< 1 Samuel 13 >

1 Après cela, Saül choisit trois mille hommes, parmi ceux d'Israël. Il y en eut avec lui deux mille à Machmas et en la montagne de Béthel, et avec Jonathan mille, à Gabaa en Benjamin. Le reste du peuple fut congédié, et chacun retourna en sa demeure.
Sauli alikuwa na miaka thelathini, alipokuwa mfalme, akatawala Israeli miaka arobaini na miwili.
2 Après cela, Saül choisit trois mille hommes, parmi ceux d'Israël. Il y en eut avec lui deux mille à Machmas et en la montagne de Béthel, et avec Jonathan mille, à Gabaa en Benjamin. Le reste du peuple fut congédié, et chacun retourna en sa demeure.
Sauli alichagua watu 3,000 kutoka Israeli; miongoni mwa hao watu 2,000 walikuwa pamoja naye huko Mikmashi na katika nchi ya vilima ya Betheli, nao watu 1,000 walikuwa pamoja na Yonathani huko Gibea ya Benyamini. Watu waliosalia aliwarudisha nyumbani mwao.
3 Jonathan battit le Nasib, étranger qui demeurait sur la colline; les Philistins l'apprirent, et Saül fit retentir la trompette en toute la terre promise, disant: Les esclaves secouent le joug.
Yonathani akashambulia ngome ya Wafilisti huko Geba, nao Wafilisti wakapata habari hizo. Kisha Sauli akaamuru tarumbeta ipigwe nchi yote na kusema, “Waebrania na wasikie!”
4 Et tout Israël écouta ceux qui publiaient: Saül a détruit le Nasib étranger; et Israël se souleva contre les Philistins, et tous les fils d'Israël suivirent Saül en Galgala.
Hivyo Israeli wote wakasikia habari kwamba: “Sauli ameshambulia ngome ya Wafilisti, nao sasa Israeli wamekuwa harufu mbaya kwa Wafilisti.” Basi watu waliitwa kuungana na Sauli huko Gilgali.
5 Cependant, les Philistins se réunirent pour porter la guerre en Israël; ils firent marcher contre Israël trente mille chars, six mille cavaliers et des piétons nombreux comme le sable de la mer; ils campèrent à Machmas, en face de Béthoron du Midi.
Wafilisti wakakusanyika ili kupigana na Israeli, wakiwa na magari ya vita 3,000, waendesha magari ya vita 6,000 na askari wa miguu wengi kama mchanga wa ufuoni mwa bahari. Walipanda na kupiga kambi huko Mikmashi, mashariki ya Beth-Aveni.
6 Or, Israël vit qu'il était trop faible pour les aborder; et le peuple se cacha dans les cavernes, dans les lieux fermés, dans les rochers, dans les puits, dans les citernes.
Watu wa Israeli walipoona kuwa hali yao ni ya hatari na kuwa jeshi lao limesongwa sana, wakajificha katika mapango na katika vichaka, katikati ya miamba, kwenye mashimo na kwenye mahandaki.
7 Ceux qui avaient passé le Jourdain le traversèrent encore pour se réfugier dans les territoires de Gad et de Galaad. Et Saül était encore à Galgala, et toute la troupe qui le suivait était frappée d'effroi.
Hata baadhi ya Waebrania wakavuka Yordani mpaka nchi ya Gadi na Gileadi. Sauli akabaki huko Gilgali, navyo vikosi vyote vilivyokuwa pamoja naye vilikuwa vikitetemeka kwa hofu.
8 Il laissa écouler sept jours, comme le lui avait dit Samuel; mais Samuel ne vint pas le trouver en Galgala, et la troupe qui l'entourait se dispersa.
Akangoja kwa siku saba, muda uliowekwa na Samweli; lakini Samweli hakuja Gilgali, nao watu wa Sauli wakaanza kutawanyika.
9 Et Saül dit: Amenez ici des victimes pour que je prépare un holocauste et des hosties pacifiques; puis, il offrit l'holocauste.
Basi akasema, “Nileteeni hapa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani.” Naye Sauli akatoa sadaka ya kuteketezwa.
10 Comme il achevait le sacrifice, Samuel arriva, et Saül sortit à sa rencontre afin de lui rendre hommage.
Mara alipomaliza kutoa hiyo sadaka, Samweli akatokea, naye Sauli akaondoka kwenda kumlaki.
11 Et Samuel dit: Qu'as-tu fait? Et Saül répondit: J'ai vu que le peuple autour de moi se dispersait, que tu n'étais point venu au temps indiqué, et que les Philistins étaient réunis à Machmas,
Samweli akamuuliza, “Umefanya nini?” Sauli akajibu, “Nilipoona kwamba watu wanatawanyika, na kwamba hukuja wakati uliopangwa na kwamba Wafilisti walikuwa wakikusanyika huko Mikmashi,
12 Et j'ai dit: Maintenant les Philistins vont descendre sur moi à Galgala et je n'ai point prié devant le Seigneur: je me suis donc résolu à offrir l'holocauste.
nikawaza, ‘Sasa Wafilisti watateremka dhidi yangu huko Gilgali nami sijaomba kibali kwa Bwana.’ Hivyo nikalazimika kutoa sadaka ya kuteketezwa.”
13 Et Samuel dit à Saül: Tu as agi en insensé, car tu n'as point obéi à mon ordre, à l'ordre du Seigneur, au moment où le Seigneur t'avait préparé sur son peuple une royauté perpétuelle.
Samweli akasema, “Umetenda kwa upumbavu. Hukuyashika maagizo ya Bwana Mungu wako aliyokupa. Kama ungelitii, angeudumisha ufalme wako juu ya Israeli kwa wakati wote.
14 Maintenant donc cette royauté ne te restera pas, et Dieu se cherchera un homme selon son cœur; et le Seigneur le chargera de gouverner son peuple, parce que tu n'as pas observé le commandement du Seigneur.
Lakini sasa ufalme wako hautadumu; Bwana amemtafuta mtu aupendezaye moyo wake, na amemchagua awe kiongozi wa watu wake, kwa sababu hukuyatii maagizo ya Bwana.”
15 Et Samuel partit, il quitta Galgala, et ce qu'il y avait encore là de peuple suivit Saül pour rejoindre les hommes de guerre. Quand ils furent arrivés de Galgala en Gabaa, Saül passa en revue la troupe qui se trouvait avec lui; elle était réduite à six cents hommes.
Kisha Samweli akaondoka Gilgali, akapanda Gibea ya Benyamini, naye Sauli akawahesabu watu aliokuwa nao. Jumla yao walikuwa watu 600.
16 Et Saül, avec son fils Jonathan et la troupe qui les avait suivis, s'arrêta à Gabaa en Benjamin, où tous pleurèrent; cependant les Philistins étaient campés à Machmas.
Sauli, mwanawe Yonathani na watu waliokuwa pamoja nao walikuwa wakiishi huko Gibea ya Benyamini, wakati Wafilisti wakiwa wamepiga kambi huko Mikmashi.
17 Et ceux-ci, portant avec eux le ravage, sortirent de leur camp en trois troupes: l'une prit le chemin de Gophera sur le territoire de Sogal.
Makundi ya wavamiaji walikuja kutoka kambi ya Wafilisti katika vikosi vitatu. Kikosi kimoja kilielekea Ofra karibu na Shuali,
18 Une autre prit la route de Béthoron; la troisième, le chemin de Gabaa, qui fait un détour vers Haï des Sabim.
kikosi kingine kilielekea Beth-Horoni, nacho kikosi cha tatu kilielekea kwenye nchi ya mpakani ielekeayo Bonde la Seboimu linalotazamana na jangwa.
19 Et, sur tout le territoire d'Israël, on ne trouvait pas un seul forgeron, parce que les Philistins avaient dit: Il ne faut pas que les Hébreux fabriquent lance ou épée.
Hapakuwa na mhunzi ambaye angeweza kupatikana katika nchi yote ya Israeli, kwa sababu Wafilisti walikuwa wamesema, “Waebrania wasije wakatengeneza panga au mikuki!”
20 Et tout Israël descendait chez les Philistins pour forger chacun sa faucille, ses outils, sa hache ou sa faux.
Hivyo Waisraeli wote huteremka kwa Wafilisti ili kunoa majembe ya plau, majembe ya mkono, mashoka na miundu.
21 On était près de vendanger; or, pour un outil à dents, il fallait payer trois sicles, et autant pour une hache ou pour une faux.
Bei ilikuwa fedha theluthi mbili za shekeli kunoa majembe ya plau na majembe ya mkono, na theluthi moja ya shekeli kwa nyuma, mashoka na michokoo.
22 Et, dans les jours de la guerre de Machmas, on ne trouva pas une épée ni une lance dans la main de l'un des fils d'Israël qui accompagnaient Saül et Jonathan; on n'en eût trouvé que dans les mains du roi et de son fils.
Kwa hiyo siku ya vita hakuna askari yeyote aliyekuwa kambini na Sauli na Yonathani ambaye alikuwa na upanga wala mkuki mkononi mwake; Sauli tu na mwanawe Yonathani ndio waliokuwa navyo.
23 Cependant, des Philistins étaient sortis du côté opposé au camp de Machmas.
Basi kikosi cha Wafilisti kilikuwa kimetoka kuelekea njia iendayo Mikmashi.

< 1 Samuel 13 >