< 2 Chroniques 28 >
1 Achaz avait vingt-cinq ans lorsqu'il monta sur le trône, et il régna seize ans à Jérusalem; et il ne fit point ce qui est droit devant le Seigneur, comme David, son aïeul.
Ahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, na akatawala miaka kumi na sita katika Yerusalemu. Hakufanya yaliyoadili katika macho ya Yahwe, kama Daudi babu yake alivyokuwa amefanya.
2 Mais il marcha dans les voies des rois d'Israël, car il fit des sculptures,
Badala yake, alitembea katika njia za wafalme wa Israeli; pia alitengeneza sanamu za kusubu kwa ajila ya Mabaali.
3 Et il sacrifia à leurs idoles dans le val de Benennom, et il fit passer ses enfants à travers la flamme; selon les abominations des peuples que le Seigneur avait exterminés devant les fils d'Israël.
Zaidi ya hayo, akafukiza uvumba katika bonde la Beni Hinomu na akawaweka watoto wake ndani ya moto, kwa mjibu wa desturi za uzinzi za watu ambao Yahwe aliwafukuza nje ya nchi zao mbele za watu wa Israeli.
4 Et il brûla de l'encens sur les hauts lieux, et sur les terrasses des maisons, et sous les arbres touffus.
Akatoa sadaka na kufukiza uvumba katika sehemu za juu na juu ya vilima na chini ya kila mti wenye majani mabichi.
5 Alors le Seigneur Dieu le livra au roi de Syrie; il le frappa par ses mains, en permettant aux Syriens d'emmener à Damas une multitude de captifs; il le livra aussi au roi d'Israël, et de ses propres mains, il le frappa d'une grande plaie.
Kwa hiyo Yahwe Mungu wa Ahazi, akamweka katika mikono ya mfalme wa Shamu. Waaramu wakamshinda na kuchukua kutoka kwake kundi kubwa la mateka, wakawapeleka Damesiki. Ahazi pia aliwekwa katika mikono ya mfalme wa Israeli ambaye alimshinda kwa mauji makuu.
6 Phacée, fils de Romélie, roi d'Israël, tua, en un seul jour, cent vingt mille hommes de Juda, forts et vaillants, parce qu'ils avaient abandonné le Seigneur Dieu de leurs pères.
Kwa maana Peka mwana wa Remalia, aliwaua katika Yuda wanajeshi 120, 00 kwa siku moja, wote walikuwa wanaume hodari, kwa maana walikuwa wamemsahau Yahwe, Mungu wa babu zao.
7 Et Zéchri, homme vaillant d'Ephraïm, tua Maasias, fils du roi; Esrican, son grand maître du palais, et Elcana, son lieutenant.
Zikri, mtu mwenye nguvu kutoka Efraimu, akawaua Maaseya mwana wa mfalme, Azrikamu, mwangalizi mkuu wa ikulu, na Elkana, ambaye alikuwa karibu na mfalme.
8 Et les fils d'Israël firent parmi leurs frères trois cent mille captifs: femmes, fils et filles; et ils leur enlevèrent un immense butin, et emportèrent les dépouilles à Samarie.
Jeshsi la Israeli likachukua mateka kutoka kwa ndugu zao 200, 000 wake, wana, na mabinti. Pia wakachukua nyara nyingi, ambazo walipeleka Samaria.
9 Or, il y avait là un prophète du Seigneur nommé Obed, qui sortit à la rencontre de l'armée pendant qu'elle revenait à Samarie, et il leur dit: Voilà que la colère du Seigneur Dieu de vos pères est sur Juda; il vous les a livrés, et vous les avez massacrés avec fureur, et le bruit en est monté jusqu'au ciel.
Lakini nabii wa Yahwe alikuwapo huko, jina lake aliitwa Odedi. Alikwenda nje kukutana na jeshi likiingia Samaria. Akawaambia, “Kwa sababu Yahwe, Mungu wa babu zenu, alikuwa na hasiri na Yuda, akawatia katika mikono yenu. Lakini mmewaua katika hasira inayofika juu mbinguni.
10 Et maintenant vous pensez garder comme esclaves les fils de Juda et de Jérusalem; mais ne suis-je point parmi vous pour prendre à témoin le Seigneur votre Dieu?
Sasa ninyi badala ya kuwahifadhi wanaume na wanawake wa Yuda na Yerusalemu kama watumwa wenu. Lakini je hamko na hatia ya dhambi zenu zidi ya Yahwe Mungu wenu?
11 Écoutez-moi donc, et délivrez les captifs que vous avez enlevés chez vos frères; car la colère du Dieu terrible est sur vous.
Sasa basi, nisikilizeni: warudisheni wafubgwa, ambao mmewachukua wa ndugu zenu, kwa maana ghadhabu ya Yahwe iko juu yenu.”
12 Et les chefs des fils d'Ephraïm: Udie, fils de Jean; Barachias, fils de Mosolmoth; Ezéchias, fils de Sellem; et Amasias, fils d'Eldaï, s'élevèrent pareillement contre ceux qui revenaient du combat.
Kisha baadhi ya viongozi wa watu wa Efraimu—Azaria mwana wa Yohanani, Berekia mwana wa Meshiremothi, na Yehizikia mwana wa Shalumu, na Amasa mwana wa Hadlai, wakasimama kinyume na wale waliorudi kutoka vitani.
13 Et ils leur dirent: Vous n'introduirez point ici, chez nous, ces captifs; car, lorsque vous péchez contre le Seigneur, votre péché retombe sur nous; et vous entendez ajouter à vos péchés et à vos délits par ignorance, quand déjà vos fautes sont nombreuses, et quand une terrible colère du Seigneur est sur Israël?
Wakasema kwao, “Lazimaa msiwaleta wafungwa hapa, kwa kuwa mlikusudia jambo ambalo litaleta juu yetu dhambi dhidi ya Yahwe, kuongeza dhambi juu yetu na makosa yetu, kwa maana makosa yetu ni makuu, na kuna hasira kali dhidi ya Israeli.”
14 Et les guerriers mirent en liberté les captifs, et ils leur rendirent les dépouilles, devant les chefs de toute l'Église.
Hivyo watu wenye silaha wakawaacha wafungwa na mateka mbele ya viongozi wa Israeli na kusanyiko lote
15 Et les hommes qui viennent d'être nominativement désignés, se levèrent, prirent soin des captifs, les vêtirent d'objets compris dans les dépouilles, les habillèrent, les chaussèrent, leur donnèrent des vivres pour manger, de l'huile pour se parfumer, firent monter les infirmes sur des ânes, les menèrent avec leurs frères jusqu'à Jéricho, ville des palmiers, et retournèrent à Samarie.
Watu ambao walipangwa kwa majina wakanyanyuka na kuwachukua wafungwa, na kuwavika wote waliokuwa uchi miongoni mwa mateka. Wakawavika na kuwapa viatu. Wakawapa chakula wale na kunywa. Wakawahudumia majeraha yao na kuwaweka waliodhaifu juu ya punda. Wakawarudisha kwenye familia zao katika Yeriko, (Ulioitwa mji wa mitende). Kisha wakarudi Samaria.
16 En ce temps-là, le roi Achaz envoya chez le roi assyrien demander son secours,
Wakati huo Mfalme Ahazi akatuma wajumbe kwa wafalme wa Ashuru kuwaomba wamsaidie.
17 Et voici pourquoi: les Sidoniens faisaient des irruptions; ils frappaient Juda, et lui enlevaient des captifs.
Kwa maana Waedomu walikuwa wamekuja tena na kuvamia Yuda, wakachukua wafungwa.
18 Les Philistins aussi avaient pris les armes contre les villes de la plaine, au midi de Juda, et s'étaient emparés de Bethsamys, de Galero, de Socho et de ses bourgs, de Thamna et de ses bourgs, de Gamzo et de ses bourgs, et ils s'y étaient établis.
Wafilisti pia wakavamia miji ya nchi ya chini na ya Negebu ya Yuda. Waliichukua Beth-shemeshi, Ayaloni, Giderothi, SoKo pamoja na vijiji vyake, Timna pamoja na vijiji vyake. Wakaenda kuishi katika sehemu hizo.
19 Car le Seigneur avait humilié Juda, à cause du roi Achaz qui s'était détourné du Seigneur.
Kwa kuwa Yahwe aliishusha chini Yuda kwa sababu ya Ahazi, mfalme wa Israeli; kwa maana alikuwa ametenda maovu katika Yuda na alikuwa ametenda dhambi nzito sana dhidi ya Yahwe.
20 Alors, Thelgath-Phalnasar, roi des Assyriens, intervint, mais contre lui, et il l'opprima.
Tiglath-pileseri, mfalme wa Ashuru, akaja kwake na akampa tabu badala ya kumpa nguvu.
21 Et Achaz prit les richesses du temple du Seigneur, celles du palais du roi, celles des demeures des princes, et il les donna au roi assyrien; or, celui-ci n'était pas venu pour le secourir,
Kwa kuwa Ahazi aliteka nyara nyumba ya Yahwe na nyumba ya mfalme na viongozi, kwa ajili ya kuvitoa vitu vya thamani kwa mfalme wa Ashuru. Lakini kufanya hivyo hakukumfaidisha yeye.
22 Mais pour l'écraser; cependant, le roi Achaz continua de se détourner du Seigneur, et il dit:
Mfalme Ahazi huyu huyu akatenda dhambi hata zaidi dhidi ya Yahwe katika muda wa mateso yake.
23 Je chercherai les dieux de Damas qui me frappent. Puis, il ajouta: Ce sont les dieux du roi de Syrie qui lui donnent de la force; je leur sacrifierai donc, et ils me protégeront. Et ils furent une cause de chute pour lui et pour Israël.
Kwa maana aliwatolea dhabihu mingu wa Dameski, miungu ambao walimshinda. Akasema, “Kwa sababu miungu wa mfalme wa Aramu waliwasaidia, nitawatolea sadaka ili wanisaidie.” Lakini walikuwa watesi wake na Israeli yote.
24 Achaz retira donc les vases du temple du Seigneur, il les brisa, ferma les portes du temple, et se fit des autels dans tous les carrefours de Jérusalem.
Ahazi akazikusanya pamoja samani za nyumba ya Mungu na kuzikata vipande vipande. Akaifunga milango ya nyumba ya Yahwe na kuzitengeneza madhabahu kwa ajili yake mwenyewe katika kila kona ya Yerusalemu.
25 Et il établit des hauts lieux dans toutes les villes de Juda pour que l'on y encensât des dieux étrangers; et les fils de Juda excitèrent le courroux du Seigneur Dieu de leurs pères.
Katika kila mji wa Yuda akafanya sehemu za juu kwa ajili ya kutolea sadaka za kuteketezwa kwa miungu wengine. Akamfanya Yahwe, Mungu wa babu zake, akasirike.
26 Le reste de ses faits et gestes, les premiers et les derniers, sont écrits au livre des Rois de Juda et d'Israël.
Sasa matendo yake yaliyobaki, na njia zake zote, mwanzo na mwisho, ona, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
27 Et Achaz s'endormit avec ses pères, et il fut enseveli en la ville de David; mais on ne le transporta pas dans le sépulcre des rois d'Israël, et son fils Ezéchias régna à sa place.
Ahazi akalala pamoja na babu zake, na wakamzika katika mji, katika Yerusalemu, lakini hawakumleta kwenye makaburi ya wafalme wa Israeli. Hezekia, mwanaye, akawa mfamle katika nafasi yake.