< 2 Chroniques 18 >

1 La gloire et la richesse de Josaphat s'accrurent encore, et il s'allia par un mariage à la famille d'Achab.
Basi, Yehoshafati alikuwa na mali nyingi sana na heshima. Naye akafanya urafiki na Ahabu kwa mwanawe kumwoa binti wa Ahabu.
2 Au bout de quelques années, il alla voir Achab en Samarie, et Achab immola, pour lui et sa suite, quantité de bœufs et de brebis; il lui fit beaucoup d'amitiés pour l'emmener avec lui contre Ramoth-Galaad.
Baada ya miaka kadhaa akashuka kumtembelea Ahabu huko Samaria. Ahabu akachinja ngʼombe na kondoo wengi kwa ajili yake na watu aliokuwa amefuatana nao. Kisha Ahabu akamshawishi Yehoshafati kukwea pamoja naye ili kuishambulia Ramoth-Gileadi.
3 Et Achab, roi d'Israël, dit à Josaphat, roi de Juda: Viendras-tu avec moi à Ramoth-Galaad? L'autre répondit: Comme tu es, je suis; mon peuple est comme ton peuple, il fera la guerre comme lui.
Ahabu mfalme wa Israeli akamuuliza Yehoshafati mfalme wa Yuda, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako. Tutakuwa pamoja nawe vitani.”
4 Et Josaphat dit au roi d'Israël: Consulte aujourd'hui le Seigneur.
Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
5 Et le roi d'Israël rassembla tous les prophètes, au nombre de quatre cents, et il leur dit: Irai-je en guerre à Ramoth-Galaad, ou m'abstiendrai-je? Et ils répondirent: Marche, le Seigneur les livrera aux mains du roi.
Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda kwa kuwa Mungu ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
6 Et Josaphat dit: N'y a-t-il plus ici un seul prophète du Seigneur par qui nous puissions consulter?
Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
7 Et le roi d'Israël répondit à Josaphat: Il y a encore un homme par qui l'on peut consulter le Seigneur; mais je le hais, parce que, à mon sujet, il ne prophétise jamais le bien, mais toujours le mal. C'est Michée, fils de Semis. Et Josaphat reprit: Que le roi ne tienne pas un tel langage.
Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
8 Et le roi appela un eunuque, et il dit: Fais venir tout de suite Michée, fils de Semis.
Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
9 Or, le roi d'Israël et Josaphat, roi de Juda, revêtus de robes, étaient assis chacun sur son trône, sur l'esplanade de la porte de Samarie, et tous les prophètes prophétisaient devant eux.
Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
10 L'un d'eux, Sédécias, fils de Chanaan, s'était fait des cornes de fer, et il dit: Voici ce que dit le Seigneur: Avec ces cornes tu frapperas la Syrie jusqu'à ce qu'elle soit abattue.
Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
11 Et tous les prophètes prédisaient ainsi: Marche sur Ramoth-Galaad, et tu réussiras, et le Seigneur livrera à tes mains le roi de Syrie.
Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho, wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
12 Et le messager qui était allé querir Michée dit à celui-ci: Tous les prophètes n'ont qu'une voix pour dire de bonnes choses concernant le roi; que tes paroles soient comme celles de l'un d'eux, et tu auras bien parlé.
Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
13 Mais Michée répondit: Vive le Seigneur! ce que le Seigneur me dira, je le répèterai.
Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
14 Et il alla devant le roi, et le roi lui dit: Michée, dois je aller en guerre à Ramoth-Galaad, ou m'en abstenir? Et il répondit: Marche, et tu réussiras, et ils te seront livrés.
Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa watatiwa mkononi mwako.”
15 Et le roi lui dit: Combien de fois t'adjurerai-je pour que tu ne me dises rien que la vérité au nom du Seigneur?
Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
16 Et Michée reprit: J'ai vu Israël dispersé sur les montagnes, comme un troupeau sans pasteur. Et le Seigneur a dit: Ces hommes n'ont point de chef, que chacun retourne en paix dans sa maison.
Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
17 Et le roi d'Israël dit à Josaphat, roi de Juda: Ne t'ai-je point dit qu'à mon sujet il ne prophétisait jamais le bien, mais toujours le mal?
Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu bali mabaya tu?”
18 Michée reprit: Il n'en est pas ainsi; écoutez la parole du Seigneur: J'ai vu le Seigneur assis sur son trône, et toute l'armée du ciel se tenait auprès de lui à sa droite et à sa gauche.
Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama upande wa kulia na wa kushoto.
19 Et le Seigneur a dit: Qui trompera Achab, roi d'Israël, pour qu'il parte et succombe à Ramoth-Galaad? Et l'un répondit au Seigneur d'une sorte, l'autre différemment.
Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu, mfalme wa Israeli, ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
20 Et l'esprit sortit des rangs, et il se plaça devant le Seigneur, et il dit: C'est moi qui le tromperai. Et le Seigneur reprit: De quelle manière?
Mwishoni, roho akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’ “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’
21 Et il dit: Je partirai, et je serai un esprit trompeur en la bouche de tous ses prophètes. Et le Seigneur dit: Tu le tromperas, et tu prévaudras; va, et fais ce que tu as dit.
“Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
22 Maintenant donc, voici que le Seigneur a placé un esprit trompeur en la bouche de tous tes prophètes, et le Seigneur t'a annoncé le mal.
“Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
23 Alors, Sédécias le Chananéen s'avança, frappa Michée à la joue, et dit: Par quel chemin l'Esprit du Seigneur est-il sorti de moi pour te parler à toi?
Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
24 Et Michée reprit: Tu le verras le jour où tu passeras de chambre en chambre pour te cacher.
Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
25 Et le roi d'Israël s'écria: Que l'on saisisse Michée; menez-le chez Emer, gouverneur de la ville, et chez le prince Joas, fils du roi,
Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
26 Et dites: Voici ce que dit le roi: Emprisonnez cet homme; qu'il se nourrisse du pain et de l'eau de l'affiction jusqu'à je revienne en paix.
Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
27 Et Michée reprit: Si tu reviens en paix, le Seigneur n'a point parlé par ma bouche. Et il ajouta: Peuple, écoutez-moi tous.
Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
28 Après cela, le roi d'Israël partit avec Josaphat, roi de Juda, pour Ramoth-Galaad.
Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
29 Et le roi d'Israël dit au roi de Juda: Aide-moi à me déguiser, et j'engagerai la bataille, et toi tu auras mes vêtements. Le roi d'Israël se déguisa donc, et il engagea la bataille.
Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
30 Et le roi de Syrie donna cet ordre aux chefs des chars qui l'accompagnaient: N'attaquez ni petit ni grand, mais le seul roi d'Israël.
Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
31 Et ceci advint: quand les chefs des chars virent Josaphat, roi de Juda, ils se dirent: C'est le roi d'Israël. Et ils l'entourèrent pour l'attaquer; mais Josaphat cria au Seigneur, et le Seigneur voulut le sauver, et Dieu les détourna de lui.
Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati, wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele, naye Bwana akamsaidia. Mungu akawaondoa kwake,
32 Et quand les chefs des chars virent que ce n'était pas le roi d'Israël, ils s'éloignèrent de lui.
wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli nao wakaacha kumfuatilia.
33 Alors, un homme adroit, ayant tendu son arc, frappa le roi d'Israël au flanc, au défaut de la cuirasse; et le roi dit à son cocher: Tourne bride, emmène-moi hors de la mêlée, car j'ai une blessure.
Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma, mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
34 Et la bataille fut perdue pour lui ce jour-là, et il resta jusqu'au soir sur son char, en face de l'armée syrienne, et, au soleil couchant, il mourut.
Vita vikaendelea mchana kutwa, naye mfalme wa Israeli akajitegemeza ndani ya gari lake kuwaelekea Waaramu hadi jioni. Basi jioni yake akafa.

< 2 Chroniques 18 >