< 1 Samuel 10 >

1 Alors, Samuel prit une petite fiole d'huile, il la vida sur sa tête, il le baisa, et lui dit: Le Seigneur ne vient-il pas de t'oindre pour que tu sois chef de son peuple Israël? Tu règneras sur le peuple du Seigneur; tu le sauveras des mains de ses ennemis. Voici le signe à quoi tu reconnaîtras que tu es oint par le Seigneur, comme roi de son héritage:
Ndipo Samweli akachukua chupa ndogo ya mafuta na kuyamimina juu ya kichwa cha Sauli, akambusu, akisema, “Je, Bwana hakukutia mafuta uwe kiongozi juu ya watu wake Israeli?
2 Aussitôt qu'aujourd'hui tu te seras éloigné de moi, tu rencontreras, près du sépulcre de Rachel, en la montagne de Benjamin, deux hommes, courant à grands pas; ils te diront: On a retrouvé les ânesses que vous êtes allés chercher; ton père ne compte plus pour rien les ânesses, et il prépare grande chère, à cause de vous, disant: Que ferai-je pour mon fils?
Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na watu wawili karibu na kaburi la Raheli, huko Selsa kwenye mpaka wa Benyamini. Watakuambia, ‘Punda wale uliotoka kwenda kuwatafuta, wamekwisha kupatikana. Sasa baba yako ameacha kufikiri kuhusu punda na sasa ana hofu kukuhusu wewe. Anauliza, “Nitafanyaje kuhusu mwanangu?”’
3 Tu partiras de ce lieu; ensuite, tu iras jusqu'au chêne de Thabor; là, tu trouveras trois hommes montant vers le Seigneur en Béthel, et portant: l'un, trois chevreaux; le second, trois corbeilles pleines de pains; le troisième, une outre de vin.
“Kisha utakwenda mbele kutoka hapa mpaka uufikie mwaloni wa Tabori. Watu watatu wanaopanda kwa Mungu huko Betheli watakutana nawe hapo. Mmoja atakuwa amechukua wana-mbuzi watatu, mwingine mikate mitatu, na mwingine kiriba cha divai.
4 Ils te demanderont si tu vas bien, et te donneront deux de leurs pains, que tu accepteras.
Watakusalimu na kukupa mikate miwili, ambayo utaipokea kutoka kwao.
5 Après cela, tu arriveras sur la colline de Dieu, où les Philistins ont un tertre fortifié, et où réside le Nasib philistin; quand tu y seras entré, tu rencontreras un chœur de prophètes descendant du haut lieu, précédés d'instruments à cordes, de tambours et de flûtes; tous prophétisant.
“Baada ya hayo utakwenda Gibea ya Mungu, ambapo hapo kuna kambi ya Wafilisti. Unapokaribia mji utakutana na kundi la manabii wakiteremka kutoka mahali pa juu wakiwa na vinubi, matari, filimbi na zeze vikipigwa mbele yao, nao watakuwa wakitoa unabii.
6 Et l'esprit du Seigneur s'élancera sur toi; tu prophétiseras avec eux, et tu seras devenu un autre homme.
Roho wa Bwana atakuja juu yako kwa nguvu, nawe utatoa unabii pamoja nao; nawe utageuzwa kuwa mtu wa tofauti.
7 Lorsque tous ces signes seront venus, fais tout ce que te suggérera l'occasion, parce que Dieu sera avec toi.
Mara ishara hizi zitakapotimizwa, fanya lolote mkono wako upasao kufanya, kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe.
8 Tu descendras en face de Galgal, et je te rejoindrai pour offrir un holocauste et des hosties pacifiques; tu attendras mon arrivée sept jours; ensuite, je t'instruirai de tout ce que tu auras à faire.
“Tangulia kushuka mbele yangu mpaka Gilgali. Hakika nami nitateremka nikujie ili kutoa dhabihu za sadaka za kuteketezwa na dhabihu za amani, lakini lazima ungoje kwa siku saba hata nitakapokujia na kukuambia likupasalo kufanya.”
9 Dès que Saül se fut retourné pour s'éloigner de Samuel, Dieu changea son cœur, et, ce jour-là, tous les signes arrivèrent.
Ikawa Sauli alipogeuka kumwacha Samweli, Mungu aliubadilisha moyo wa Sauli, na ishara hizi zote zikatimizwa siku ile.
10 De ce lieu, il se rendit à la colline, il vit devant lui le chœur des prophètes, l'Esprit de Dieu s'élança sur lui; et il prophétisa au milieu d'eux.
Walipofika Gibea, akakutana na kundi la manabii. Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akajiunga nao katika kutoa unabii kwao.
11 Or, tous ceux qui le connaissaient précédemment, le virent; il était au milieu des prophètes; et, parmi le peuple, chacun dit à son voisin: Qu'est-il arrivé au fils de Cis? Saül aussi est-il au nombre des prophètes?
Ikawa wale wote waliomfahamu hapo mwanzo walipomwona akitoa unabii pamoja na manabii, wakaulizana, “Ni nini hiki kilichomtokea mwana wa Kishi? Je, Sauli naye pia yumo miongoni mwa manabii?”
12 L'un d'eux répondit, et il dit: Quel est donc son père? A cause de cela, ce mot est passé en proverbe: Saül aussi est-il au nombre des prophètes?
Mtu mmoja ambaye aliishi huko akajibu, “Je, naye baba yao ni nani?” Basi ikawa mithali, kusema, “Je, Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?”
13 Ensuite, il cessa de prophétiser, et il alla sur la colline à l'autel.
Baada ya Sauli kumaliza kutoa unabii, alikwenda mahali pa juu.
14 Et l'un de ses parents dit à lui et à son serviteur: Où êtes-vous allés? A quoi ils répondirent: Chercher les ânesses, mais nous ne les avons pas trouvées, et nous sommes entrés chez Samuel.
Basi babaye mdogo akamuuliza Sauli na mtumishi wake, “Je, mlikuwa wapi?” Akajibu, “Tulikuwa tukiwatafuta punda. Lakini tulipoona hawapatikani, tulikwenda kwa Samweli.”
15 Puis, le parent dit à Saül: Fais-moi connaître ce que t'a dit Samuel?
Babaye mdogo Sauli akasema, “Niambie Samweli amekuambia nini.”
16 Saül répondit: Que les ânesses étaient retrouvées; mais il ne lui dit rien de la royauté.
Sauli akajibu, “Alituhakikishia kwamba punda wamepatikana.” Lakini hakumwambia babaye mdogo kila kitu Samweli alichomwambia kuhusu ufalme.
17 Et Samuel convoqua tout le peuple devant le Seigneur, à Masphath.
Samweli akawaita watu wa Israeli kuja kwa Bwana huko Mispa,
18 Et il dit aux fils d'Israël: Voici ce qu'a dit le Seigneur Dieu d'Israël: J'ai fait sortir d'Égypte les fils d'Israël, je vous ai tirés des mains du Pharaon, roi d'Égypte, et de tous les rois qui vous avaient opprimés.
naye akawaambia, “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Niliwatoa Israeli kutoka Misri, nami niliwaokoa toka nguvu za Misri na falme zote zilizowaonea.’
19 Aujourd'hui, vous avez rejeté le Dieu qui seul est votre Sauveur en tous vos maux, en toutes vos afflictions, et vous avez dit: Nous le voulons, donne- nous un roi. Maintenant donc, présentez-vous devant le Seigneur, par tribus, par familles.
Lakini sasa mmemkataa Mungu wenu, ambaye anawaokoa toka katika maafa yenu yote na taabu zenu zote. Nanyi mmesema, ‘Hapana, tuteulie mfalme atutawale.’ Sasa basi, jihudhurisheni wenyewe mbele za Bwana kwa kabila zenu na kwa koo zenu.”
20 Samuel fit alors avancer toutes les tribus d'Israël, et le sort désigna la tribu de Benjamin.
Samweli alipoyasogeza makabila yote ya Israeli, kabila la Benyamini likachaguliwa.
21 Il fit avancer la tribu de Benjamin, par familles, et le sort désigna la famille de Mattari. On fit avancer la famille de Mattari homme par homme, et le sort désigna Saül, fils de Cis. Samuel le demanda, mais on ne le trouva point.
Kisha akalisogeza mbele kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo, nao ukoo wa Matri ukachaguliwa. Mwishoni Sauli mwana wa Kishi akachaguliwa. Lakini walipomtafuta, hakuonekana.
22 Et Samuel interrogea encore le Seigneur, disant: L'homme est-il venu ici? Et le Seigneur lui répondit: Il est caché parmi les bagages.
Wakazidi kuuliza kwa Bwana, “Je, huyo mtu amekwisha kufika hapa?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, amejificha katikati ya mizigo.”
23 Il y courut, il l'y trouva, et il l'amena au milieu du peuple. Or, il dépassait le peuple entier de toute la tête.
Wakakimbia na kumleta kutoka huko, naye aliposimama katikati ya watu, alikuwa mrefu kuliko watu wengine wote.
24 Samuel dit alors à tout le peuple: Avez-vous vu celui que le Seigneur s'est choisi? a-t-il parmi vous son pareil? Tout le peuple fut de son avis, et ils crièrent: Vive le roi!
Samweli akawaambia watu wote, “Je, mnamwona mtu ambaye Bwana amemchagua? Hayupo aliye kama yeye miongoni mwa watu wote.” Ndipo watu wakapiga kelele, wakasema, “Mfalme na aishi maisha marefu.”
25 Samuel apprit ensuite au peuple les justes droits du roi; il les transcrivit en un livre qu'il déposa devant le Seigneur. Enfin, Samuel congédia tout le peuple, et chacun retourna en sa demeure.
Samweli akawaeleza watu madaraka ya ufalme. Akayaandika kwenye kitabu na kuweka mbele za Bwana. Kisha Samweli akawaruhusu watu, kila mmoja aende nyumbani kwake.
26 Saül rentra dans sa maison à Gabaa; et les hommes vaillants, dont Dieu avait touché le cœur pour qu'ils s'unissent à Saül, l'accompagnèrent.
Sauli pia akaenda nyumbani kwake huko Gibea, akisindikizwa na watu hodari ambao Mungu alikuwa amegusa mioyo yao.
27 Mais les fils de pestilence dirent: Est-ce celui-là qui nous sauvera? Et ils le méprisèrent, et ils ne lui portèrent point de présents.
Lakini baadhi ya watu wakorofi walisema, “Huyu mtu atawezaje kutuokoa?” Wakamdharau na wala hawakumletea zawadi. Lakini Sauli akanyamaza kimya.

< 1 Samuel 10 >