< 2 Rois 23 >
1 Et ils rapportèrent au roi ces paroles; et il envoya des messagers, et il assembla autour de lui tous les anciens de Juda et de Jérusalem.
Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
2 Et le roi monta au temple du Seigneur avec tout Juda, tous les habitants de Jérusalem, les prêtres, les prophètes, tout le peuple, depuis le petit jusqu'au grand, et il lut à leurs oreilles toutes les paroles du livre de l'alliance trouvé dans le temple du Seigneur.
Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
3 Ensuite, le roi, debout sur le piédestal, renouvela l'alliance devant le Seigneur, afin de suivre le Seigneur, de garder ses commandements, ses témoignages et ses justices, de tout son cœur, dans la plénitude de son âme; et enfin, de faire revivre toutes les paroles de l'alliance écrite dans le livre; or, tout le peuple acquiesça à l'alliance.
Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
4 Et le roi prescrivit à Helcias le grand prêtre, aux prêtres du second rang et aux gardiens de la porte, d'enlever du temple du Seigneur tous les vases faits pour Baal, pour le bois sacré et pour l'armée du ciel; il les brûla hors de Jérusalem dans la vallée de Cédron, et il en fit porter les cendres à Béthel.
Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
5 Puis, il brûla vifs les prêtres idolâtres qu'avaient institués les rois de Juda et qui encensaient sur les hauts lieux, soit dans les villes de Juda, soit autour de Jérusalem, et aussi ceux qui encensaient Baal, le soleil, la lune, les douze signes et toute l'armée du ciel.
Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
6 Et il emporta l'idole des bois sacrés hors du temple, hors de Jérusalem dans le torrent de Cédron; il la réduisit en cendres qu'il dispersa sur la sépulture des fils du peuple.
Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
7 Il démolit la demeure des initiés qu'on avait construite dans le temple, et où les femmes tissaient des tentes pour le bois sacré.
Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
8 Il assembla ensuite tous les prêtres des villes de Juda; et il souilla les hauts lieux, où les prêtres avaient brûlé de l'encens, depuis Gebal jusqu'à Bersabée; puis, il abattit la maison des portes, à côté de la demeure de de Josué, prince de Jérusalem, à gauche, en sortant de la ville.
Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
9 Cependant, les prêtres des hauts lieux ne montèrent plus à l'autel du Seigneur à Jérusalem, à moins qu'ils n'eussent mangé des azymes au milieu de leurs frères.
Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
10 Josias souilla encore Tapheth dans le val des fils d'Ennom, où ils faisaient passer dans la flamme de Moloch, les uns leurs fils, les autres leurs filles.
Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
11 Il brûla les chevaux que les rois de Juda avaient consacrés au soleil, à l'entrée du temple, dans le trésor de Nathan, eunuque du roi, à Pharurim; il brûla en outre le char du soleil,
Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
12 Et les autels que les rois de Juda avaient élevés sur la terrasse au- dessus de la chambre d'Achaz, et ceux que Manassé avait construits dans les deux parvis du temple; il en fit jeter les cendres dans le torrent de Cédron.
Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
13 Le roi souilla aussi le temple que Salomon, roi d'Israël, avait érigé en face de Jérusalem, à droite du chemin de la montagne de Mosthath, en l'honneur d'Astarté, abomination des Sidoniens et de Chamos, abomination de Moab et de Moloch, abomination des Ammonites.
Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
14 Il mit en pièces leurs colonnes, détruisit leurs bois sacrés, et remplit d'ossements humains le lieu où on les adorait.
Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
15 Puis, il abattit l'autel qu'en Béthel, sur le haut lieu, Jéroboam, fils de Nabat, avait élevé et où il avait fait tomber tout le peuple dans le péché; il le démolit. Il en broya les pierres, il les réduisit en poudre, et il brûla le bois sacré.
Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
16 Et Josias, se détournant, vit les sépulcres de cette ville; aussitôt, il donna ses ordres: il en fit extraire les ossements, et il les brûla sur l'autel pour le souiller, selon la parole du Seigneur qu'avait dite l'homme de Dieu quand Jéroboam avait célébré la fête de l'autel; puis, se retournant encore, il leva les yeux et il vit la sépulture de cet homme de Dieu qui avait dit ces paroles.
Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
17 Et il dit: Quel est ce tombeau que j'aperçois? Et les hommes de la ville lui répondirent: Celui de l'homme de Dieu qui est venu de Juda, et qui a fait les imprécations contre l'autel de Béthel.
Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
18 Et le roi dit: Respectez-le; que nul n'enlève ses ossements. Et ses os furent sauvés avec ceux du prophète qui était venu de Samarie.
Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
19 Josias détruisit donc tous les temples des hauts lieux que les rois d'Israël avaient élevés dans les villes de Samarie, pour y irriter le Seigneur, et il y fit la même chose qu'à Béthel.
Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
20 Et il sacrifia sur leurs autels tous les prêtres des hauts lieux qui étaient là, il y brûla les os des hommes, et il retourna à Jérusalem.
Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
21 Et le roi donna ses ordres à tout le peuple, disant: Immolez la pâque au Seigneur notre Dieu, comme il est écrit au livre de cette alliance.
Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
22 Car, on n'avait point ainsi célébré cette fête depuis le temps des Juges qui jugeaient Israël; ni sous les rois d'Israël, ni sous les rois de Juda.
Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
23 Ce ne fut qu'en la dix-huitième année du règne de Josias, que l'on immola la pâque au Seigneur à Jérusalem
Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
24 En outre, Josias extermina les initiés et les devins; Il détruisit les idoles, les images et toutes les abominations qui existaient tant à Jérusalem qu'en Juda, afin de respecter les paroles de la Loi écrite dans le livre, que le prêtre Chelsias avait trouvé dans la maison du Seigneur.
Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
25 Il n'y avait point eu auparavant de roi qui, comme lui, se convertît à Dieu de tout son cœur, de toute son âme et de toutes ses forces, conformément à la loi de Moïse; et il n'y en eut point après lui.
Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
26 Mais le Seigneur ne détourna point la colère dont il était enflammé contre Juda, à cause des offenses qu'il avait reçues de Manassé.
Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
27 Et le Seigneur dit: J'expulserai aussi Juda de devant ma face comme j'ai expulsé Israël; je répudierai cette ville que j'avais choisie, cette Jérusalem, et le temple dont j'avais dit: C'est là que sera mon nom.
Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
28 Quant au reste de l'histoire de Josias, n'est-il pas écrit au livre des Faits et gestes des rois de Juda?
Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
29 Sous son règne, le Pharaon d'Égypte Néchao marcha sur le fleuve Euphrate contre le roi des Assyriens; Josias se porta à sa rencontre, et Néchao le tua à Mageddo, au premier choc.
Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
30 Les serviteurs placèrent son corps sur un char, et le ramenèrent de Mageddo à Jérusalem, et ils l'ensevelirent dans son sépulcre; alors, le peuple de la terre prit Joachaz, fils de Josias; il le sacra, et il le proclama roi la place de son père.
Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
31 Joachaz avait vingt-trois ans quand il monta sur le trône, et il régna trois mois à Jérusalem; le nom de sa mère était Amital, fille de Jérémie de Lebna.
Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
32 Et il fit le mal aux yeux du Seigneur, comme l'avaient fait ses pères.
Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
33 Et le Pharaon Néchao le transporta en Rablaam dans la terre d'Emath, pour qu'il ne régnât point à Jérusalem; puis, il imposa à la terre un tribut de cent talents d'argent et de cent talents d'or.
Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
34 A sa place, le Pharaon Néchao leur donna pour roi Eliacim, fils de Josias, et il changea son nom, et il l'appela Joacin. Et il emmena Joachaz en Égypte, où il mourut.
Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
35 Joacin donna au Pharaon de l'argent et de l'or, mais il taxa la terre pour payer le tribut au Pharaon; chacun donna de l'argent et de l'or selon sa taxe; tout le peuple donna donc le tribut au Pharaon.
Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
36 Joacin avait vingt-cinq ans lorsqu'il monta sur le trône, et il régna onze ans à Jérusalem; sa mère se nommait Jeldaph, fille de Phadaël, de Rhuma.
Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
37 Et il fit le mal aux yeux du Seigneur comme avaient fait tous ses aïeux.
Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.