< 1 Samuel 15 >

1 Et Samuel dit à Saül: Le Seigneur m'a jadis envoyé pour t'oindre roi d'Israël; maintenant, écoute la voix du Seigneur.
Samweli akamwambia Sauli, “Mimi ndiye ambaye Bwana alinituma nikutie mafuta uwe mfalme juu ya watu wake Israeli, basi sasa sikiliza ujumbe kutoka kwa Bwana.
2 Voici ce que dit le Seigneur sabaoth: Je veux tirer vengeance de ce qu'a fait Amalec contre Israël lorsqu'il est venu à sa rencontre sur sa voie, comme il revenait d'Égypte.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu Waamaleki kwa kile walichowatendea Israeli walipowavizia wakati walipanda kutoka Misri.
3 Marche donc, et tu frapperas Amalec et Hiérim, et ce qui lui appartient; tu ne t'en approprieras rien, tu extermineras tout. Amalec sera anathème avec tout ce qui lui appartient; tu n'en épargneras aucune chose. Tu mettras à mort hommes et femmes, nourrissons et nourrices, bœufs et brebis, chamelles et ânesses.
Basi sasa nenda ukawashambulie Waamaleki na kuwaangamiza kabisa pamoja na kila kitu kilicho mali yao. Usiwahurumie; waue wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, ngʼombe na kondoo, ngamia na punda.’”
4 Et Saül convoqua le peuple, et il passa en revue, à Galgala, quatre cent mille combattants, outre trente mille hommes de Juda.
Ndipo Sauli akawaita watu na kuwapanga huko Telaimu, askari wa miguu 200,000 pamoja na watu 10,000 kutoka Yuda.
5 Puis, Saül marcha sur la ville d'Amalec, et il se mit en embuscade dans le torrent.
Sauli akaenda katika mji wa Amaleki na kuwavizia bondeni.
6 Et Saül dit au Cénéen: Éloigne-toi et te sépare des Amalécites, de peur que je ne te confonde avec eux, car tu as été miséricordieux pour les fils d'Israël quand ils revenaient d'Égypte. Et le Cénéen se sépara d'Amalec.
Kisha akawaambia Wakeni, “Ondokeni, waacheni Waamaleki ili nisije nikawaangamiza ninyi pamoja nao, kwa kuwa ninyi mliwatendea mema Waisraeli wote wakati walipanda kutoka Misri.” Basi Wakeni wakaondoka, wakawaacha Waamaleki.
7 Et Saül battit Amalec, depuis Evilat jusqu'à Sur, en face de l'Égypte.
Ndipo Sauli akawashambulia Waamaleki toka Havila mpaka Shuri, hadi mashariki ya Misri.
8 Il prit vivant Agag, roi d'Amalec, et il passa au fil de l'épée tout le peuple, tout Hiérim.
Akamchukua Agagi, mfalme wa Waamaleki akiwa hai, nao watu wake wote akawaangamiza kabisa kwa upanga.
9 Mais Saül et tout le peuple laissèrent vivre Agag; ils épargnèrent ce qu'il y avait de meilleur parmi ses brebis, ses bœufs, ses vivres, le vin de ses vignes, tous ses biens; ils résolurent de ne les point détruire, et ils détruisirent toutes les choses viles ou de peu de valeur.
Lakini Sauli na hilo jeshi wakamhifadhi hai Agagi na kondoo na ngʼombe walio wazuri, mafahali na wana-kondoo walionona kila kitu kilichokuwa kizuri. Hivi vitu hawakuwa radhi kuviangamiza kabisa, bali kila kitu kilichodharauliwa na kilicho dhaifu wakakiangamiza kabisa.
10 Et la parole du Seigneur vint à Samuel, disant:
Kisha neno la Bwana likamjia Samweli kusema:
11 Je me reproche d'avoir fait roi Saül, parce qu'il a cessé de me suivre, et qu'il n'a point observé mes ordres; Samuel en fut abattu, et il cria toute la nuit au Seigneur.
“Ninasikitika kwamba nimemfanya Sauli kuwa mfalme, kwa sababu ameacha kunifuata mimi na hakutimiza maagizo yangu.” Samweli akafadhaika, naye akamlilia Bwana usiku ule wote.
12 Et Samuel se leva de grand matin; dès l'aurore, il partit à la rencontre d'Israël. On l'alla rapporter à Saül, disant: Samuel est arrivé au mont Carmel; il a levé une poignée d'hommes. A ce moment, Samuel tourna son char, et il descendit à Galgala vers Saül, comme celui-ci offrait en holocauste au Seigneur les prémices des dépouilles qu'il avait amenées d'Amalec.
Asubuhi na mapema Samweli akaamka kwenda kukutana na Sauli, lakini akaambiwa, “Sauli amekwenda Karmeli. Huko amesimamisha mnara kwa heshima yake mwenyewe naye ameendelea na kuteremkia Gilgali.”
13 Samuel s'approcha de Saül, et Saül lui dit: Béni sois-tu au nom du Seigneur, j'ai fait tout ce qu'a ordonné le Seigneur.
Samweli alipomfikia, Sauli akamwambia, “Bwana akubariki! Nimetimiza yale Bwana aliniagiza.”
14 Mais Samuel dit à Saül: Quels sont donc ces bêlements de brebis qui parviennent à mes oreilles, et ces mugissements de bœufs que je viens d'entendre?
Lakini Samweli akasema, “Nini basi huu mlio wa kondoo masikioni mwangu? Huu mlio wa ngʼombe ninaousikia ni kitu gani?”
15 Et Saül lui dit: J'ai amené ce bétail d'Amalec; le peuple a épargné les plus belles têtes pour les sacrifier au Seigneur; j'ai détruit tout le reste.
Sauli akajibu, “Askari wamewaleta kutoka kwa Waamaleki, waliwaacha wale kondoo na ngʼombe wazuri ili kuwatoa dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, lakini tuliwaangamiza kabisa wengine wote.”
16 Alors, Samuel dit à Saül: Permets, je vais te dévoiler ce que cette nuit m'a dit le Seigneur. Et Saül répondit: Parle.
Samweli akamwambia Sauli, “Ngoja! Nami nitakuambia lile Bwana aliloniambia usiku huu.” Sauli akajibu, “Niambie.”
17 Et Samuel dit à Saül: N'es-tu point petit à ses yeux, toi qui règnes sur les tribus d'Israël? C'est le Seigneur qui t'a sacré roi.
Samweli akamwambia, “Ingawa zamani ulijiona mdogo machoni pako mwenyewe, Je, hukuwa kiongozi wa kabila za Israeli? Bwana alikutia mafuta kuwa mfalme juu ya Israeli.
18 Et le Seigneur t'a envoyé contre Amalec, et il t'a dit: Marche, et extermine. Mets à mort ce peuple qui a péché contre moi; fais-lui la guerre jusqu'à ce que tu l'aies détruit.
Naye akakutuma kwa kazi maalum, akisema, ‘Nenda ukaangamize kabisa wale watu waovu, wale Waamaleki, upigane nao vita mpaka utakapowaangamiza kabisa.’
19 Pourquoi donc n'as-tu pas été docile à la voix du Seigneur? Pourquoi as- tu pris sur toi de disposer du butin? Pourquoi as-tu fait le mal devant le Seigneur?
Kwa nini hukumtii Bwana? Kwa nini ulivamia nyara na kufanya uovu machoni pa Bwana?”
20 C'est, reprit Saül, pour avoir écouté la clameur du peuple; je suivais la voie que m'avait indiquée le Seigneur; j'avais fait prisonnier Agag, et exterminé Amalec;
Sauli akasema, “Lakini nilimtii Bwana. Nilikamilisha ile kazi ambayo Bwana alinituma. Niliwaangamiza Waamaleki kabisa na kumleta Agagi mfalme wao.
21 Mais le peuple prit des dépouilles ce qu'il y avait de meilleur, parmi les brebis et les bœufs, pour les sacrifier, en Galgala, au Seigneur notre Dieu.
Askari walichukua kondoo na ngʼombe kutoka kwenye nyara, zile ambazo ni nzuri sana zimewekwa wakfu kwa Mungu, ili zitolewe dhabihu kwa Bwana Mungu wako huko Gilgali.”
22 Les holocaustes, dit Samuel, et les victimes sont-ils plus agréables au Seigneur que l'obéissance à sa voix? La docilité vaut mieux que les offrandes; l'obéissance vaut mieux que la graisse des béliers.
Lakini Samweli akajibu: “Je, Bwana anafurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama vile kuitii sauti ya Bwana? Kutii ni bora zaidi kuliko dhabihu, nako kusikia ni bora kuliko mafuta ya kondoo dume.
23 La désobéissance est un péché comme la divination; les theraphim amènent peines et douleurs. Parce que tu as dédaigné la parole du Seigneur, le Seigneur te rejettera du trône d'Israël.
Kwa maana kuasi ni kama dhambi ya uaguzi, nao ukaidi ni kama uovu wa kuabudu sanamu. Kwa sababu umelikataa neno la Bwana, naye amekukataa wewe kuendelea kuwa mfalme.”
24 J'ai péché, répondit Saül, en transgressant l'ordre du Seigneur et le tien; j'ai eu crainte du peuple, et j'ai écouté sa clameur.
Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Nimetenda dhambi. Nimevunja amri ya Bwana na maagizo yako. Niliwaogopa watu na kwa hiyo nikafanya walivyotaka.
25 Maintenant, ôte-moi mon péché, reviens avec moi, et j'adorerai le Seigneur ton Dieu.
Sasa ninakusihi usamehe dhambi yangu, nawe urudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana.”
26 Mais Samuel dit à Saül: Je ne reviendrai plus vers toi; parce que tu as méprisé la parole du Seigneur, le Seigneur te méprisera; tu ne seras plus roi d'Israël.
Lakini Samweli akamwambia, “Sitarudi pamoja nawe. Umelikataa neno la Bwana, naye Bwana amekukataa wewe, usiendelee kuwa mfalme juu ya Israeli!”
27 Et Samuel se retourna pour partir, mais Saül saisit le pan de son double manteau, et il le déchira.
Samweli alipogeuka ili aondoke, Sauli akangʼangʼania pindo la joho lake, nalo likararuka.
28 Et Samuel lui dit: Le Seigneur, par tes mains, a déchiré aujourd'hui ta royauté en Israël; il la donnera à ton prochain qui vaut mieux que toi.
Samweli akamwambia, “Bwana ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako leo, naye ameutia kwa mmoja wa majirani zako, aliye bora kuliko wewe.
29 Israël aussi sera déchiré en deux parts; le Seigneur ne changera pas, et il ne se repentira pas; car il n'est point comme un homme pour se repentir.
Yeye aliye Utukufu wa Israeli hasemi uongo wala hana kigeugeu; kwa kuwa yeye si mwanadamu, hata abadili nia yake.”
30 Et Saül dit: J'ai péché; mais ne laisse pas de m'honorer devant les anciens d'Israël et devant mon peuple; viens-t'en avec moi, et j'adorerai ton Dieu.
Sauli akajibu, “Nimetenda dhambi. Lakini tafadhali niheshimu mbele ya wazee wa watu wangu na mbele ya Israeli; rudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana Mungu wako.”
31 Et Samuel revint auprès de Saül, et celui-ci adora le Seigneur.
Hivyo Samweli akarudi pamoja na Sauli, naye Sauli akamwabudu Bwana.
32 Samuel dit ensuite: Amenez-moi Agag, roi d'Amalec; et Agag arriva tout tremblant. Et Agag dit: Faut-il que la mort soit si amère?
Ndipo Samweli akasema, “Niletee Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akaja kwake kwa ujasiri, akifikiri, “Hakika uchungu wa mauti umepita.”
33 Et Samuel dit à Agag: De même que par ton glaive les femmes sont restées sans enfants, ta mère, parmi les femmes, tout à l'heure n'aura plus d'enfant. Et Samuel égorgea Agag devant le Seigneur, à Galgala.
Lakini Samweli akasema, “Kama upanga wako ulivyofanya wanawake kufiwa na watoto wao, ndivyo mama yako atakavyokuwa hana mtoto miongoni mwa wanawake.” Naye Samweli akamuua Agagi mbele za Bwana huko Gilgali.
34 Puis, Samuel retourna en Armathem, et Saül partit pour sa demeure à Gabaa.
Kisha Samweli akaenda Rama, lakini Sauli akapanda nyumbani kwake huko Gibea ya Sauli.
35 Et Samuel cessa de visiter Saül jusqu'au jour de sa mort; mais il pleurait sur lui, parce que le Seigneur s'était repenti d'avoir fait Saül roi d'Israël.
Hadi siku Samweli alipofariki hakwenda kumwona Sauli tena, ingawa Samweli alimwombolezea. Naye Bwana alihuzunika kwamba alimfanya Sauli kuwa mfalme juu ya Israeli.

< 1 Samuel 15 >