< 1 Rois 3 >

1 Mais le peuple sacrifiait encore sur les hauts lieux, parce que le temple du Seigneur n'était pas encore bâti.
Solomoni akafanya urafiki na Mfalme Farao wa Misri na kumwoa binti yake. Akamleta huyo binti katika Mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga jumba lake la kifalme na Hekalu la Bwana, pamoja na ukuta kuzunguka Yerusalemu.
2 Mais le peuple sacrifiait encore sur les hauts lieux, parce que le temple du Seigneur n'était pas encore bâti.
Hata hivyo, watu bado walikuwa wakitoa dhabihu huko kwenye vilima, kwa sababu Hekalu lilikuwa bado halijajengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.
3 Or, Salomon aimait le Seigneur, et marchait en la voie des commandements du roi David son père; seulement il sacrifiait et encensait sur, les hauts lieux.
Solomoni akaonyesha upendo wake kwa Bwana kwa kuenenda sawasawa na amri za Daudi baba yake, ila yeye alitoa dhabihu na kufukiza uvumba huko mahali pa juu.
4 Et il partit pour Gabaon, afin d'y offrir un sacrifice; car c'était le lieu le plus élevé et le plus célèbre. Salomon offrit en holocauste mille victimes sur l'autel de Gabaon.
Mfalme akaenda Gibeoni kutoa dhabihu, kwa maana ndipo palipokuwa mahali pa juu pa kuabudia, naye Solomoni akatoa sadaka elfu moja za kuteketezwa juu ya hayo madhabahu.
5 Et la nuit venue, le Seigneur apparut à Salomon pendant son sommeil, et le Seigneur lui dit: Demande-moi quelque chose pour toi.
Bwana akamtokea Solomoni huko Gibeoni wakati wa usiku katika ndoto, naye Mungu akasema, “Omba lolote utakalo nikupe.”
6 Et Salomon répondit: Vous avez usé d'une grande miséricorde envers mon père David votre serviteur, parce qu'il avait marché devant vous dans les voies de la vérité et de la justice, et dans la droiture du cœur. Et gardant envers lui cette grande miséricorde, vous avez fait monter son fils sur le trône où il est aujourd'hui.
Solomoni akajibu, “Umemfanyia mtumishi wako, baba yangu Daudi, fadhili nyingi, kwa kuwa alikuwa mwaminifu kwako na mwenye haki, tena mnyofu wa moyo. Nawe umemzidishia fadhili hii kuu kwani umempa mwana wa kuketi kwenye kiti chake cha ufalme, kama ilivyo leo.
7 Vous venez, Seigneur mon Dieu, de mettre à la place de David mon père, moi votre serviteur, moi qui suis encore un jeune adolescent, et qui ne sais encore ni entrer, ni sortir.
“Sasa, Ee Bwana Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako mfalme badala ya baba yangu Daudi. Lakini mimi ni mtoto mdogo tu, wala sijui jinsi ya kutekeleza wajibu wangu.
8 Et votre serviteur se trouve au milieu de votre peuple, du peuple nombreux que vous vous êtes choisi, d'un peuple innombrable.
Mtumishi wako yuko hapa miongoni mwa watu uliowachagua: taifa kubwa, watu wengi wasioweza kuhesabika wala kutoa idadi yao.
9 Donnez donc à votre serviteur un cœur qui écoute, qui juge votre peuple selon la justice, et qui sache discerner le bien et le mal; car qui pourrait juger votre peuple, ce peuple puissant?
Hivyo mpe mtumishi wako moyo wa ufahamu ili kutawala watu wako na kupambanua kati ya mema na mabaya. Kwa maana, ni nani awezaye kutawala watu wako hawa walio wengi hivi?”
10 Et il fut agréable au Seigneur que Salomon eût fait cette demande.
Bwana akapendezwa kwamba Solomoni ameliomba jambo hili.
11 Et le Seigneur lui dit: Parce que tu m'as demandé cette chose, et que tu ne m'as pas demandé pour toi de longs jours, que tu ne m'as pas demandé des richesses, que tu ne m'as pas demandé la mort de tes ennemis, mais que tu m'as demandé pour toi la sagesse, afin de discerner ce qui est juste,
Basi Mungu akamwambia, “Kwa kuwa umeomba neno hili na hukuomba maisha marefu au upate utajiri kwa nafsi yako, wala adui zako wafe, bali umeomba ufahamu katika kutoa haki,
12 J'ai déjà fait selon ta parole: voilà que je t'ai doué d'un cœur prudent et sage; il n'a existé avant toi personne qui te ressemble, et après toi, on ne verra jamais ton semblable.
nitafanya lile uliloomba. Nitakupa moyo wa hekima na wa ufahamu, kiasi kwamba hajakuwepo mtu mwingine kama wewe, wala kamwe hatakuwepo baada yako.
13 Je t'ai donné, en outre, ce que tu n'as pas demandé, la richesse et la gloire, au point que nul des rois ne t'a jamais égalé.
Zaidi ya hayo, nitakupa yale ambayo hukuomba, yaani utajiri na heshima, ili kwamba maisha yako yote hapatakuwa na mtu kama wewe miongoni mwa wafalme.
14 Si tu marches en ma voie comme a marché David ton père, en gardant mes commandements et mes ordonnances, je t'accorderai, de plus, de longs jours.
Nawe kama ukienenda katika njia zangu na kutii sheria na amri zangu kama baba yako Daudi alivyofanya, nitakupa maisha marefu.”
15 Et Salomon s'éveilla, et il n'oublia point ce songe; il se leva, et rentra dans Jérusalem; il se plaça debout devant l'autel et devant l'arche du Seigneur en Sion; puis, il sacrifia des holocaustes et des hosties pacifiques; enfin il fit préparer un grand festin pour lui-même et pour tous ses serviteurs.
Ndipo Solomoni akaamka, akatambua kuwa ilikuwa ndoto. Akarudi Yerusalemu, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Bwana, naye akatoa dhabihu za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha akawafanyia watumishi wake wote karamu.
16 Alors, deux femmes prostituées apparurent en présence du roi, et elles se tinrent debout devant lui.
Basi wanawake wawili makahaba walikuja kwa mfalme na kusimama mbele yake.
17 L'une des deux femmes dit: Je te prie, Seigneur: Moi et cette femme nous habitons la même maison, et dans cette maison nous avons enfanté.
Mmojawapo akasema, “Bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunaishi kwenye nyumba moja. Nilikuwa nimezaa alipokuwa pamoja nami.
18 Trois jours après que je fus accouchée, cette femme est accouchée aussi; nous étions ensemble, et il n'y avait personne que nous deux dans la maison.
Siku ya tatu baada ya mtoto wangu kuzaliwa, mwanamke huyu pia naye akazaa mtoto. Tulikuwa peke yetu, hapakuwa na mtu mwingine yeyote katika nyumba isipokuwa sisi wawili.
19 Or, l'enfant de cette femme est mort la nuit dernière, parce qu'elle s'était couchée sur lui.
“Wakati wa usiku mwana wa huyu mwanamke akafa kwa sababu alimlalia.
20 Et elle s'est levée au milieu de la nuit; et elle a pris mon enfant dans mes bras, et elle l'a mis en son sein; et son fils mort elle l'a placé en mon sein.
Hivyo akaondoka katikati ya usiku na kumchukua mwanangu kutoka ubavuni pangu wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa nimelala. Akamweka kifuani mwake na kumweka mwanawe aliyekufa kifuani mwangu.
21 Je me suis réveillée de grand matin pour allaiter mon fils, et l'enfant était mort; or, comme je le regardais bien attentivement aux premières lueurs du jour, je vis que ce n'était pas le fils que j'avais enfanté.
Asubuhi yake, nikaamka ili kumnyonyesha mwanangu, naye alikuwa amekufa! Lakini nilipomwangalia sana katika nuru ya asubuhi, niliona kuwa hakuwa yule mwana niliyekuwa nimemzaa.”
22 L'autre femme s'écria: Du tout, mais mon fils est vivant, c'est ton fils qui est mort. Et elles parlaient ainsi devant le roi.
Huyo mwanamke mwingine akasema, “Hapana! Mwana aliye hai ndiye wangu, aliyekufa ni wako.” Lakini yule wa kwanza akasisitiza, “Hapana! Mwana aliyekufa ni wako, aliye hai ni wangu.” Hivi ndivyo walivyobishana mbele ya mfalme.
23 Et le roi dit à l'une: Tu dis: Celui-ci, le vivant, est mon fils, et le fils de cette femme est mort; puis il dit à l'autre: Tu dis: Du tout, mais mon fils est vivant, et c'est ton fils qui est mort.
Mfalme akasema, “Huyu anasema, ‘Mwanangu ndiye aliye hai, na aliyekufa ndiye mwanao,’ maadamu yule anasema, ‘Hapana! Aliyekufa ni wako, na aliye hai ni wangu.’”
24 Et le roi ajouta: Que l'on prenne un glaive. Et l'on apporta un glaive devant le roi.
Kisha mfalme akasema, “Nileteeni upanga.” Basi wakamletea mfalme upanga.
25 Et le roi dit: Coupez en deux cet enfant vivant qui est à la mamelle, donnez-en la moitié à celle-ci, la moitié à celle-là.
Ndipo mfalme akatoa amri: “Mkate mtoto aliye hai vipande viwili; mpe huyu nusu na mwingine nusu.”
26 Et la femme à qui était l'enfant vivant se hâta de parler au roi, car ses entrailles étaient troublées à cause de son fils, et elle dit: Je te prie, Seigneur, qu'on lui donne l'enfant, qu'on ne le fasse pas mourir. Mais l'autre dit: Qu'il ne soit ni pour elle, ni pour moi, partagez-le.
Mwanamke ambaye mwanawe alikuwa hai akajawa na huruma kwa ajili ya mwanawe na kumwambia mfalme, “Tafadhali, bwana wangu, mpe yeye mtoto aliye hai! Usimuue!” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Mkate vipande viwili. Asiwe wangu au wake!”
27 Et le roi prit la parole, et il dit: Donnez l'enfant à celle qui a dit: Donnez-lui l'enfant, ne le faites pas mourir; celle-là est sa mère.
Kisha mfalme akatoa uamuzi wake: “Mpeni mama wa kwanza mtoto aliye hai. Msimuue; ndiye mama yake.”
28 Et tout Israël citât le jugement qu'avait rendu le roi, et ils eurent crainte du roi, car ils virent que la sagesse de Dieu était en lui quand il rendait la justice.
Wakati Israeli yote iliposikia hukumu aliyotoa mfalme, wakamwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa alikuwa na hekima kutoka kwa Mungu kwa kutoa haki.

< 1 Rois 3 >