< 1 Rois 11 >

1 Et le roi Salomon aimait les femmes. Il avait sept cents femmes princesses et trois cents concubines. Il avait épousé des femmes étrangères: la fille du Pharaon, puis des Moabites, des Ammonites, des Syriennes, des Iduméennes, des Hettéennes et des Amorrhéennes,
Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
2 Des femmes de ces peuples dont le Seigneur avait dit aux fils d'Israël: «Vous n'aurez point avec eux de commerce, ni eux avec vous, de peur qu'ils ne détournent vos cœurs vers leurs idoles.» Salomon s'était attaché à elles, il les aimait.
Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
3 Et, au temps de sa vieillesse, son cœur ne fut point parfait à l'égard du Seigneur son Dieu, comme le cœur de David, son père. Car les femmes étrangères détournèrent son cœur vers leurs dieux.
Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
4 Et, au temps de sa vieillesse, son cœur ne fut point parfait à l'égard du Seigneur son Dieu, comme le cœur de David, son père. Car les femmes étrangères détournèrent son cœur vers leurs dieux.
Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
5 Alors, Salomon bâtit un haut lieu à Chamos, idole de Moab; à leur roi, idole des fils d'Ammon,
Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
6 Et à Astarté, abomination des Sidoniens.
Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
7 A toutes ses femmes étrangères, il accorda de sacrifier à leurs idoles et de les encenser.
Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
8 Et Salomon fit le mal devant le Seigneur; il ne suivit point le Seigneur, comme l'avait suivi David, son père.
Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
9 Et le Seigneur se courrouça contre Salomon, parce qu'il avait détourné son cœur du Seigneur Dieu d'Israël qui lui était apparu deux fois,
Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
10 Et lui avait expressément commandé de ne jamais suivre d'autres dieux, d'être attentif à faire tout ce qu'avait prescrit le Seigneur Dieu; en effet, son cœur n'était point parfait à l'égard du Seigneur, comme le cœur de David, son père.
Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
11 Et le Seigneur dit à Salomon: En punition de ce que tu as agi de la sorte et n'as point gardé mes commandements et mes ordonnances que je t'avais donnés, je déchirerai dans tes mains ton royaume, et j'en donnerai une part à ton serviteur.
Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
12 Seulement, à cause de David, ton père, je ne ferai point ces choses de ton vivant; je retirerai des mains de ton fils cette part du royaume.
Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
13 Car je ne le lui prendrai pas tout entier; je laisserai un sceptre à ton fils, à cause de David, mon serviteur, et à cause de Jérusalem, ville que j'ai choisie.
Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
14 Et le Seigneur avait suscité des satans contre Salomon: Ader l'Iduméen et Esron, fils d'Eliadaé de Raama, jadis serviteur d'Adadézer, roi de Suba; ils avaient rassemblé des hommes contre lui, et Ader, chef de cette troupe, avait pris Damas; il fut l'ennemi d'Israël tant que vécut Salomon, et il était de la famille des rois de l'Idumée.
Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
15 Or, ceci était advenu: Dans le temps que David exterminait Edom, et que Joab, général de son armée, était à ensevelir les morts, car ils frappaient tous les mâles dans l'Idumée,
Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
16 (Joab y passa six mois avec tout Israël, jusqu'à ce qu'ils eussent détruit tous les mâles de l'Idumée.)
Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
17 Ader s'enfuit emmenant avec lui tous les Iduméens, serviteurs de son père; il se réfugia en Égypte, alors petit enfant;
Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
18 Et des hommes de la ville de Madian s'étaient soulevés; quand Ader et les siens entrèrent dans Pharan, prirent avec eux les hommes, et allèrent chez le Pharaon, roi d'Égypte. Ader fut introduit auprès du Pharaon; le roi lui donna une demeure, et lui assigna des vivres.
Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
19 Et Ader trouva grâce devant le Pharaon, et le roi lui fit épouser la sœur de sa femme Thécémina, la sœur aînée de Thécémina.
Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
20 Cette sœur de Thécémina enfanta pour Ader un fils nommé Ganebath, que Thécémina éleva avec les fils du Pharaon; Ganebath était donc parmi les fils du Pharaon.
Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
21 Lorsque Ader apprit en Égypte que David dormait auprès de ses pères, et que Joab, général de son armée, était mort; il dit au Pharaon: Congédie-moi, et je retournerai dans mon pays.
Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
22 Et le Pharaon répondit à Ader: Que te manque-t-il parmi nous? Pourquoi demandes-tu à retourner en ton pays? Ader reprit: Je désire que tu me congédies. Et il revint en sa contrée.
Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
23 Voilà d'où venait la méchanceté d'Ader, il contristait Israël et il régnait sur Edom.
Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
24 Voilà d'où venait la méchanceté d'Ader, il contristait Israël et il régnait sur Edom.
Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
25 Voilà d'où venait la méchanceté d'Ader, il contristait Israël et il régnait sur Edom.
Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
26 Or, Jéroboam, fils de Nabat l'Ephrathéen de Sarira, fils d'une femme veuve, était serviteur de Salomon.
Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
27 Voici à quelle occasion il leva les mains contre le roi son maître. Le roi Salomon était à bâtir la citadelle, et il entourait de murs l'enceinte de la ville de David.
Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
28 Jéroboam était vaillant, et Salomon discerna que le jeune serviteur était un homme d'action, et il le nomma intendant des tributs de la maison de Joseph.
Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
29 En ce temps-là, Jéroboam sortit de Jérusalem, et il fut rencontré sur la route par Achias, le prophète silonite. Achias se détourna du chemin, et Achias était enveloppé d'un manteau neuf; ils étaient seuls tous les deux dans les champs,
Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
30 Et Achias ôta son manteau neuf et le déchira en douze parts,
naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
31 Et il dit à Jéroboam: Prends pour toi dix de ces lambeaux; car voici ce que dit le Seigneur Dieu d'Israël: Je déchirerai entre les mains de Salomon son royaume, et je te donnerai dix tribus.
Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
32 Et il lui restera deux tribus, à cause de mon serviteur David, et à cause de Jérusalem, ville que j'ai choisie parmi toutes les tribus d'Israël.
Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
33 C'est en punition de ce qu'il m'a abandonné; de ce qu'il a sacrifié à Astarté, abomination des Sidoniens, à Chamos, aux idoles de Moab et à leur roi, abomination des fils d'Ammon, et de ce qu'il n'a point marché en toutes mes voies pour faire devant moi ce qui est droit, comme l'a fait David, son père.
Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
34 Toutefois, je ne retirerai point de sa main le royaume entier; je le lui laisserai même tout le reste de sa vie, à cause de David, son père, mon élu.
“‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
35 Mais je prendrai le royaume des mains de son fils, et je te donnerai dix tribus.
Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
36 Et je laisserai à son fils deux tribus, afin qu'il y ait toujours devant moi, pour mon serviteur David, un trône en Jérusalem, dans la ville que je me suis choisie pour que mon nom y résidât.
Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
37 Pour toi, je te prendrai, et tu règneras comme le désire ton âme; tu seras roi d'Israël.
Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
38 Et, si tu observes tout ce que je t'ordonnerai, si tu marches en mes voies, si tu fais devant moi ce qui est droit, en gardant mes commandements et mes ordonnances, comme a fait David, mon serviteur, je serai avec toi, et je te bâtirai une maison sûre, de même que j'en ai bâti une pour David.
Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
39 Et Salomon chercha à faire périr Jéroboam; mais il partit, et s'enfuit auprès de Sésac, roi d'Égypte, et il y demeura jusqu'à la mort de Salomon.
Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
40 Et Salomon chercha à faire périr Jéroboam; mais il partit, et s'enfuit auprès de Sésac, roi d'Égypte, et il y demeura jusqu'à la mort de Salomon.
Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
41 Le reste de l'histoire de Salomon, tout ce qu'il a fait, toute sa sagesse, ne sont-ils pas écrits au livre de la vie de Salomon?
Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
42 Salomon régna quarante ans sur tout Israël.
Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
43 Et il s'endormit avec ses pères, et on l'ensevelit en la ville de David, et Roboam, son fils, régnait à sa place.
Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 1 Rois 11 >