< 2 Rois 2 >

1 Or, dans le temps que le Seigneur ravit Elie, comme au ciel au milieu d'un tourbillon, Elie et Elisée sortirent de Galgala.
Wakati Bwana alipokuwa karibu kumchukua Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya na Elisha walikuwa njiani wakitoka Gilgali.
2 Et Elie dit à Elisée: Reste ici, car Dieu veut que j'aille jusqu'à Béthel. Elisée répondit: Vive le Seigneur, et vive ton 'âme, je ne te quitterai pas. Ils entrèrent donc à Béthel.
Eliya akamwambia Elisha, “Kaa hapa. Bwana amenituma Betheli.” Lakini Elisha akasema, “Kwa hakika, kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Kwa hiyo wakaenda Betheli pamoja.
3 Et les fils des prophètes qui étaient à Béthel, s'approchèrent d'Elisée, et ils lui dirent: Ne sais-tu pas qu'aujourd'hui le Seigneur doit ravir ton maître au-dessus de ta tête? Il répondit Oui, je le sais, gardez le silence.
Wana wa manabii waliokuwako huko Betheli wakamjia Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Elisha akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
4 Elie dit ensuite à Elisée: Reste ici, car Dieu veut que j'aille jusqu'à Jéricho. Et il répondit: Vive le Seigneur, et vive ton âme! je ne te quitterai pas. Ils entrèrent donc à Jéricho.
Kisha Eliya akamwambia, “Baki hapa, Elisha. Bwana amenituma Yeriko.” Naye akajibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.
5 Et les fils des prophètes qui étaient à Jéricho s'approchèrent d'Elisée, et ils lui dirent Ne sais-tu pas qu'aujourd'hui le Seigneur doit ravir ton maître au-dessus de ta tête? Il répondit: Oui, je le sais, gardez le silence.
Wana wa manabii waliokuwako huko Yeriko wakamwendea Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
6 Elie lui dit ensuite: Reste ici, le Seigneur veut que j'aille jusqu'au Jourdain. Elisée répondit: Vive le Seigneur et vive ton âme! je ne te quitterai point. Ils marchèrent donc tous les deux.
Kisha Eliya akamwambia, “Kaa hapa. Bwana amenituma kwenda Yordani.” Naye akamjibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wote wawili wakaendelea pamoja.
7 Or, il y avait au loin, vis-à-vis d'eux, cinquante fils des prophètes, et ils s'arrêtèrent l'un et l'autre aux bords du fleuve.
Wana hamsini wa manabii wakaenda na kusimama kwa mbali, kuelekea mahali ambapo Eliya na Elisha walikuwa wamesimama kando ya Mto Yordani.
8 Et Elie prit sa peau de brebis, la fit tourner, et en frappa l'eau du fleuve: et l'eau se sépara à leur droite et à leur gauche; ils passèrent tous les deux, et ils s'en furent dans le désert.
Eliya akachukua vazi lake, akalisokota na kupiga nalo maji. Maji yakagawanyika upande wa kuume na upande wa kushoto, nao wawili wakavuka pakavu.
9 Pendant qu'ils traversaient le Jourdain, Elie dit à Elisée: Demande ce que je ferai pour toi avant d'être ravi loin de toi. Elisée répondit: Que j'aie part à ton double esprit.
Walipokwisha kuvuka, Eliya akamwambia Elisha, “Niambie, nikufanyie nini kabla sijaondolewa kutoka kwako?” Elisha akajibu, “Naomba nirithi sehemu maradufu ya roho yako.”
10 Elie reprit: Tu as demandé une chose difficile: si tu me vois quand je serai ravi d'auprès de toi, il en sera pour toi ainsi; sinon, cela ne sera pas.
Eliya akasema, “Umeomba jambo gumu. Lakini kama utaniona wakati ninapoondolewa kutoka kwako litakuwa lako. La sivyo, hautalipata.”
11 Ils parlaient ainsi en marchant, et voilà qu'un char de feu et des chevaux de feu les séparèrent l'un de l'autre; puis, Elie fut ravi dans un tourbillon comme au ciel.
Walipokuwa wakitembea pamoja na kuzungumza, ghafula gari la moto na farasi wa moto vilitokea na kuwatenganisha wao wawili, naye Eliya akapanda mbinguni katika upepo wa kisulisuli.
12 Et Elisée le vit, et il cria: Père, père, char et conducteur d'Israël. Bientôt il ne le vit plus; et il saisit ses vêtements, et il les déchira en deux lambeaux.
Elisha aliona hili, naye akapaza sauti, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya Israeli na wapanda farasi wake!” Naye Elisha hakumwona tena. Kisha akazishika nguo zake mwenyewe na kuzirarua.
13 Ensuite, Elisée ramassa la peau de brebis qui était tombée de dessus Elie, et s'en retourna. Il s'arrêta aux bords du Jourdain.
Akaliokota lile vazi lililoanguka kutoka kwa Eliya, kisha akarudi na kusimama ukingoni mwa Yordani.
14 Et il prit la peau de brebis qui était tombée de dessus Elie, en frappa l'eau du fleuve, et dit: Où est maintenant le Dieu d'Elfe? Et il frappa les eaux, qui s'ouvrirent à droite et à gauche, et Elisée passa.
Ndipo akalichukua lile vazi ambalo lilikuwa limeanguka kutoka kwa Eliya, naye akayapiga yale maji nalo. Akauliza, “Yuko wapi sasa Bwana, Mungu wa Eliya?” Elisha alipoyapiga maji, yakagawanyika kulia na kushoto, naye akavuka.
15 Les fils des prophètes qui étaient à Jéricho, sur la rive opposée, le virent alors arriver, et dirent: L'esprit d'Elie est resté sur Elisée. Et ils allèrent à sa rencontre, et se prosternèrent devant lui la face contre terre.
Wale wana wa manabii kutoka Yeriko waliokuwa wakitazama wakasema, “Roho wa Eliya inamkalia Elisha.” Nao wakaenda kumlaki na kusujudu hadi nchi mbele yake.
16 Puis, ils lui dirent: Il y a avec tes serviteurs cinquante hommes vaillants; qu'ils partent, qu'ils s'informent de ton maître; est-ce que l'Esprit du Seigneur l'a ravi, et l'a jeté dans le Jourdain ou sur l'une des montagnes, ou sur l'une des collines? Mais Elisée répondit: N'envoyez pas.
Wakasema, “Tazama, sisi watumishi wako tunao watu hamsini wenye uwezo. Waruhusu waende kumtafuta bwana wako. Labda Roho wa Bwana amemtwaa na kumweka katika mlima fulani au bonde fulani.” Elisha akajibu, “Hapana, msiwatume.”
17 Ils le pressèrent tant qu'il en eut honte, il dit enfin: Envoyez; en conséquence, ils firent partir cinquante hommes qui cherchèrent trois jours, et ne trouvèrent point Elie.
Lakini wakasisitiza, mpaka akaona aibu kuwakatalia. Hivyo akasema, “Watumeni.” Nao wakawatuma watu hamsini, wakamtafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata.
18 Ils revinrent auprès d'Elisée, car il s'était établi à Jéricho, et il leur dit: Ne vous avais-je point dit: Ne partez pas.
Walipomrudia Elisha, ambaye alikuwa akingojea huko Yeriko, akawaambia, “Je, sikuwaambia msiende?”
19 Or, les hommes de la ville dirent à Elisée: Voilà que la ville est bien située comme celles que regarde le Seigneur, mais les eaux y sont mauvaises et la terre est stérile.
Watu wa mji wakamwambia Elisha, “Tazama, bwana wetu, mahali mji huu ulipojengwa ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo, lakini maji yake ni mabaya, na nchi haizai.”
20 Et Elisée dit: Prenez-moi une cruche neuve et mettez-y du sel. Ils prirent donc une cruche, et la lui apportèrent.
Akasema, “Nileteeni bakuli mpya, mweke chumvi ndani yake.” Kwa hiyo wakamletea.
21 Ensuite, Elisée alla à la source, y versa le sel, et dit: Voici ce que dit le Seigneur: J'ai assaini ces eaux; il n'y aura plus ici ni mortalité ni stérilité.
Kisha akaenda kwenye chemchemi na kuitupa ile chumvi ndani yake, akisema, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nimeyaponya maji haya. Kamwe hayatasababisha mauti tena wala kutozaa.’”
22 Et les eaux sont restées saines jusqu'à nos jours, selon la parole qu'avait dite Elisée.
Nayo yale maji yakaponywa mpaka leo, sawasawa na neno la Elisha alilokuwa amesema.
23 De là, il monta à Béthel, et comme il marchait dans le chemin, de petits enfants sortirent de la ville, le raillèrent, et lui dirent: Monte, chauve, monte.
Kutoka huko Elisha akakwea kwenda Betheli. Ikawa alipokuwa akitembea barabarani, baadhi ya vijana wakatoka mjini na kumfanyia mzaha. Wakasema, “Paa, wewe mwenye upaa! Paa, wewe mwenye upaa!”
24 Il se retourna, les vit, et les maudit au nom du Seigneur; or, voilà que deux ours s'élancèrent de la forêt, et mirent en pièces quarante-deux de ces enfants.
Akageuka, akawatazama na kuwalaani kwa Jina la Bwana. Kisha dubu wawili wa kike wakatokea mwituni na kuwararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao.
25 De là, il alla au mont Carmel, puis il retourna à Samarie.
Naye akaondoka huko, akaenda Mlima Karmeli, na kutoka huko akarudi Samaria.

< 2 Rois 2 >