< 2 Rois 5 >

1 Et Naaman, général de l'armée syrienne, était un homme considérable aux yeux de son maître, et d'un aspect imposant; c'était par lui que le Seigneur avait sauvé la Syrie, et l'homme était très-puissant, mais il était lépreux.
Wakati huu, Naamani alikuwa jemadari wa jeshi la mfalme wa Aramu. Alikuwa mtu mkuu mbele ya bwana wake na aliyeheshimiwa sana, kwa sababu kupitia kwake, Bwana alikuwa amewapa Aramu ushindi. Alikuwa askari shujaa, lakini alikuwa na ukoma.
2 Or, des maraudeurs sortis de la Syrie avaient emmené captive, de la terre d'Israël, une petite fille qui servait la femme de Naaman,
Siku hizo vikosi kutoka Aramu vilikuwa vimekwenda na vikawa vimemteka msichana kutoka Israeli, naye akamtumikia mkewe Naamani.
3 Cette fille dit à sa maîtresse: Plût à Dieu que mon maître fût en présence du prophète de Dieu en Samarie; il le guérirait de sa lèpre.
Akamwambia bibi yake, “Kama bwana wangu angelimwona nabii aliyeko Samaria! Angemponya ukoma wake.”
4 Et la femme entra auprès de son seigneur, et elle lui dit: La jeune fille de la terre d'Israël a parlé de telle et telle manière.
Naamani akaenda kwa bwana wake na kumwambia alichosema yule msichana kutoka Israeli.
5 Et le roi de Syrie dit à Naaman: Vas-y, va, et j'enverrai une lettre au roi d'Israël. Naaman partit donc, et il prit avec lui dix talents d'argent, six mille sicles d'or, et dix robes diverses.
Mfalme wa Aramu akamjibu, “Hakika, nenda. Nitatuma barua kwa mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo Naamani akaondoka, akiwa amechukua talanta kumi za fedha, shekeli 6,000 za dhahabu, na mivao kumi ya mavazi.
6 Et il porta au roi d'Israël la lettre où il était écrit: Dès que tu auras reçu cette lettre, tu guériras de sa lèpre mon serviteur Naaman, que j'ai envoyé auprès de toi.
Barua aliyopelekea mfalme wa Israeli iliandikwa hivi: “Pamoja na barua hii ninamtuma mtumishi wangu, Naamani, kwako ili uweze kumponya ukoma wake.”
7 Quand le roi d'Israël eut lu la lettre, il déchira ses vêtements, et il s'écria: Suis-je un Dieu pour donner la mort et la vie? Pourquoi celui-ci envoie-t-il un homme auprès de moi, afin que je le guérisse de sa lèpre? Vous le voyez, il cherche un prétexte contre moi.
Mara mfalme wa Israeli alipomaliza kuisoma ile barua, akararua mavazi yake na kusema, “Je, mimi ni Mungu? Je, mimi naweza kuua na kufufua tena? Kwa nini huyu mtu anamtuma mtu ili mimi nipate kumponya ukoma wake? Tazama jinsi anavyotafuta kuanzisha ugomvi nami!”
8 Aussitôt qu'Elisée apprit que le roi d'Israël avait déchiré ses vêtements, il envoya près de lui, disant: Pourquoi as-tu déchiré tes vêtements? Que Naaman vienne me trouver, qu'il sache qu'en Israël il y a un prophète.
Elisha mtu wa Mungu aliposikia kwamba mfalme wa Israeli alikuwa amerarua mavazi yake, akamtumia ujumbe huu: “Kwa nini umerarua mavazi yako? Mwamuru mtu huyo aje kwangu, naye atajua ya kuwa yuko nabii katika Israeli.”
9 Et Naaman y alla avec ses chevaux et son char, et il se tint à la porte d'Elisée.
Kwa hiyo Naamani akaenda, akiwa na farasi zake na magari yake, na kusimama mlangoni mwa nyumba ya Elisha.
10 Et le prophète lui envoya un messager, qui lui dit: Pars et baigne-toi sept fois dans le Jourdain, ta chair te reviendra, et tu seras guéri.
Elisha akamtuma mjumbe kumwambia, “Nenda uoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itapona, nawe utatakasika.”
11 Mais, Naaman irrité s'en alla en disant: Je m'étais dit: Il va certainement venir me trouver; il se tiendra devant moi, il invoquera le nom du Seigneur son Dieu, il imposera les mains sur mes plaies, et il me guérira de la lèpre.
Lakini Naamani akaondoka akiwa amekasirika, akasema, “Hakika nilidhani kwamba angetoka nje, asimame na kuliitia jina la Bwana Mungu wake, na kuweka mkono wake juu ya mahali pagonjwa, aniponye ukoma wangu.
12 Les eaux de l'Abana et du Pharphar, fleuves de Damas, ne valent-elles pas mieux que toutes les eaux du Jourdain? Si je m'y baigne après mon retour, ne serai-je point plus tôt guéri? Et il s'éloigna, et il partit courroucé;
Je, Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora zaidi kuliko mito yoyote ya Israeli? Je, nisingeweza kuoga ndani ya hiyo mito na kutakasika?” Basi akageuka na kuondoka kwa hasira kuu.
13 Et ses serviteurs s'approchèrent de lui, disant: Si le prophète t'avait prescrit une grande chose, ne la ferais-tu point? A plus forte raison, puisqu'il t'a dit: Baigne-toi, et tu seras guéri.
Watumishi wa Naamani wakamwendea na kumwambia, “Baba yangu, kama huyo nabii angekuambia kufanya jambo lililo kubwa, je, usingelifanya? Je, si zaidi sana basi, anapokuambia, ‘Oga na utakasike!’”
14 Et Naaman, ayant mis pied à terre, se baigna sept fois dans le Jourdain selon la parole d'Elisée; et sa chair redevint comme la chair d'un petit enfant; il était guéri.
Hivyo akashuka na kujizamisha ndani ya Yordani mara saba, kama vile huyo mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia, nayo nyama ya mwili wake ikapona na kutakasika kama ya mwili wa mvulana mdogo.
15 Et il retourna en personne auprès d'Elisée avec toute sa troupe; arrivé vers le prophète, il se tint debout devant lui, et dit: Je reconnais qu'il n'y a point de Dieu sur la terre sinon en Israël; maintenant reçois la bénédiction de ton serviteur.
Kisha Naamani na wahudumu wake wote wakarudi kwa yule mtu wa Mungu. Akasimama mbele yake na kusema, “Sasa najua kwamba hakuna Mungu katika ulimwengu wote isipokuwa katika Israeli. Tafadhali sasa upokee zawadi kutoka kwa mtumishi wako.”
16 Elisée répondit: Vive le Seigneur, devant qui je me tiens! je n'accepterai rien. L'autre le pressa d'accepter, mais il ne le voulut pas.
Nabii akajibu, “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ninamtumikia, sitapokea kitu hata kimoja.” Ingawa Naamani alimsihi sana, yeye alikataa.
17 Et Naaman dit: Puisque tu refuses, que l'on donne du moins à ton serviteur assez de terre pour charger deux mulets; car ton serviteur ne fera plus d'holocaustes, et ne brûlera plus d'encens pour d'autres dieux; il ne sacrifiera qu'au Seigneur, à cause de cette affaire.
Naamani akasema, “Ikiwa hutapokea, tafadhali mtumishi wako na apewe udongo kiasi cha mzigo wa kuweza kubebwa na punda wawili, kwa sababu mtumishi wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa na dhabihu kwa mungu mwingine isipokuwa Bwana.
18 Et que le Seigneur pardonne à ton serviteur, si, lorsque mon maître entrera dans le temple de Remman, pour y adorer, appuyé sur mon bras, je me prosterne aussi dans le temple de Remman, pendant que mon maître y adorera; que le Seigneur pardonne alors à ton serviteur.
Lakini Bwana na amsamehe mtumishi wake kwa kitu hiki kimoja: Wakati bwana wangu atakapoingia kwenye hekalu la Rimoni ili kusujudu, naye akiwa anauegemea mkono wangu, nami nikasujudu huko pia, wakati nitakaposujudu ndani ya hekalu la Rimoni, Bwana na amsamehe mtumishi wako kwa ajili ya jambo hili.”
19 Le prophète dit à Naaman: Va-t'en en paix. Et il s'éloigna pour retourner en la terre de Debratha.
Elisha akamwambia, “Nenda kwa amani.” Baada ya Naamani kusafiri umbali fulani,
20 Mais Giézi, le serviteur d'Elisée, se dit: Voilà que mon maître s'est abstenu de rien accepter des choses qu'avait apportées ce Naaman le Syrien; vive le Seigneur! je courrai après lui, et j'en obtiendrai quoi que ce soit.
Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akajiambia mwenyewe, “Bwana wangu amemwachia kirahisi sana Naamani, huyu Mwaramu, kwa kutokupokea kutoka kwake vile alivyovileta. Hakika kama Bwana aishivyo, nitamkimbilia na kupata kitu kutoka kwake.”
21 Et Giézi courut après Naaman; le Syrien le vit courant après lui, et il retourna son char pour le rencontrer.
Hivyo Gehazi akaharakisha kumfuatilia Naamani. Naamani alipomwona akikimbia kumwelekea, akashuka chini kutoka kwenye gari lake na kwenda kumlaki. Akauliza, “Je, mambo yote ni sawa?”
22 Et Giézi dit: Tout va bien, mon maître m'envoie, disant: Voilà que deux jeunes gens fils de prophètes m'arrivent des montagnes d'Ephraïm, donne-leur un talent d'argent et deux robes.
Gehazi akajibu, “Mambo yote ni sawa. Bwana wangu amenituma nikuambie, ‘Vijana wawili kutoka kwa wana wa manabii wamenijia kutoka nchi ya vilima ya Efraimu. Tafadhali wape talanta ya fedha na mivao miwili ya mavazi.’”
23 Naaman répondit: Prends un double talent d'argent. Et il prit deux talents d'argent, en deux sacs, et deux robes, puis il les donna à porter à ses deux serviteurs qui partirent devant lui.
Naamani akasema, “Hakika, chukua talanta mbili za fedha.” Akamsihi Gehazi azipokee, kisha akafunga talanta mbili za fedha katika mifuko miwili pamoja na mivao miwili ya mavazi. Akawapa watumishi wake wawili mizigo hiyo, nao wakaibeba wakitangulia mbele ya Gehazi.
24 Il arriva à la brune, prit de leurs mains les présents, les déposa dans la maison, et congédia les deux hommes.
Gehazi alipofika kwenye kilima, akavichukua vile vitu kutoka kwa wale watumishi na kuvificha ndani ya nyumba. Akawaaga wale watu, nao wakaondoka.
25 Lui-même entra ensuite, et se tint auprès de son maître. Or, Elisée lui dit: Giézi, d'où viens-tu? Celui-ci répondit: Ton serviteur ne s'éloigne ni à droite, ni à gauche.
Kisha akaingia ndani na kusimama mbele ya Elisha bwana wake. Elisha akamuuliza, “Gehazi, ulikuwa wapi?” Gehazi akajibu, “Mtumishi wako hakwenda popote.”
26 Et le prophète reprit: Est-ce que mon cœur n'était pas avec toi quand l'homme a retourné son char pour aller à ta rencontre? Et maintenant, tu as pris de l'argent, tu as reçu des robes; tu veux acheter des oliviers, des vignes, des brebis, des bœufs, des serviteurs et des servantes.
Lakini Elisha akamwambia, “Je, roho yangu haikuwa pamoja nawe wakati yule mtu aliposhuka kutoka kwenye gari lake ili kukulaki? Je, huu ni wakati wa kupokea fedha au kupokea nguo, mashamba ya mizeituni, mashamba ya mizabibu, makundi ya kondoo na mbuzi, makundi ya ngʼombe, au watumishi wa kiume na wa kike?
27 Eh bien! la lèpre de Naaman s'attachera à toi et à ta race pour toujours. Et Giézi sortit de sa présence, couvert d'une lèpre blanche comme la neige.
Ukoma wa Naamani utakushika wewe na wazao wako milele.” Kisha Gehazi akaondoka mbele ya Elisha, mwenye ukoma, mweupe kama theluji.

< 2 Rois 5 >