< 2 Rois 12 >

1 Joas monta sur le trône la septième année du règne de Jéhu; il régna quarante ans à Jérusalem; le nom de sa mère était Sabia de Bersabée.
Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
2 Et Joas fit ce qui était droit devant le Seigneur tant que le prêtre Joïada vécut pour l'éclairer.
Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
3 Seulement, aucun des autels des hauts lieux ne fut déplacé; le peuple y fit encore des sacrifices et y brûla de l'encens.
Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
4 Or, Joas dit aux prêtres: Que les prêtres prennent tout l'argent des choses saintes, entrant dans le temple du Seigneur, et provenant soit des évaluations, soit des dons que chacun fait au gré de son cœur.
Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
5 Que les prêtres le prennent, chacun selon son rang, et qu'ils l'emploient aux réparations du temple partout où ils en trouveront à faire.
Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
6 En la vingt-troisième année du règne de Joas, le temple n'était pas encore entièrement réparé.
Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
7 Alors, le roi Joas fit venir le prêtre Joïada et les autres prêtres, et il leur dit: Pourquoi le temple n'est-il pas réparé? Désormais, ne prenez plus d'argent selon votre rang; donnez-le pour réparer le temple.
Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
8 Et les prêtres consentirent à ne plus recevoir d'argent du peuple, pourvu qu'ils ne fussent plus chargés des réparations du temple.
Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
9 Et Joad le prêtre prit une cassette; il en troua le couvercle, et il le mit près de l'autel, en la demeure d'un homme appartenant au temple du Seigneur. Puis, les prêtres, gardiens de la porte, y versèrent tout l'argent trouvé dans la maison du Seigneur.
Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
10 Lorsqu'ils virent qu'il y avait beaucoup d'argent dans la cassette, le scribe du roi et le grand prêtre lièrent et comptèrent l'argent trouvé dans le temple du Seigneur.
Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
11 Puis, il remirent l'argent qu'on avait recueilli entre les mains de ceux qui exécutaient les travaux signalés par les surveillants du temple du Seigneur; ils en donnèrent aussi aux charpentiers et aux constructeurs employés au temple,
Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
12 Ainsi qu'aux maçons et aux tailleurs de pierre, afin qu'ils achetassent des bois et des pierres de taille pour consolider le temple, jusqu'à ce que l'on eût dépensé tout ce que l'on avait reçu, pour les réparations du temple.
waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
13 Mais on ne devait rien prendre de l'argent offert dans le temple du Seigneur, pour fabriquer les portes d'argent, les clous, les fioles, les trompettes, les vases d'or et les vases d'argent;
Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
14 Parce qu'on devait le donner à ceux qui faisaient les réparations; et ceux-ci l'employèrent à consolider le temple du Seigneur.
zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
15 Et l'on ne demanda pas de comptes aux hommes à qui l'argent fut donné, pour qu'ils le remissent aux ouvriers chargés des travaux, parce que les réparations furent exécutées de bonne foi.
Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
16 L'argent dû pour les péchés, l'argent dû pour les omissions, tout ce qu'on apporta dans le temple alla aux prêtres.
Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
17 En ce temps-là, Azaël, roi de Syrie, sortit pour combattre Geth, et il s'en empara; puis, il se retourna pour marcher sur Jérusalem.
Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
18 Mais Joas, roi de Juda, prit toutes les offrandes consacrées par Josaphat, par Joram et par Ochozias, ses pères, rois de Juda; il prit ses propres offrandes et tout l'or qui se trouva, soit dans le temple du Seigneur, soit dans le palais du roi; puis, il envoya tout à Azaël, roi de Syrie; et celui-ci s'éloigna de Jérusalem.
Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
19 Quant au reste de l'histoire de Joas, n'est-il pas écrit au livre des Faits et gestes des rois de Juda?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 Et ses serviteurs se révoltèrent; ils tramèrent un complot, et ils frappèrent Joas en la maison de Mello qui est à Sella.
Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
21 Jézirchar, fils de Jémuath, et Jézébuth, fils de Somer, ses serviteurs, le frappèrent, et il mourut; on l'ensevelit auprès de ses pères en la ville de David; et son fils Amasias régna à sa place.
Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Rois 12 >