< 1 Samuel 11 >

1 Environ un mois plus tard, Naas l'Ammonite, s'étant mis en marche, campa vers Jabès-Galaad. Tous les hommes de Jabès-Galaad lui dirent alors: Fais avec nous alliance, et nous te servirons.
Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
2 Mais Naas l'Ammonite leur dit: Je ferai alliance avec vous, à la condition de vous arracher à tous l'œil droit, et j'imposerai un opprobre à Israël.
Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
3 Les hommes de Jabès lui dirent: Accorde-nous sept jours; nous dépêcherons des envoyés sur tout le territoire d'Israël, et, si personne ne vient nous sauver, nous nous rendrons à toi.
Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
4 Et les messagers allèrent trouver Saül en Gabaa; ils répétèrent au peuple ces discours, et tout le peuple, élevant la voix, se prit à pleurer.
Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
5 Or, Saül à ce moment revenait des champs, après le matin, et il dit: Pourquoi le peuple pleure-t-il? On lui rapporta les paroles des hommes de Jabès.
Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
6 Lorsque Saül les eut entendues, l'Esprit du Seigneur s'élança sur lui, et, en son cœur, il se courrouça vivement contre l'Ammonite.
Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
7 Il prit deux vaches, et il les dépeça, et il envoya leurs membres sur tout le territoire d'Israël, par la main de messagers, disant: C'est ainsi que seront traités ceux qui ne marcheront pas avec Saül et avec Samuel. Un transport suscité par le Seigneur vint au peuple d'Israël, et il cria comme un seul homme.
Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
8 Et Saül les passa en revue à Bésech en Bama; il y avait d'Israël six cent mille hommes, et de Juda soixante-dix mille.
Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
9 Il dit alors aux messagers, qui étaient revenus: Portez ces paroles aux hommes de Jabès: A demain votre salut, au moment de la grande chaleur du soleil. Les messagers retournèrent à la ville, et racontèrent tout aux hommes de Jabès; ceux-ci en furent remplis de joie.
Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
10 Les hommes de Jabès dirent alors à Naas l'Ammonite: Demain, nous nous rendrons à vous, et vous nous traiterez comme bon vous semblera.
Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
11 Le lendemain, Saül divisa le peuple en trois corps; ils entrèrent dans le camp ennemi pendant la garde de l'aurore, et ils frappèrent les fils d'Ammon jusqu'à ce que le jour s'échauffât. Les survivants se dispersèrent, et il n'en resta pas deux ensemble.
Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
12 Et le peuple dit à Samuel: Qui donc prétendait que Saül ne règnerait pas sur nous? Livre-nous-les ces hommes, et nous les mettrons à mort.
Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
13 Mais Saül dit: Personne ne mourra en un jour où le Seigneur a sauvé Israël.
Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
14 Et Samuel dit au peuple: Allons à Galgala; nous inaugurerons en cette ville la royauté nouvelle.
Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
15 Tout le peuple se rendit à Galgala, et là, devant le Seigneur, Samuel sacra Saül comme roi; il y fit au Seigneur des sacrifices, et il y offrit des hosties pacifiques. Et Samuel et le peuple se réjouirent extrêmement.
Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.

< 1 Samuel 11 >