamkamata na akalala naye.
15 Et Amnon la prit soudain en grande haine, et sa haine l'emporta sur l'amour qu'il avait auparavant; car sa dernière méchanceté fut plus grande que la première. Amnon lui dit donc: Lève-toi, et va-t'en.
Kisha Amnoni akamchukia Tamari kwa chuki kuu. Akamchukia zaidi ya jinsi alivyokuwa amemtamani. Amnoni akamwambia, “Inuka na uondoke.”
16 Thamar lui parla au sujet de cette grande méchanceté qu'il faisait en la chassant; plus grande, dit-elle, que la première; mais Amnon ne voulut rien entendre.
Lakini yeye akamjibu, “Hapana! kwa maana uovu wa kunifanya ni uondoke ni mbaya zaidi ya kile ulichonitenda!” Lakini Amnoni hakumsikiliza.
17 Et il appela le serviteur qui se tenait à l'entrée de l'appartement, et il lui dit: Chasse-moi d'ici cette femme, et ferme la porte sur elle.
Badala yake, akamwita mtumishi wake na akasema, “Mwondoe mwanamke huyu mbele yangu, na uufunge mlango nyuma yake.”
18 Elle avait un vêtement à longues manches comme en portaient les filles du roi qui étaient vierges. Et le serviteur la mit dehors, puis il ferma la porte sur elle.
Hivyo mtumishi wake akamtoa na kufunga mlango. Tamari alikuwa amevaa vazi lilinakishiwa kwani ndivyo binti za wafalme waliobikra valivyokuwa wakivaa.
19 Et Thamar prit de la cendre, s'en couvrit la chevelure, déchira son vêtement à longues manches, croisa les mains sur sa tête, et s'en alla, jetant les hauts cris.
Tamari akaweka majivu juu ya kichwa chake na akalirarua vazi lake
20 Absalon, son frère, lui dit: Est-ce qu'Amnon, ton frère, a été avec toi? Alors, ma sœur, sois muette, car c'est ton frère. Ne prends pas à cœur d'ébruiter cette affaire. Ainsi Thamar demeura, comme une veuve, en la maison de son frère Absalon.
Absalome, kaka yake, akamwambia, “Amnoni, kaka yako, amekuwa nawe? Lakini sasa nyamaza, dada yangu. Yeye ni kaka yako. Usiliweke hili moyoni.” Hivyo Tamari akakaa peke yake katika nyumba ya Absalomu kaka yake.
21 Le roi David apprit tout, et il en fut violemment courroucé, mais il ne chagrina point Amnon; car il l'aimait, parce que c'était son premier-né.
Mfalme Daudi aliposikia haya yote, alikasirika sana.
22 Quant à Absalon, il ne dit mot à son frère, ni en bien ni en mal; mais il le prit en haine pour avoir avili Thamar, sa sœur.
Absalome hakusema chochote kwa Amnoni, kwa maana Absalome alimchukia kwa kile alichokifanya, kumdhalilisha Tamari, dada yake.
23 Et ceci advint: au bout de deux années, on faisait la tonte pour Absalon en Belasor, sur le territoire d'Ephraïm, et Absalon invita tous les fils du roi.
Ikawa baada ya miaka miwili mizima Absalomu akawa na wakatao kondoo manyoya wakifanya kazi huko Baali Hazori, ulioko karibu na Efraim, naye Absalomu akawaarika wana wote wa mfalme kufika huko.
24 Absalon, d'abord, alla trouver le roi, et lui dit: Voilà que l'on fait la tonte pour ton serviteur, que le roi et tous ses fils viennent chez ton serviteur.
Absalomu akamwendea mfalme na kusema, “Tazama sasa, mtumishi wako anao wakatao kondoo manyoya. Tafadhari, naomba mfalme na watumishi wake waende nami, mtumishi wako.”
25 Le roi répondit à Absalon: Non, mon fils, nous n'irons pas tous; nous ne voulons point t'être à charge. Absalon le pressa; mais il ne céda point, et il le bénit.
Mfalme akamjibu Absalomu, “hapana mwanangu, tusiende sisi yote kwani tutakuwa mzigo kwako.” Absalomu akamhakikishia mfalme, lakini yeye asikubali kwenda, ila alimbariki Absalomu.
26 Alois, Absalon lui dit: Si tu refuses, que du moins mon frère Amnon vienne avec nous. Le roi lui répondit: Pourquoi donc irait-il avec toi?
Kisha Absalomu akasema, “kama sivyo, basi tafadhari mwache ndugu yangu Amnoni aende nasi.” Mfalme akamuliza, “Kwa nini Amnoni aende nanyi?”
27 Absalon le pressa, et David laissa partir avec lui Amnon et tous ses fils. Absalon leur fit un festin comme un festin de roi.
Absalomu akamsihi Daudi, hivyo akamruhusu Amnoni na wana wengine wa mfalme kwenda naye.
28 Puis, il donna ses ordres à ses serviteurs, disant: Faites attention; quand le cœur d'Amnon se complaira dans le vin, je vous dirai: Frappez Amnon et le mettez à mort; n'ayez point de crainte; n'est-ce point moi qui vous le commande? Soyez hommes, agissez en fils de la force.
Absalomu akawaamuru watumishi wake kusema, “Sikilizeni kwa makini. Amnoni atakapokuwa amelewa mvinyo, na nitakapowambia, 'Mpigeni Amnoni,' msiogope mwueni. Je siyo mimi niliyewamru? Mwe jasiri na hodari.”
29 Les serviteurs d'Absalon exécutèrent contre Amnon ce que leur avait prescrit leur maître. Et tous les fils du roi se levèrent; chacun d'eux se mit en selle sur sa mule, et ils s'enfuirent.
Hivyo watumishi wa Absalome wakamtendea Amnoni kama walivyoamriwa. Kisha wana wote wa mfalme wakainuka na kila mmoja akapanda nyumbu wake akakimbia.
30 Pendant qu'ils étaient encore en route, on vint dire à David: Absalon a tué tous les fils du roi, et il n'en reste pas un seul.
Hata ikawa wakati wakiwa njiani habari zikafika kwa Daudi kusema, “Absalomu ameua wana wote wa mfalme na hakuna hata mmoja aliyesalia.”
31 A ces mots, le roi se leva; il déchira ses vêtements, et il se jeta à terre; et tous ses serviteurs qui l'entouraient déchirèrent leurs vêtements.
Kisha mfalme akainuka na kurarua mavazi yake na kujilaza juu ya sakafu; watumishi wake wote wakasimama karibu naye mavazi yao yameraruriwa.
32 Et Jonabab, fils de Samaa, frère de David, prit la parole, et il dit: Que le roi mon maître ne dise pas que tous ses serviteurs les fils du roi ont été mis à mort, car Amnon seul a péri; et c'était sur les lèvres d'Absalon depuis le jour où sa sœur Thamar a été humiliée.
Yehonadabu mwana wa Shama, nduguye Daudi, akajibu na kusema, “Bwana wangu asidhani kuwa vijana wote ambao ni wana wa mfalme wameuawa, kwa maana ni Amnoni pekee ndiye aliyeuawa. Absalomu alilipanga jambo hili tangu siku ile Amnoni alivyomwaribu Tamari, dada yake.
33 Maintenant donc, que le roi mon maître n'ait pas à cœur tout ce qu'on lui a rapporté, quand on a dit: Tous les fils du roi sont morts, car Amnon seul n'existe plus.
Kwa hiyo basi, bwana wangu mfalme asiiweke taarifa hii moyoni, kudhani kwamba wana wote wa mfalme wameuawa, kwani aliyeuawa ni Amnoni peke yake.”
34 Or, Absalon s'était enfui; cependant, le serviteur qui faisait sentinelle leva les yeux, et il vit une nombreuse troupe qui accourait et descendait de la montagne; il entra pour l'apprendre au roi, et il dit: J'ai vu des hommes sur le chemin d'Oronen; ils descendent la montagne.
Absalomu akakimbia. Mtumishi aliyekuwa akiangalia akainua macho yake na kuona watu wengi wakija njiani kando ya kilima upande wake wa magharibi.
35 Et Jonabab dit au roi: Tu vois, les fils du roi sont vivants; il est advenu ce qu'avait dit ton serviteur.
Kisha Yehonadabu akamwambia mfalme, “Tazama, wana wa mfalme wanakuja. kama mtumishi wako alivyosema.”
36 Comme il achevait de parler, les fils du roi entrèrent; ils élevèrent la voix et ils pleurèrent; le roi aussi et tous ses serviteurs se prirent à pleurer amèrement.
Ikawa mara alipomaliza kusema wana wa mfalme wakafika, wakainua sauti zao na kulia. Na mfalme pamoja na watumishi wake wote pia wakalia kwa uchungu.
37 Or, Absalon s'était enfui; il se réfugia chez Tholmi, fils d'Emiud, roi de Gedsur, en la terre de Chamaachad, et le roi David pleura tous les jours son fils.
Lakini Absalomu akakimbia na kwenda kwa Talmai mwana wa Amihudi, mfalme wa Geshuri. Mfalme akaomboleza kila siku kwa ajili ya mwanaye.
38 Absalon s'était donc enfui, et il s'était retiré à Gedsur, où il demeura trois ans.
Hivyo Absalomu akakimbia na kwenda Geshuri na akakaa huko kwa miaka mitatu.
39 Le roi David renonça à le faire poursuivre, parce qu'il était consolé de la mort d'Amnon.
Moyo wa mfalme Daudi ukatamani kwenda kumwona Absalomu, kwa maana alikuwa amefarijika kwa habari ya kifo cha Amnoni.