< 1 Rois 5 >

1 Et Hiram, roi de Tyr, envoya ses serviteurs, sachant que Salomon avait été oint à la place de David, son père; car Hiram avait aimé David tous les jours de sa vie.
Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
2 Salomon envoya aussi des messagers à Hiram, disant:
Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
3 Tu sais que David, mon père, n'a pu bâtir un temple au nom du Seigneur mon Dieu, à cause des guerres qui ont éclaté tout alentour, jusqu'à ce que le Seigneur eût abattu ses ennemis sous la plante de ses pieds.
“Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
4 Maintenant, le Seigneur mon Dieu m'a donné la paix tout alentour; il n'est point de complot contre moi ni de mauvais desseins.
Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
5 Et voilà que j'ai résolu de bâtir un temple au nom du Seigneur mon Dieu, comme le Seigneur Dieu l'a dit à David mon père: C'est ton fils, que je mettrai sur le trône à ta place, qui bâtira un temple à mon nom.
Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
6 Donne donc tes ordres, et que l'on coupe des arbres du Liban; voici mes serviteurs pour aider les tiens, et je te paierai le salaire de tes services comme tu le demanderas; car tu sais que parmi nous personne n'est aussi habile que les Sidoniens à travailler le bois.
“Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
7 Or, Hiram fut grandement réjoui d'entendre ces paroles, et il dit: Béni soit aujourd'hui le Seigneur, qui a donné à David un fils aussi sage pour gouverner ce peuple nombreux.
Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
8 Puis, il envoya dire à Salomon: J'ai ouï toutes les choses au sujet desquelles tu as envoyé près de moi; je ferai tout ce que tu veux; cèdres et sapins,
Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
9 Mes serviteurs transporteront tout du Liban à la mer; on en formera des radeaux jusqu'au lieu que tu m'indiqueras; là, je les ferai délier, et tu les enlèveras, et tu feras tout ce que je désire en donnant des vivres à ma maison.
Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
10 Hiram donna donc à Salomon des cèdres, des sapins et tout ce qu'il voulut.
Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
11 Et Salomon donna à Hiram vingt mille mesures de froment pour alimenter sa maison, et vingt mille mesures d'huile battue; voilà ce que Salomon donna par an à Hiram.
naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
12 Or, le Seigneur avait donné à Salomon la sagesse comme il le lui avait dit. Et la paix régnait entre Hiram et Salomon, qui contractèrent entre eux une alliance.
Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
13 Le roi imposa une corvée à tout Israël, et il requit pour ce service trente mille hommes.
Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
14 Il les fit partir pour le Liban, dix mille par dix mille qui se relevaient mois par mois; ils passaient un mois au Liban et deux mois chez eux. Adoniram était à leur tête.
Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
15 Et Salomon employait soixante-dix mille hommes à transporter les matériaux, et quatre-vingt mille à tailler des pierres dans la montagne,
Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
16 Sans compter les conducteurs des travaux; il y en avait trois mille six cents habiles à ces sortes d'œuvres.
pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
17 Et l'on mit trois ans à préparer les pierres et les bois.
Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
18 Et l'on mit trois ans à préparer les pierres et les bois.
Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.

< 1 Rois 5 >