< 1 Rois 18 >

1 Après bien des jours, la parole du Seigneur vint à Elie pendant la troisième année, disant: Pars, présente-toi devant Achab, et je donnerai de la pluie à la terre.
Baada ya muda mrefu, katika mwaka wa tatu, neno la Bwana likamjia Eliya kusema, “Nenda ukajionyeshe kwa Ahabu na mimi nitanyesha mvua juu ya nchi.”
2 Et Elie partit pour se présenter devant Achab. En ce temps-là, il y avait à Samarie une famine très grande.
Kwa hiyo Eliya akaenda kujionyesha kwa Ahabu. Wakati huu njaa ilikuwa kali sana katika Samaria,
3 Et Achab appela son économe Abdias; or, Abdias craignait beaucoup le Seigneur.
naye Ahabu alikuwa amemwita Obadia ambaye alikuwa msimamizi wa jumba lake la kifalme. (Obadia alimcha Bwana sana.
4 Quand Jézabel frappait les prophètes du Seigneur, Abdias avait pris cent hommes qui prophétisaient; il les avait cachés cinquante par cinquante dans des cavernes où il les avait nourris de pain et d'eau.
Wakati Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa Bwana, Obadia alikuwa amewachukua manabii mia moja na kuwaficha katika mapango mawili, hamsini kwenye kila moja na akawa akiwapa chakula na maji.)
5 Et Achab dit à Abdias: Viens, parcourons la contrée, visitons les torrents et les fontaines; peut-être trouverons-nous de l'herbe; nous y ferons paître les chevaux et les mules, et ils ne périront pas dans les étables.
Ahabu alikuwa amemwambia Obadia, “Nenda katika nchi yote kwenye vijito vyote na mabonde. Huenda tunaweza kupata majani ya kuwalisha farasi na nyumbu wapate kuishi ili tusilazimike kuwaua hata mmoja wa wanyama wetu.”
6 Et ils se partagèrent les territoires à visiter; Achab prit une route; Abdias, de son côté, en prit une autre.
Kwa hiyo wakagawanya nchi waliyokusudia kutafuta majani, Ahabu akaenda upande mmoja na Obadia upande mwingine.
7 Comme Abdias s'en allait seul sur un chemin, Elie arriva seul à sa rencontre. Abdias, pressant le pas, tomba la face contre terre, et il dit: Est-ce bien toi, Elie, mon maître?
Wakati Obadia alipokuwa akitembea njiani, Eliya akakutana naye. Obadia akamtambua, akamsujudia hadi nchi na kusema, “Je, hivi kweli ni wewe, bwana wangu Eliya?”
8 Elie répondit: C'est moi; pars, et dis à ton maître: Voici Elie.
Eliya akamjibu, “Ndiyo, nenda ukamwambie bwana wako Ahabu, ‘Eliya yuko hapa.’”
9 Abdias reprit: Quel péché ai-je fait pour que tu livres ton serviteur aux mains d'Achab, afin qu'il me fasse mourir.
Obadia akamuuliza, “Ni kosa gani nimefanya, hata ukaamua kumkabidhi mtumishi wako mkononi mwa Ahabu ili aniue?
10 Vive le Seigneur ton Dieu! il n'est ni peuple ni royaume où mon maître n'ait envoyé pour te prendre, et quand on disait: Elie n'est pas ici, il portait la flamme en ce royaume et en ses campagnes, parce qu'il ne t'avait point trouvé.
Hakika kama Bwana Mungu wako aishivyo, hakuna taifa hata moja au ufalme ambapo bwana wangu hajamtuma mtu kukutafuta. Kila wakati taifa au ufalme walipodai kwamba haupo huko, aliwafanya waape kwamba hawakuweza kukupata.
11 Et maintenant, tu veux que je parte et que je dise à ton maître: Voici Elie!
Lakini sasa unaniambia niende kwa bwana wangu na kusema, ‘Eliya yuko hapa.’
12 Voici ce qui adviendra: Lorsque je me serai éloigné de toi, l'Esprit du Seigneur te ravira en une terre je ne sais laquelle; et je me présenterai devant Achab et je t'annoncerai; mais lui, ne te trouvant pas, me fera mourir; or, ton serviteur, depuis son enfance, a la crainte de Dieu.
Sijui ni wapi Roho wa Bwana ataamua kukupeleka wakati nitakapokuacha. Kama nikienda kumwambia Ahabu na asikupate, ataniua. Hata hivyo mimi mtumishi wako nimemwabudu Bwana tangu ujana wangu.
13 Ne sais-tu pas, ô mon maître, que quand Jézabel tuait les prophètes du Seigneur, j'ai caché cent prophètes du Seigneur, cinquante par cinquante, en des cavernes, et que je les ai nourris de pain et d'eau?
Je, hukusikia, bwana wangu, nilifanya nini wakati Yezebeli alipokuwa akiua manabii wa Bwana? Niliwaficha manabii wa Bwana mia moja katika mapango mawili, hamsini katika kila moja, nami nikawapatia chakula na maji.
14 Et maintenant, tu veux que je parte et que je dise à mon maître: Voici Elie! Mais il me tuera.
Nawe sasa unaniambia niende kwa bwana wangu na kumwambia, ‘Eliya yuko hapa.’ Yeye ataniua!”
15 Elie reprit: Vive le Seigneur Dieu des armées, devant qui je suis! aujourd'hui même Achab me verra.
Eliya akasema, “Kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo, yeye ninayemtumikia, hakika nitajionyesha kwa Ahabu leo.”
16 Abdias alla donc à la rencontre d'Achab; il lui annonça le prophète, et Achab accourut au-devant d'Elie.
Basi Obadia akaenda kukutana na Ahabu na kumwambia, naye Ahabu akaenda kukutana na Eliya.
17 Aussitôt qu'il aperçut Elie, il s'écria: Es-tu donc celui qui pervertit Israël?
Ahabu alipomwona Eliya, akamwambia, “Je, ni wewe, mtaabishaji wa Israeli?”
18 Et le prophète répondit: Ce n'est point moi qui pervertis Israël, mais toi-même et la maison de ton père; car, vous abandonnez le Seigneur votre Dieu pour suivre Baal.
Eliya akamjibu, “Mimi sijaitaabisha Israeli. Lakini wewe na jamaa ya baba yako ndio mnaofanya hivyo. Mmeziacha amri za Bwana na mkafuata Mabaali.
19 Donne à ce moment tes ordres: rassemble devant moi, sur le mont Carmel, tout le peuple des dix tribus avec les quatre cent cinquante prophètes de l'opprobre, et les quatre cents prophètes des bois sacrés, qui mangent à la table de Jézabel.
Sasa waite watu kutoka Israeli yote tukutane nao juu ya Mlima Karmeli. Nawe uwalete hao manabii wa Baali mia nne na hamsini na hao manabii mia nne wa Ashera, walao chakula mezani mwa Yezebeli.”
20 Et Achab envoya par tout Israël; et il rassembla sur le mont Carmel tous les prophètes.
Ndipo Ahabu akatuma ujumbe katika Israeli yote na kuwakusanya manabii hao juu ya mlima Karmeli.
21 Devant eux tous, il mena Elie, et celui-ci leur dit: Jusqu'à quand boiterez-vous des deux jambes? Si le Seigneur est Dieu, suivez le Seigneur; si Baal est Dieu, suivez Baal. Et le peuple ne souffla mot.
Eliya akasimama mbele ya watu na kusema, “Mtasitasita katika mawazo mawili hadi lini? Ikiwa Bwana ndiye Mungu, mfuateni yeye; lakini ikiwa Baali ni Mungu, basi mfuateni yeye.” Lakini watu hawakusema kitu.
22 Elie dit ensuite au peuple: Il n'y a plus que moi de prophète du Seigneur; les prophètes de Baal sont quatre cent cinquante, et les prophètes des bois sacrés quatre cents.
Kisha Eliya akawaambia, “Ni mimi peke yangu nabii wa Bwana aliyebaki, lakini Baali ana manabii mia nne na hamsini.
23 Que l'on nous donne deux bœufs; qu'ils en choisissent un pour eux, qu'ils le séparent par membres, qu'ils le posent sur le bûcher sans qu'on y mette le feu; moi cependant j'apprêterai de même l'autre bœuf, et je n'allumerai point le bûcher.
Leteni mafahali wawili. Wao na wajichagulie mmoja, wamkate vipande vipande na waweke juu ya kuni lakini wasiiwashie moto. Nitamwandaa huyo fahali mwingine na kumweka juu ya kuni lakini sitawasha moto.
24 Criez alors au nom de vos dieux, et moi j'invoquerai le nom du Seigneur mon Dieu; le Dieu qui nous exaucera en envoyant de la flamme, celui-là est Dieu. A ces mots tout le peuple répondit, et il dit: Tu as bien parlé.
Kisha mliitie jina la mungu wenu, nami nitaliitia jina la Bwana Mungu yule ambaye atajibu kwa moto, huyo ndiye Mungu.” Kisha watu wote wakasema, “Hilo unalosema ni jema.”
25 Aussitôt, Elie dit aux prophètes de l'opprobre: Choisissez pour vous l'un des bœufs, et apprêtez-le les premiers, car vous êtes nombreux; invoquez le nom de vos dieux, et n'allumez pas le bûcher.
Eliya akawaambia manabii wa Baali, “Chagueni mmoja kati ya hawa mafahali na mwe wa kwanza kumwandaa, kwa kuwa ninyi mko wengi sana. Liitieni jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.”
26 Ils prirent le bœuf, ils l'apprêtèrent, ils invoquèrent le nom de Baal depuis l'aurore jusqu'au milieu du jour, et ils dirent: Exaucez-nous, ô Baal, exaucez-nous. Mais il n'y avait point de voix pour leur répondre, point d'oreilles pour les ouïr, et ils passaient et repassaient devant l'autel qu'ils avaient élevé.
Kwa hiyo wakamchukua yule fahali waliyepewa, nao wakamwandaa. Kisha wakaliitia jina la Baali kutoka asubuhi hadi adhuhuri, wakapiga kelele, “Ee Baali, utujibu!” Lakini hapakuwa na jibu; hakuna aliyejibu. Nao wakacheza kuizunguka madhabahu waliyoijenga.
27 Le milieu du jour vint, et le Thesbite Elie les railla, et il dit; Invoquez-le à grands cris, puisque vous le dites dieu; il est peut-être à méditer, il est peut-être en affaire, ou peut-être il dort, et il se réveillera.
Wakati wa adhuhuri, Eliya akaanza kuwadhihaki, akisema, “Pigeni kelele zaidi! Hakika yeye ni mungu! Labda amezama katika mawazo mazito, au ana shughuli nyingi, au amesafiri. Labda amelala usingizi mzito, naye ni lazima aamshwe.”
28 Ils firent donc leurs invocations à grands cris; puis, selon leurs rites, ils se firent des entailles avec des poignards et des lancettes, de telle sorte que le sang ruissela sur eux.
Kwa hiyo wakapiga kelele zaidi na kama ilivyokuwa desturi yao wakajichanja wenyewe kwa visu na vyembe, mpaka damu ikachuruzika.
29 Et ils prophétisèrent jusqu'à ce que le soleil commençât à décliner. Le moment étant venu où l'on place sur l'autel les victimes, Elie le Thesbite dit aux prophètes des abominations: Retirez-vous maintenant, et je ferai mon holocauste. Et ils se retirèrent, et ils partirent.
Adhuhuri ikapita, nao wakaendelea na utabiri wao wa kiwazimu mpaka wakati wa dhabihu ya jioni. Lakini hapakuwa na jibu, hakuna aliyejibu, hakuna aliyeangalia.
30 Alors, Elie dit au peuple: Approchez-vote de moi, et tout le peuple s'approcha de lui.
Kisha Eliya akawaambia watu wote, “Sogeeni karibu nami.” Watu wote wakamkaribia, naye akakarabati madhabahu ya Bwana, ambayo ilikuwa imevunjwa.
31 Et Elie prit douze pierres selon le nombre des tribus issues d'Israël à qui le Seigneur avait dit: Israël sera ton nom.
Eliya akachukua mawe kumi na mawili, moja kwa ajili ya kila kabila la wana wa Yakobo, ambaye neno la Bwana lilimjia, likisema, “Jina lako litakuwa Israeli.”
32 Et il mit en œuvre ces pierres au nom du Seigneur, et il répara l'autel qui avait été renversé; autour de l'autel il creusa une rigole, qui eût contenu deux mesures de semence.
Kwa mawe hayo, akajenga madhabahu katika jina la Bwana, na akachimba handaki kuizunguka, ukubwa wa kutosha vipimo viwili vya mbegu.
33 Et il empila du bois fendu sur l'autel qu'il avait construit, sépara par membres l'holocauste, le posa sur les éclats de bois, et l'empila sur l'autel.
Akapanga kuni, akamkata yule fahali vipande vipande na kuvipanga juu ya kuni. Kisha akawaambia, “Jazeni mapipa manne maji na kuyamwaga juu ya sadaka ya kuteketezwa na juu ya kuni.”
34 Puis, il dit: Prenez-moi quatre cruches d'eau que vous répandrez sur l'holocauste et sur le bois. Ainsi firent-ils, et il dit: Redoublez; ils redoublèrent, et il dit: Recommencez une troisième fois, et ils recommencèrent.
Akawaambia, “Fanyeni hivyo tena.” Nao wakafanya hivyo tena. Akaagiza, “Fanyeni kwa mara ya tatu.” Nao wakafanya hivyo kwa mara ya tatu.
35 Et l'eau coula autour de l'autel, et la rigole en fut remplie.
Maji yakatiririka kuizunguka madhabahu na hata kujaza lile handaki.
36 Et Elie cria au ciel, disant: Seigneur Dieu d'Abraham, d'Isaac et d'Israël, exaucez-moi, Seigneur, exaucez-moi aujourd'hui en m'envoyant de la flamme; que tout le peuple reconnaisse que vous êtes le Seigneur Dieu d'Israël, que je suis votre serviteur, et que je n'ai rien fait, sinon par vous.
Wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, nabii Eliya akasogea mbele na kuomba, akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Abrahamu, na Isaki na Israeli, ijulikane leo kwamba wewe ndiye Mungu katika Israeli na ya kwamba mimi ni mtumishi wako na nimefanya mambo haya yote kwa neno lako.
37 Exaucez-moi, Seigneur, exaucez-moi; que le peuple reconnaisse que vous êtes le Seigneur Dieu, et vous convertirez le cœur de ce peuple.
Unijibu mimi, Ee Bwana, nijibu mimi, ili watu hawa wajue kwamba wewe, Ee Bwana, ndiwe Mungu, na kwamba unaigeuza mioyo yao ikurudie tena.”
38 Et une flamme descendit tu ciel, envoyée par le Seigneur; elle dévora l'holocauste, le bûcher, l'eau de la rigole; elle effleura les pierres de l'autel et la terre.
Kisha moto wa Bwana ukashuka na kuiteketeza ile dhabihu, zile kuni, yale mawe, ule udongo, na pia kuramba yale maji yaliyokuwa ndani ya handaki.
39 Et le peuple tomba la face contre terre, et il dit: En vérité, le Seigneur Dieu est le seul Dieu.
Wakati watu wote walipoona hili, wakaanguka kifudifudi na kulia, “Bwana: yeye ndiye Mungu! Bwana: yeye ndiye Mungu!”
40 Elie dit ensuite au peuple: Saisissez les prophètes de Baal, que pas un seul ne soit épargné. Ils les saisirent, et Elie les traîna au torrent de Cisson, et là, il les égorgea.
Kisha Eliya akawaamuru, “Wakamateni hao manabii wa Baali. Msimwache hata mmoja atoroke!” Wakawakamata, naye Eliya akawaleta mpaka Bonde la Kishoni na kuwachinja huko.
41 Elie dit ensuite à Achab: Pars, mange et bois; car il y a un bruit de pluie qui arrive.
Eliya akamwambia Ahabu, “Nenda, ukale na kunywa, kwa kuwa kuna sauti ya mvua kubwa.”
42 Et Achab partit pour manger et boire; et le prophète monta sur le Carmel; là, il se pencha vers la terre, la tête entre les genoux.
Hivyo Ahabu akaondoka ili kula na kunywa. Lakini Eliya akapanda kileleni mwa Karmeli, akasujudu na akaweka kichwa chake katikati ya magoti yake.
43 Puis, il dit à son serviteur: Va, et regarde du côté de la mer. Le serviteur regarda, et il dit: il n'y a rien. Mais son maître lui dit: Retournes-y sept fois.
Akamwambia mtumishi wake, “Nenda ukatazame kuelekea bahari.” Akaenda na kutazama. Akasema, “Hakuna kitu chochote huko.” Mara saba Eliya akasema, “Nenda tena.”
44 Et le serviteur y retourna sept fois; à la septième fois il vit un petit nuage semblable au pied d'un homme, et ce nuage amenait de l'eau; le maître alors dit au serviteur: Va trouver Achab, et dis-lui: Attelle ton char et mets-toi en route, de peur que la pluie ne te surprenne.
Mara ya saba, mtumishi akaleta taarifa, “Wingu dogo kama mkono wa mwanadamu linainuka kutoka baharini.” Hivyo Eliya akasema, “Nenda ukamwambie Ahabu, ‘Tandika gari lako na ushuke kabla mvua haijakuzuia.’”
45 Bientôt çà et là le ciel s'obscurcit de nuées, le vent souffla, et il tomba une grande pluie. Et Achab, en pleurant, s'en alla à Jezraël.
Wakati ule ule anga likawa jeusi kwa mawingu, upepo ukainuka na mvua kubwa ikanyesha, naye Ahabu akaenda zake Yezreeli.
46 Et la main du Seigneur s'étendit sur Elie, et il serra sur ses reins sa ceinture, et il courut devant Achab jusqu'à Jezraël.
Nguvu za Bwana zikamjia Eliya, naye akajikaza viuno, akakimbia mbele ya Ahabu njia yote hadi maingilio ya Yezreeli.

< 1 Rois 18 >