< 1 Chroniques 6 >

1 Fils de Lévi: Gerson, Caath et Mérari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
2 Fils de Caath: Amram et Isaar, Hébron et Oziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
3 Enfants d'Amram: Aaron, Moïse et Marie. Fils d'Aaron: Nadab et Abiud, Eléazar et Ithamar.
Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
4 Eléazar engendra Phinéès, et Phinéès engendra Abisué.
Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
5 Abisué engendra Bocci, et Bocci engendra Ozi.
Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
6 Ozi engendra Zaraïas, et Zaraïas engendra Mariel.
Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
7 Mariel engendra Amarias, et Amarias engendra Achitob.
Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
8 Achitob engendra Sadoc, et Sadoc engendra Achimaas.
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
9 Achimaas engendra Azarias, et Azarias engendra Johanan,
Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
10 Johanan engendra Azarias; ce fut lui qui exerça le sacerdoce dans le temple que Salomon bâtit à Jérusalem.
Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
11 Azarias engendra Amarias, et Amarias engendra Achitob.
Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
12 Achitob engendra Sadoc, et Sadoc engendra Salom.
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
13 Salom engendra Helcias, et Helcias engendra Azarias.
Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
14 Azarias engendra Saraias, et Sareas engendra Josadac.
Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
15 Josadac fut enlevé, avec Juda et Jérusalem, par Nabuchodonosor.
Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
16 Fils de Lévi: Gerson, Caath et Mérari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
17 Fils de Gerson: Lobeni et Sémei.
Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
18 Fils de Caath: Amram et Isaac, Hébron et Oziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
19 Fils de Mérari: Mooli et Musi; voici les familles de Lévi, désignées par les noms de leurs pères.
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
20 A Gerson et Lobeni son fils succèdent Jeth fils de ce dernier, Zamath son fils,
Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
21 Joab son fils, Addi son fils, Zara son fils, Jethri son fils.
Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
22 De Caath descendent: Aminadab son fils, Coré son fils, Aser son fils,
Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
23 Elcana son fils, Abisaph son fils, Aser son fils,
Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
24 Thaat son fils, Uriel son fils, Saül son fils.
Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
25 D'Elcana descendent encore: Amessi et Achimoth.
Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
26 Elcana son fils, Saphi son fils, Cénaath son fils,
Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
27 Eliab son fils, Jéroboam son fils, Elcana son fils.
Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
28 Fils de Samuel: Sari, premier-né, et Ables.
Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
29 Fils de Mérari: Mooli son fils, Lobeni son fils, Sémei son fils, Oza son fils,
Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
30 Samaa son fils, Aggia son fils, Asaïas son fils.
Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
31 Et voici ceux que David institua chefs des chœurs du tabernacle, lorsqu'il eut transféré l'arche à Jérusalem.
Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
32 Et ils s'accompagnaient avec des instruments, devant le tabernacle du témoignage, jusqu'à ce que Salomon eût bâti le temple du Seigneur à Jérusalem. Et ils servaient, chacun selon la fonction qui lui était assignée.
Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
33 Voici leurs noms et ceux de leurs pères: de Caath descendait: Hëman, chantre et harpiste, fils de Johel, fils de Samuel,
Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
34 Fils d'Elcana, fils de Jéroboam, fils d'Eliel, fils de Thoü,
Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
35 Fils de Suph, fils d'Elcana, fils de Maath, fils d'Amathi,
Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
36 Fils d'Elcana, fils de Johel, fils d'Azarias, fils de Saphanie,
Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
37 Fils de Thaath, fils d'Aser, fils d'Abiasaph, fils de Coré,
Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
38 Fils d'Isaar, fils de Caath, fils de Lévi, fils d'Israël.
Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
39 Et Asaph, chantre comme lui, qui se tenait à sa droite, était fils de Barachias, fils de Samaa,
Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
40 Fils de Michel, fils de Baasie, fils de Melchias,
Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
41 Fils d'Athani, fils de Zaaraï, fils d'Adaï,
Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
42 Fils d'Etham, fils de Zamnaam, fils de Sémeï,
Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
43 Fils de Jeth, petit-fils de Gerson, fils de Lévi.
Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
44 Et de Mérari descendaient les chantres qui se tenaient à gauche, dont le chef était: Ethan, fils de Cisa, fils d'Abe, fils de Maloch,
Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
45 Fils d'Asebi,
Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
46 Fils d'Amessias, fils de Bani, fils de Semer,
Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
47 Fils de Mooli, fils de Musi, fils de Mérari, fils de Lévi.
Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
48 Et les lévites leurs frères, selon leurs familles paternelles, étaient attachés aux divers services du tabernacle de Dieu.
Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
49 Aaron, et, après lui, ses fils sacrifiaient sur l'autel des holocaustes et sur l'autel des parfums; ils remplissaient toutes les fonctions relatives au Saint des saints; et ils priaient pour Israël, conformément à ce que leur avait commandé Moïse serviteur de Dieu.
Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
50 Voici les fils d'Aaron: Eléazar son fils, Phinéès son fils, Abisué son fils,
Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
51 Bocci son fils, Ozi son fils, Saraïa son fils,
Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
52 Mariel son fils, Amarias son fils, Achitob son fils,
Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
53 Sadoc son fils, Achimais son fils.
Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
54 Voici les demeures, les bourgs et les territoires, assignés par le sort, selon leurs familles, aux fils d'Aaron, et aux fils de Caath.
Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
55 Il leur fut donné Hébron, en la terre de Juda, et sa banlieue tout alentour.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
56 Mais les champs de la ville et ses bourgs appartenaient à Caleb, fils de Jéphoné.
lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 Les villes de refuge furent aussi concédées aux fils d'Aaron, savoir: Hébron, Lobna et sa banlieue, Selna et sa banlieue, Esthamo et sa banlieue,
Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
58 Jethar et sa banlieue, Dabir et sa banlieue,
Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
59 Asan et sa banlieue, Bethsamys et sa banlieue.
Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
60 Et, dans la tribu de Benjamin, Gabée et sa banlieue, Galemath et sa banlieue, Anathoth et sa banlieue. En tout treize villes par familles.
na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
61 Et le sort assigna au reste des fils de Caath, par familles, dix villes de la demi-tribu de Manassé, en deçà du Jourdain.
Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
62 Et aux fils de Gerson, par familles, treize villes des tribus d'Issachar, d'Aser, de Nephthali et de la demi-tribu de Manassé en Hasan.
Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 Et aux fils de Mérari, par familles, douze villes des tribus de Ruben, de Gad et de Zabulon.
Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
64 Et les fils d'Israël accordèrent aux lévites ces villes et leurs banlieues.
Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
65 Le sort désigna dans les tribus de Juda, de Siméon et de Benjamin, les villes auxquelles les lévites donnèrent leurs noms,
Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
66 D'après les familles des fils de Caath. Et ils eurent aussi des villes du territoire d'Ephraïm,
Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
67 Y compris les villes de refuge: Sichem et sa banlieue, dans la montagne d'Ephraïm, Gazer et sa banlieue,
Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
68 Jecmaan et sa banlieue, Béthoron et sa banlieue.
Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
69 Et, en d'autres territoires, Aïlon et sa banlieue, Gethremmon et sa banlieue.
Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
70 Et de la demi-tribu de Manassé: Anar et sa banlieue, Jemblaan et sa banlieue, selon les familles du reste des fils de Caath.
Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
71 Les fils de Gerson, par familles, eurent dans l'autre demi-tribu de Manassé, Golan en Basan et sa banlieue, Aseroth et sa banlieue.
Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
72 Et dans la tribu d'Issachar: Cédés et sa banlieue, Deberi et sa banlieue, Dabor et sa banlieue,
Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
73 Ramoth, Aïnan et sa banlieue.
Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
74 Et dans la tribu d'Aser: Maasal et sa banlieue, Abdon et sa banlieue,
Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
75 Acac et sa banlieue, Rhoob et sa banlieue.
Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
76 Et dans la tribu de Nephthali: Cédés en Gaulée et sa banlieue, Hamoth et sa banlieue, Cariathaïm et sa banlieue.
Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
77 Et dans la tribu de Zabulon: le sort attribua au reste des fils de Mérari, Remmon et sa banlieue, Thabor et sa banlieue.
Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
78 Et dans la vallée du Jourdain à l'occident du fleuve: Jéricho, et dans la tribu de Ruben: Bosor dans le désert et sa banlieue, Jasa et sa banlieue,
Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
79 Cadmoth et sa banlieue, Maephla et sa banlieue.
Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
80 Dans la tribu de Gad: Ramoth-Galaad et sa banlieue, Maanaïm et sa banlieue,
Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
81 Esébon et sa banlieue, Jazer et sa banlieue.
Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.

< 1 Chroniques 6 >