< 2 Chroniques 20 >

1 Après cela, les fils de Moab, les fils d'Ammon, et, avec eux, des Minéens, se mirent en campagne pour attaquer Josaphat.
Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati.
2 Et des gens vinrent et ils l'apprirent au roi, disant: Une grande multitude est venue contre toi des bords de la mer, du côté de la Syrie, et la voici en Asasan-Thamar (la même qu'Engaddi).
Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako kutoka Edomu tokea ngʼambo ile nyingine ya Bahari. Tayari liko Hasason-Tamari” (yaani En-Gedi).
3 Et Josaphat eut crainte, et il s'appliqua à chercher le Seigneur, et il proclama un jeûne dans tout Juda.
Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafuta Bwana, na akatangaza kwa Yuda wote kufunga.
4 Et Juda se rassembla pour chercher le Seigneur; et, de toutes les villes de Juda, on vint pour chercher le Seigneur.
Watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kutafuta msaada kutoka kwa Bwana. Wakaja kutoka kila mji wa Yuda ili kumtafuta.
5 Et Josaphat, avec toute l'Église de Juda en Jérusalem, se tint debout dans le temple du Seigneur devant le parvis neuf.
Kisha Yehoshafati akasimama katika kusanyiko la Yuda na Yerusalemu katika Hekalu la Bwana, mbele ya ua mpya,
6 Et il dit: Seigneur Dieu de mes pères, n'êtes-vous point Dieu dans le ciel au-dessus de nous? N'êtes-vous pas le Seigneur de tous les royaumes des nations? N'est-ce pas en vos mains que réside la force du pouvoir? Est-il quelqu'un qui puisse vous résister?
akasema: “Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe ndiwe uliye Mungu mbinguni? Si wewe ndiwe utawalaye juu ya falme zote za mataifa? Uweza na nguvu viko mkononi mwako, wala hakuna yeyote awezaye kushindana nawe.
7 N'êtes-vous pas le Seigneur dont le bras a exterminé les habitants de cette terre, devant les fils d'Israël, votre peuple? Ne l'avez-vous point donnée pour toujours à la race d'Abraham, votre bien-aimé?
Je, si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu, rafiki yako, hata milele?
8 Elle y demeure; elle y a bâti un lieu saint à votre nom, disant
Wameishi ndani yake na humo wamekujengea mahali patakatifu kwa ajili ya Jina lako, wakisema:
9 Si le mal, le glaive, la vengeance, la mort, la famine, viennent sur nous, nous nous tiendrons devant le temple et devant vous, ô Seigneur, parce que votre nom est sur le temple, et, dans notre affliction, nous crierons à vous, et vous nous entendrez, et vous nous sauverez.
‘Kama maafa yakitujia, ikiwa ni upanga, hukumu, tauni, au njaa, tutasimama mbele zako, mbele ya Hekalu hili ambalo limeitwa kwa Jina lako na kukulilia katika shida yetu, nawe utatusikia na kutuokoa.’
10 Et maintenant, voilà que les fils d'Ammon, et Moab et ceux de la montagne de Seïr, chez qui vous n'avez point permis à Israël de passer, à sa sortie d'Égypte (car il s'est détourné de leurs territoires, et ne les a point exterminés),
“Lakini sasa hawa watu wa kutoka Amoni, Moabu na Mlima Seiri, ambao hukuwaruhusu Israeli wazivamie nchi zao wakati walitoka Misri, hivyo wakageukia mbali nao na hawakuwaangamiza,
11 Voilà qu'ils nous attaquent pour entrer dans l'héritage que vous nous avez donné, et pour nous en bannir.
tazama jinsi wanavyotulipa kwa kuja kututupa nje ya milki uliyotupa sisi kuwa urithi.
12 Seigneur notre Dieu, ne les jugerez-vous pas? Car nous n'avons pas la force de résister à l'immense multitude qui marche contre nous, et nous ne savons que leur faire, sinon de tourner nos yeux vers vous.
Ee Mungu wetu, je, wewe hutawahukumu? Kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kukabiliana na jeshi hili kubwa linalokuja kutushambulia. Sisi hatujui la kufanya, bali macho yetu yanakutazama wewe.”
13 Or, tout Juda était là devant le Seigneur, avec leurs enfants et leurs femmes.
Watu wote wa Yuda pamoja na wake zao, watoto wao na wadogo wao wakasimama pale mbele za Bwana.
14 Et, dans l'Église, l'Esprit du Seigneur descendit sur Oziel, fils de Zacharie, des fils de Bandias, des fils d'Elihel, fils du lévite Matthanias, des fils d'Asaph.
Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya mtu mmoja jina lake Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, Mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi mzao wa Asafu alipokuwa amesimama katika kusanyiko.
15 Et il dit: Écoutez, ô Juda, et vous habitants de Jérusalem, et toi, roi Josaphat: voici ce que vous dit le Seigneur: N'ayez point de crainte, ne tremblez pas devant cette multitude immense; car ce combat n'est point de vous, mais de Dieu.
Akasema: “Sikilizeni, enyi Yuda wote nanyi nyote mkaao Yerusalemu, nawe Mfalme Yehoshafati! Hili ndilo Bwana asemalo kwenu, ‘Msiogope wala msifadhaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Kwa maana vita hivi si vyenu, bali ni vya Mungu.
16 Marchez demain contre elle; ils monteront le coteau d'Assis, et vous les trouverez à l'extrémité du torrent qui traverse le désert de Jerihel.
Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakwea kwa kupandia Genge la Sisi, nanyi mtawakuta mwisho wa bonde, kabla ya Jangwa la Yerueli.
17 Ce n'est point à vous de les combattre; comprenez cela, et voyez comme le Seigneur, ô Juda et Jérusalem, opèrera votre salut. N'ayez point de crainte, n'hésitez pas à marcher demain à leur rencontre: le Seigneur est avec vous.
Hamtahitaji kupigana vita hivi. Kaeni kwenye nafasi zenu, simameni imara na mkaone wokovu Bwana atakaowapatia, enyi Yuda na Yerusalemu. Msiogope, wala msifadhaike. Kesho tokeni mwende mkawakabili, naye Bwana atakuwa pamoja nanyi.’”
18 Et Josaphat, et tout Juda et les habitants de Jérusalem s'étant prosternés la face contre terre tombèrent devant le Seigneur pour l'adorer.
Yehoshafati akainamisha uso wake chini, nao watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakaanguka chini ili kuabudu mbele za Bwana.
19 Puis, les lévites des fils de Caath et des fils de Coré se levèrent pour chanter à haute voix les louanges du Seigneur Dieu d'Israël.
Ndipo baadhi ya Walawi kutoka kwa Wakohathi na kwa wana wa Kora wakasimama na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.
20 Et le peuple se leva dès l'aurore, et ils sortirent dans le désert de Thécoé; et, pendant qu'ils sortaient, Josaphat, se tenant immobile, cria, et dit: Écoutez-moi, Juda, et vous, habitants de Jérusalem, mettez votre confiance dans le Seigneur notre Dieu, et il se confiera en vous; mettez votre confiance dans son prophète, et vous prospérerez.
Asubuhi na mapema wakaondoka kuelekea Jangwa la Tekoa. Walipoanza safari, Yehoshafati akasimama akasema, “Nisikilizeni, enyi Yuda, na watu wa Yerusalemu! Mwaminini Bwana Mungu wenu, hivyo mtathibitika, wasadikini manabii wake nanyi mtafanikiwa.
21 Ensuite, il tint conseil avec le peuple; puis, il plaça en tête de l'armée, comme elle sortait, des chantres harpistes pour célébrer et louer les choses saintes, et ils disaient: Rendez gloire au Seigneur, car sa miséricorde est éternelle.
Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema: “Mshukuruni Bwana kwa kuwa upendo wake wadumu milele.”
22 Et, au moment où ils commençaient à chanter ses louanges, le Seigneur excita la guerre entre les fils d'Ammon et Moab, d'une part, et ceux de la montagne de Seïr, d'autre part; ils avaient tous marché sur Israël, et ils se tournèrent les uns contre les autres.
Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.
23 Les fils d'Ammon et Moab se levèrent pour exterminer ceux de la montagne de Seïr, et, quand ils les eurent broyés, ils s'attaquèrent mutuellement, de sorte qu'ils se détruisirent.
Watu wa Amoni na Moabu wakawainukia watu wa Mlima Seiri ili kuwaua na kuwaangamiza kabisa. Baada ya kumaliza kuwachinja watu wa Seiri, wakaangamizana wao kwa wao.
24 Lors donc que Juda arriva sur la hauteur d'où l'on découvre le désert, il regarda et il vit cette multitude, et voilà qu'ils étaient tous tombés morts, et gisant à terre, pas un ne s'était échappé.
Yuda walipofika katika mnara wa ulinzi wa jangwani, wakaliangalia lile jeshi kubwa, wakaona ni maiti tupu zimetapakaa ardhini, wala hakuna yeyote aliyenusurika.
25 Et Josaphat avec tout son peuple descendit pour recueillir les dépouilles; ils trouvèrent quantité de bétail, des bagages, des couvertures et des choses précieuses; ils les prirent et ils mirent trois jours à recueillir le butin, tant il y en avait.
Hivyo Yehoshafati na watu wake wakaenda kujitwalia nyara kutoka kwao, nao wakakuta humo wingi wa mifugo, mali, nguo na vitu vya thamani, ambavyo vilikuwa vingi zaidi ya vile walivyoweza kuchukua. Wakakusanya nyara kwa siku tatu kwa sababu zilikuwa nyingi mno.
26 Le quatrième jour, ils reprirent leurs rangs dans le val de la bénédiction; car, en ce lieu, ils bénirent le Seigneur; à cause de cela cette vallée est appelée encore de nos jours la Vallée de la Bénédiction.
Siku ya nne wakakusanyika katika Bonde la Beraka kwa maana huko ndiko walikomsifu Bwana. Ndiyo sababu linaitwa Bonde la Beraka mpaka leo.
27 Et tout Juda, Josaphat à sa tête, revint à Jérusalem avec une grande allégresse, car le Seigneur les avait comblés de joie aux dépens de leurs ennemis.
Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kwa kuwa Bwana alikuwa amewasababisha wafurahi juu ya adui zao.
28 Et ils entrèrent à Jérusalem au son des harpes et des cithares, auxquelles se joignirent les trompettes quand ils arrivèrent au temple du Seigneur.
Wakaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni mwa Bwana wakiwa na vinubi, zeze na tarumbeta.
29 Et il y eut un grand trouble venant du Seigneur, parmi tous les royaumes de la terre, quand ils surent que le Seigneur avait combattu les ennemis d'Israël.
Hofu ya Mungu ikazipata falme zote za nchi waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa amepigana dhidi ya adui za Israeli.
30 Ainsi le royaume de Josaphat fut en paix; car le Seigneur, alentour, apaisa tout.
Ufalme wa Yehoshafati ukawa na amani, kwa kuwa Mungu wake alikuwa amemstarehesha pande zote.
31 Et Josaphat régna en Jérusalem; il avait trente-cinq ans lorsqu'il monta sur le trône, et son règne dura vingt-cinq ans. Sa mère s'appelait Azuba, fille de Sali.
Hivyo Yehoshafati akatawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala katika Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
32 Et il marcha dans les voies d'Asa, son père, et il ne s'en détourna pas, et il fit ce qui est droit aux yeux du Seigneur.
Alienenda katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana.
33 Cependant, les hauts lieux subsistèrent encore, et le peuple ne dirigea pas encore son cœur vers le Seigneur Dieu de ses pères.
Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa, na watu wakawa bado hawajaelekeza mioyo yao kwa Mungu wa baba zao.
34 Le reste des actes de Josaphat, des premiers et des derniers, est compris dans les récits de Jéhu, fils d'Anani, qui écrivit le livre des Rois d'Israël.
Matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Yehu mwana wa Hanani, ambazo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.
35 Après cela, Josaphat, roi de Juda, fit alliance avec Ochozias, roi d'Israël, et il pécha,
Hatimaye Yehoshafati mfalme wa Yuda akafanya urafiki na Ahazia mfalme wa Israeli ambaye alifanya maovu sana.
36 En agissant et en marchant avec lui pour construire une flotte qui partit d'Asion-Gaber, allant à Tharsis.
Akaungana naye kutengeneza meli nyingi za kwenda Tarshishi, nazo zilitengenezwa huko Esion-Geberi.
37 Alors, Eliézer, fils de Dodia de Marine, prophétisa contre Josaphat, disant: Parce que tu t'es lié avec Ochosias, le Seigneur a détruit ton ouvrage; il a brisé ta flotte, et elle n'a pu aller jusqu'à Tharsis.
Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akasema, “Kwa kuwa umeungana na Ahazia, Bwana ataangamiza vile mlivyotengeneza.” Zile meli zikavunjika na hazikuweza kungʼoa nanga ili kwenda Tarshishi.

< 2 Chroniques 20 >