< 1 Samuel 21 >
1 David se rendit à Nomba chez le prêtre Abimélech; Abimélech, étonné de sa venue, lui dit: Pourquoi es-tu seul, et n'y a-t-il personne avec toi?
Daudi akaenda Nobu, kwa Ahimeleki kuhani. Ahimeleki akatetemeka alipokutana naye, akamuuliza, “Kwa nini uko peke yako? Kwa nini hukufuatana na mtu yeyote?”
2 David dit au prêtre: Le roi aujourd'hui m'a donné ce commandement: Que nul ne sache l'affaire pour laquelle je t'envoie, et dont je te charge. J'ai donc convoqué mes serviteurs au lieu dit la Foi de Dieu (Phellani-Maimoni).
Daudi akamjibu Ahimeleki kuhani, akisema, “Mfalme ameniagiza shughuli fulani na kuniambia, ‘Mtu yeyote asijue chochote kuhusu kazi yako wala maagizo yako!’ Kuhusu watu wangu, nimewaambia tukutane mahali fulani.
3 Maintenant, as-tu sous la main cinq pains? Donne-moi ce que tu pourras trouver.
Sasa basi, una nini mkononi? Nipatie mikate mitano au chochote unachoweza kupata.”
4 Le prêtre répondit à David, et il lui dit: Je n'ai point sous la main de pains profanes, je n'ai que des pains consacrés; si tes gens se sont au moins abstenus de femmes, ils en peuvent manger.
Lakini kuhani akamjibu Daudi, “Sina mkate wowote wa kawaida kwa sasa. Hata hivyo, ipo hapa mikate iliyowekwa wakfu, iwapo watu wamejitenga na wanawake.”
5 David reprit: Quant aux femmes, depuis trois jours, nous nous en sommes abstenus; lorsque je suis parti, tous mes hommes ont été purifiés; mais la route elle-même les souille; c'est pourquoi nous nous purifions aujourd'hui en lavant nos vêtements.
Daudi akajibu, “Hakika tumejitenga na wanawake kwa siku hizi chache kama kawaida ya ninapotoka kwenda kwenye shughuli. Navyo vyombo vya wale vijana huwa ni vitakatifu hata kwenye safari ya kawaida, si zaidi sana leo vyombo vyao vitakuwa ni vitakatifu?”
6 Alors, Abimélech le prêtre lui donna les pains de proposition; car il n'y avait là d'autres pains que ceux qu'on venait d'ôter de devant la face du Seigneur, pour les remplacer par des pains chauds, le jour même où David les prit.
Hivyo kuhani akampa ile mikate iliyowekwa wakfu, kwa kuwa hapakuwepo mikate mingine isipokuwa hiyo ya Wonyesho iliyokuwa imeondolewa hapo mbele za Bwana na kubadilishwa na mingine yenye moto siku ile ilipoondolewa.
7 Or, il se trouvait là un serviteur de Saül, retenu devant le Seigneur; il se nommait Doeg le Syrien, et il faisait paître les mulets de Saül.
Basi siku hiyo palikuwepo na mmoja wa watumishi wa Sauli, aliyezuiliwa mbele za Bwana; alikuwa Doegi Mwedomu, kiongozi wa wachunga wanyama wa Sauli.
8 Et David dit à Abimélech: Vois si tu as ici sous la main quelque javeline ou quelque épée; car je n'ai pris ni mon glaive ni aucune arme, tant l'affaire du roi exigeait de précipitation.
Daudi akamuuliza Ahimeleki, “Je, unao mkuki au upanga hapa? Sikuleta upanga wala silaha nyingine yoyote, kwa sababu shughuli ya mfalme ilikuwa ya haraka.”
9 Et le prêtre dit: Voici l'épée de Goliath le Philistin, que tu as vaincu dans le vallon d'Ela; elle est enveloppée dans un manteau; si tu la veux, tu peux l'emporter; hormis cette arme, il n'en est aucune ici. A quoi David répondit: Donne-la-moi; elle n'a pas sa pareille.
Kuhani akajibu, “Upanga wa Goliathi Mfilisti, ambaye ulimuua katika Bonde la Ela, upo hapa, umefungiwa katika kitambaa nyuma ya kisibau. Kama unauhitaji, uchukue, hakuna upanga mwingine hapa ila huo tu.” Daudi akasema, “Hakuna upanga mwingine kama huo. Nipatie huo.”
10 Le prêtre la lui donna, et David partit. Ce jour-là, il s'enfuit loin de Saül, et il alla chez Achis, roi de Geth.
Siku ile Daudi akamkimbia Sauli na kwenda kwa Akishi mfalme wa Gathi.
11 Et les serviteurs d'Achis dirent à leur maître: N'est-ce point là David, le roi de la terre? N'est-ce pas celui dont les danseuses, en chantant, disaient: Saül les a tués par milliers, David les a tués par myriades?
Lakini watumishi wa Akishi wakamwambia, “Je, huyu si ndiye Daudi mfalme wa nchi? Je, huyu si ndiye yule ambaye wanaimba katika ngoma zao wakisema: “‘Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake’?”
12 Et David pesa ces paroles en son cœur, et il eut grande crainte en présence du roi Achis.
Daudi akayaweka maneno haya moyoni naye akamwogopa sana Akishi mfalme wa Gathi.
13 Aussitôt, devant lui, il se donna un nouvel aspect, et, ce jour-là, il usa de feinte; il tambourina sur les portes de la ville; il fit de ses mains des gestes insensés; il tomba contre les battants des portes, et l'écume ruisselait sur sa barbe.
Basi akajifanya mwendawazimu mbele yao; naye alipokuwa mikononi mwao, alitenda kama kichaa, akikwaruza kwa kutia alama juu ya milango ya lango na kuachia udelele kutiririka kwenye ndevu zake.
14 Et Achis dit à ses serviteurs: Voyez, cet homme est épileptique. Pourquoi me l'avez-vous amené?
Akishi akawaambia watumishi wake, “Tazameni mtu huyu! Ana wazimu! Kwa nini mnamleta kwangu?
15 Ai-je besoin d'épileptiques? A quoi bon l'avoir amené pour qu'il tombe en épilepsie devant moi? Il n'entrera pas dans ma maison.
Je, mimi nimepungukiwa na wenda wazimu kiasi kwamba mmeniletea mtu huyo hapa aendelee kufanya hivi mbele yangu? Je, ilikuwa ni lazima mtu huyo aje nyumbani kwangu?”