< 2 Chroniques 30 >

1 Et Ézéchias envoya en tout Israël et en Juda, et il écrivit des lettres à Ephraïm et à Manassé, pour qu'ils vinssent au temple du Seigneur à Jérusalem, faire la Pâque du Seigneur Dieu d'Israël.
Hezekia akatuma ujumbe kuwaita Israeli wote na Yuda, pia akaandika barua kwa Efraimu na Manase, kuwakaribisha ili waje hekaluni mwa Bwana huko Yerusalemu kuadhimisha Pasaka kwa Bwana, Mungu wa Israeli.
2 Et le roi, et les princes et toute l'Église de Jérusalem, résolurent de faire la Pâque le second mois.
Mfalme na maafisa wake pamoja na kusanyiko lote katika Yerusalemu waliamua kuadhimisha Pasaka katika mwezi wa pili.
3 Car ils ne la pouvaient faire en ce moment, parce qu'il n'y avait point assez de prêtres consacrés, et que tout le peuple n'était point réuni à Jérusalem.
Kwa sababu makuhani hawakuwa wamejitakasa idadi ya kutosha na watu wakawa hawajakusanyika huko Yerusalemu, hawakuwa wameweza kuadhimisha Pasaka kwa wakati wake wa kawaida.
4 Et cette décision fut agréable au roi et à toute l'Église.
Mpango huu ukaonekana wafaa kwa mfalme na kusanyiko lote.
5 Ils ordonnèrent aussi que l'on proclamât en tout Israël, depuis Bersabée jusqu'à Dan, que l'on eût à venir pour faire la Pâque du Seigneur Dieu à Jérusalem; car la multitude ne l'avait jamais faite comme le prescrit l'Écriture.
Wakaamua kupeleka tangazo Israeli kote, kuanzia Beer-Sheba hadi Dani, wakiwaita watu waje Yerusalemu kuadhimisha Pasaka ya Bwana, Mungu wa Israeli. Ilikuwa haijaadhimishwa na idadi kubwa ya watu kama hiyo kufuatana na yale yaliyokuwa yameandikwa.
6 Les courriers, avec les lettres du roi et des princes, parcoururent tout Juda et tout Israël, selon l'ordre d'Ézéchias, et ils dirent: Fils d'Israël, revenez au Seigneur Dieu d'Abraham, d'Isaac et d'Israël; ramenez ceux de vous qui survivent et qui ont échappé aux mains du roi d'Assyrie.
Kwa amri ya mfalme, matarishi wakapita katika Israeli na Yuda kote wakiwa na barua kutoka kwa mfalme na kutoka kwa maafisa wake zikisema: “Watu wa Israeli, mrudieni Bwana, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Israeli, ili naye awarudie ninyi mliosalia, mlionusurika kutoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru.
7 Ne soyez pas comme vos pères et vos frères; ils se sont séparés du Seigneur Dieu de leurs pères, et le Seigneur les a livrés à la dévastation, comme vous avez vu.
Msiwe kama baba zenu na ndugu zenu, ambao hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Mungu wa baba zao, hivyo akawafanya kitu cha kushangaza kama mnavyoona.
8 Maintenant donc, n'endurcissez point vos cœurs comme vos pères; glorifiez le Seigneur votre Dieu, entrez dans le lieu saint qu'il a consacré pour toujours; servez le Seigneur votre Dieu, et il détournera de vous sa terrible colère.
Msiwe na shingo ngumu, kama baba zenu walivyokuwa, bali nyenyekeeni kwa Bwana. Njooni mahali patakatifu, alipopatakasa milele. Mtumikieni Bwana Mungu wenu, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nanyi.
9 Car, lorsque vous serez revenus au Seigneur, vos frères et vos enfants trouveront miséricorde chez ceux qui les ont emmenés captifs, et Dieu vous les ramènera en cette terre; car le Seigneur notre Dieu est miséricordieux et compatissant, et il ne détournera point de vous sa face, si nous retournons à lui.
Kama mkimrudia Bwana ndipo wale ndugu zenu waliotekwa pamoja na watoto wenu watakapoonewa huruma na wale waliowateka na kuwaachia warudi katika nchi hii, kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni mwenye neema na huruma, hatageuzia uso wake mbali nanyi kama ninyi mkimrudia yeye.”
10 Et les courriers passèrent de ville en ville, dans les montagnes d'Ephraïm et de Manassé, jusqu'à Zabulon, et ils furent un sujet de risée et de raillerie.
Matarishi wakaenda mji hadi mji katika Efraimu na Manase, wakafika mpaka Zabuloni, lakini watu wakawadharau na kuwadhihaki.
11 Toutefois, des hommes d'Aser, de Manassé et de Zabulon, rentrèrent en eux-mêmes, et vinrent à Jérusalem en Juda.
Lakini, baadhi ya watu wa Asheri, Manase na Zabuloni, wakajinyenyekeza wakaja Yerusalemu.
12 Car la main du Seigneur excita leur cœur à partir et à suivre les ordres du roi et des princes, selon la parole du Seigneur.
Pia katika Yuda mkono wa Mungu ulikuwa juu ya watu kuwapa umoja katika kutenda yale ambayo mfalme na maafisa wake waliwaamuru, kulingana na neno la Bwana.
13 Une grande multitude se réunit donc à Jérusalem pour faire la fête des azymes le second mois; l'Église fut très-nombreuse.
Basi umati mkubwa wa watu ukakusanyika huko Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu katika mwezi wa pili.
14 Et ils se levèrent, et ils abattirent dans Jérusalem tous les autels où l'on brûlait de l'encens pour les faux dieux; ils les enlevèrent et les jetèrent dans le torrent de Cédron.
Wakajitia kazini kuyaondoa yale madhabahu yaliyokuwa huko Yerusalemu, wakayaondoa pia yale madhabahu ya kufukizia uvumba kwa miungu na kuyatupa Bonde la Kidroni.
15 Et ils immolèrent la pâque le quatorzième jour de la seconde lune, et les prêtres et les lévites, s'étant repentis et purifiés, offrirent des holocaustes dans le temple du Seigneur.
Kisha wakamchinja mwana-kondoo wa Pasaka katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Makuhani na Walawi waliona aibu, wakajitakasa na kuleta sadaka za kuteketezwa katika Hekalu la Bwana.
16 Et chacun se tint à son rang, selon leur ordonnance et selon les commandements de Moïse, homme de Dieu; les prêtres reçurent le sang des mains des lévites.
Kisha wakachukua nafasi zao za kawaida kama ilivyoelezwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu. Makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa na Walawi.
17 Car la plus grande partie de l'Église ne s'était point encore sanctifiée, et les lévites étaient prêts à immoler la pâque pour tous ceux qui n'avaient pu se sanctifier au Seigneur.
Kwa kuwa wengi waliokuwa katika lile kusanyiko walikuwa hawajajitakasa, iliwapasa Walawi wachinje wana-kondoo wengine wa Pasaka kwa ajili ya wale watu ambao hawakuwa safi, kwa kufuata taratibu za ibada ili kuwatakasa kwa Bwana.
18 Parmi le peuple d'Ephraïm, de Manassé, d'Issachar, de Zabulon, le plus grand nombre ne s'était pas purifié; mais ils mangèrent la pâque contrairement à l'Écriture; à cause de cela, Ezéchias fit pour eux cette prière, disant: Que le Seigneur, dans sa bonté, soit propice
Ingawa watu wengi miongoni mwa wale waliotoka Efraimu, Manase, Isakari na Zabuloni walikuwa hawajajitakasa, hata hivyo walikula Pasaka kinyume na ilivyoandikwa. Lakini Hezekia akawaombea, akisema, “Bwana, ambaye ni mwema na amsamehe kila mmoja
19 A tous les cœurs qui cherchent avec droiture le Seigneur Dieu de leurs pères, quoiqu'ils n'aient point la pureté que veulent les choses saintes.
ambaye anauelekeza moyo wake kumtafuta Mungu, Bwana, Mungu wa baba zake, hata kama yeye si safi kulingana na sheria za mahali patakatifu.”
20 Et le Seigneur exauça Ezéchias, et il guérit tout le peuple.
Naye Bwana akamsikia Hezekia akawaponya watu.
21 Et les fils d'Israël, qui se trouvaient à Jérusalem, firent la fête des Azymes sept jours, en grande allégresse, célébrant chaque jour le Seigneur; et les prêtres et les lévites accompagnaient leurs chants avec les instruments consacrés.
Waisraeli waliokuwa Yerusalemu wakaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa muda wa siku saba, nao Walawi na makuhani walikuwa wakiimba kila siku, wakiwa na ala za uimbaji za kumsifu Bwana.
22 Et Ezéchias parla au cœur des lévites et de tous ceux qui comprenaient le mieux le Seigneur, et ils firent la fête des Azymes sept jours, sacrifiant l'hostie pacifique, et rendant gloire au Seigneur Dieu de leurs pères.
Hezekia akazungumza akiwatia moyo Walawi wote, ambao walionyesha ustadi katika kumtumikia Bwana. Hivyo watu wakala chakula cha sikukuu kwa siku saba, wakitoa sadaka za amani na kumshukuru Bwana, Mungu wa baba zao.
23 Et l'Église résolut de fêter une seconde fois sept jours, et ils les fêtèrent avec joie.
Kisha kusanyiko lote likakubali kuendelea na sikukuu kwa siku saba zaidi, kwa hiyo kwa siku saba nyingine wakaendelea kuiadhimisha kwa furaha.
24 Car Ezéchias offrit à Juda et à l'Église mille bœufs et sept mille brebis, et les princes amenèrent, pour le peuple, mille bœufs et dix mille brebis, et il y eut une multitude de prêtres qui furent sanctifiés.
Hezekia, mfalme wa Yuda akatoa mafahali 1,000, kondoo na mbuzi 7,000 kwa ajili ya kusanyiko, nao maafisa wakatoa mafahali 1,000 pamoja na kondoo na mbuzi 10,000. Idadi kubwa ya makuhani wakajiweka wakfu.
25 Et toute l'Église était pénétrée de joie: prêtres, lévites, Église de Juda, peuple réuni à Jérusalem, prosélytes venus de la terre d'Israël, étrangers habitant Juda.
Kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi na lile kusanyiko lote lililotoka Israeli, pamoja na wale wageni waliotoka Israeli na wale walioishi katika Yuda wakafurahi.
26 Et l'allégresse fut grande en Jérusalem; on n'y avait point vu pareille fête depuis les jours de Salomon et de David.
Kulikuwa na furaha kubwa katika Yerusalemu, kwa sababu tangu siku za Mfalme Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli halijakuwepo jambo kama hili katika Yerusalemu.
27 Et les prêtres et les lévites se levèrent, et ils bénirent le peuple, et leur voix fut entendue, et leur prière monta jusqu'aux saintes demeures de Dieu dans le ciel.
Ndipo makuhani na Walawi wakasimama wakawabariki watu, naye Mungu akawasikia, kwa sababu maombi yao yalifika mbinguni, makao yake matakatifu.

< 2 Chroniques 30 >