< 1 Chroniques 6 >

1 Fils de Lévi: Gerson, Caath et Mérari.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
2 Fils de Caath: Amram et Isaar, Hébron et Oziel.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
3 Enfants d'Amram: Aaron, Moïse et Marie. Fils d'Aaron: Nadab et Abiud, Eléazar et Ithamar.
Amramu alikuwa na wana: Aroni, Mose, na Miriamu. Aroni alikuwa na wana: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
4 Eléazar engendra Phinéès, et Phinéès engendra Abisué.
Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
5 Abisué engendra Bocci, et Bocci engendra Ozi.
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi,
6 Ozi engendra Zaraïas, et Zaraïas engendra Mariel.
Uzi akamzaa Zerahia, Zerahia akamzaa Merayothi,
7 Mariel engendra Amarias, et Amarias engendra Achitob.
Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
8 Achitob engendra Sadoc, et Sadoc engendra Achimaas.
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi,
9 Achimaas engendra Azarias, et Azarias engendra Johanan,
Ahimaasi akamzaa Azaria, Azaria akamzaa Yohanani,
10 Johanan engendra Azarias; ce fut lui qui exerça le sacerdoce dans le temple que Salomon bâtit à Jérusalem.
Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),
11 Azarias engendra Amarias, et Amarias engendra Achitob.
Azaria akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
12 Achitob engendra Sadoc, et Sadoc engendra Salom.
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Shalumu,
13 Salom engendra Helcias, et Helcias engendra Azarias.
Shalumu akamzaa Hilkia, Hilkia akamzaa Azaria,
14 Azarias engendra Saraias, et Sareas engendra Josadac.
Azaria akamzaa Seraya, Seraya akamzaa Yehosadaki.
15 Josadac fut enlevé, avec Juda et Jérusalem, par Nabuchodonosor.
Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.
16 Fils de Lévi: Gerson, Caath et Mérari.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
17 Fils de Gerson: Lobeni et Sémei.
Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni: Libni na Shimei.
18 Fils de Caath: Amram et Isaac, Hébron et Oziel.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
19 Fils de Mérari: Mooli et Musi; voici les familles de Lévi, désignées par les noms de leurs pères.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Zifuatazo ni koo za Walawi zilizoorodheshwa kufuatana na baba zao:
20 A Gerson et Lobeni son fils succèdent Jeth fils de ce dernier, Zamath son fils,
Wazao wa Gershoni: Gershoni akamzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,
21 Joab son fils, Addi son fils, Zara son fils, Jethri son fils.
Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.
22 De Caath descendent: Aminadab son fils, Coré son fils, Aser son fils,
Wazao wa Kohathi: Kohathi akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,
23 Elcana son fils, Abisaph son fils, Aser son fils,
Asiri akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,
24 Thaat son fils, Uriel son fils, Saül son fils.
Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Uzia, Uzia akamzaa Shauli.
25 D'Elcana descendent encore: Amessi et Achimoth.
Wazao wa Elikana walikuwa: Amasai na Ahimothi,
26 Elcana son fils, Saphi son fils, Cénaath son fils,
Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,
27 Eliab son fils, Jéroboam son fils, Elcana son fils.
Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Samweli.
28 Fils de Samuel: Sari, premier-né, et Ables.
Wana wa Samweli walikuwa: Yoeli mzaliwa wake wa kwanza, na Abiya mwanawe wa pili.
29 Fils de Mérari: Mooli son fils, Lobeni son fils, Sémei son fils, Oza son fils,
Wafuatao ndio wazao wa Merari: Merari akamzaa Mahli, Mahli akamzaa Libni, Libni akamzaa Shimei, Shimei akamzaa Uza,
30 Samaa son fils, Aggia son fils, Asaïas son fils.
Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia, Hagia akamzaa Asaya.
31 Et voici ceux que David institua chefs des chœurs du tabernacle, lorsqu'il eut transféré l'arche à Jérusalem.
Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.
32 Et ils s'accompagnaient avec des instruments, devant le tabernacle du témoignage, jusqu'à ce que Salomon eût bâti le temple du Seigneur à Jérusalem. Et ils servaient, chacun selon la fonction qui lui était assignée.
Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.
33 Voici leurs noms et ceux de leurs pères: de Caath descendait: Hëman, chantre et harpiste, fils de Johel, fils de Samuel,
Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao: Kutoka ukoo wa Kohathi walikuwa: Hemani, mpiga kinanda, alikuwa mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli,
34 Fils d'Elcana, fils de Jéroboam, fils d'Eliel, fils de Thoü,
mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,
35 Fils de Suph, fils d'Elcana, fils de Maath, fils d'Amathi,
mwana wa Sufu, mwana wa Elikana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,
36 Fils d'Elcana, fils de Johel, fils d'Azarias, fils de Saphanie,
mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,
37 Fils de Thaath, fils d'Aser, fils d'Abiasaph, fils de Coré,
mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,
38 Fils d'Isaar, fils de Caath, fils de Lévi, fils d'Israël.
mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;
39 Et Asaph, chantre comme lui, qui se tenait à sa droite, était fils de Barachias, fils de Samaa,
na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume: Asafu mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,
40 Fils de Michel, fils de Baasie, fils de Melchias,
mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,
41 Fils d'Athani, fils de Zaaraï, fils d'Adaï,
mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,
42 Fils d'Etham, fils de Zamnaam, fils de Sémeï,
mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,
43 Fils de Jeth, petit-fils de Gerson, fils de Lévi.
mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
44 Et de Mérari descendaient les chantres qui se tenaient à gauche, dont le chef était: Ethan, fils de Cisa, fils d'Abe, fils de Maloch,
Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto: Ethani mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,
45 Fils d'Asebi,
mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,
46 Fils d'Amessias, fils de Bani, fils de Semer,
mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,
47 Fils de Mooli, fils de Musi, fils de Mérari, fils de Lévi.
mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
48 Et les lévites leurs frères, selon leurs familles paternelles, étaient attachés aux divers services du tabernacle de Dieu.
Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.
49 Aaron, et, après lui, ses fils sacrifiaient sur l'autel des holocaustes et sur l'autel des parfums; ils remplissaient toutes les fonctions relatives au Saint des saints; et ils priaient pour Israël, conformément à ce que leur avait commandé Moïse serviteur de Dieu.
Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
50 Voici les fils d'Aaron: Eléazar son fils, Phinéès son fils, Abisué son fils,
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni: Aroni akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
51 Bocci son fils, Ozi son fils, Saraïa son fils,
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Zerahia,
52 Mariel son fils, Amarias son fils, Achitob son fils,
Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
53 Sadoc son fils, Achimais son fils.
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.
54 Voici les demeures, les bourgs et les territoires, assignés par le sort, selon leurs familles, aux fils d'Aaron, et aux fils de Caath.
Zifuatazo ni sehemu walizopewa ziwe nchi yao kwa ajili ya makazi yao (walipewa wazao wa Aroni waliotoka katika ukoo wa Wakohathi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
55 Il leur fut donné Hébron, en la terre de Juda, et sa banlieue tout alentour.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda pamoja na sehemu ya malisho inayouzunguka.
56 Mais les champs de la ville et ses bourgs appartenaient à Caleb, fils de Jéphoné.
Lakini mashamba pamoja na vijiji vilivyouzunguka mji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 Les villes de refuge furent aussi concédées aux fils d'Aaron, savoir: Hébron, Lobna et sa banlieue, Selna et sa banlieue, Esthamo et sa banlieue,
Kwa hiyo wazao wa Aroni walipewa miji ifuatayo pamoja na eneo la malisho: Hebroni (mji wa makimbilio), Libna, Yatiri, Eshtemoa,
58 Jethar et sa banlieue, Dabir et sa banlieue,
Hileni, Debiri,
59 Asan et sa banlieue, Bethsamys et sa banlieue.
Ashani, Yuta na Beth-Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho.
60 Et, dans la tribu de Benjamin, Gabée et sa banlieue, Galemath et sa banlieue, Anathoth et sa banlieue. En tout treize villes par familles.
Kutoka kabila la Benyamini walipewa Gibeoni, Geba, Alemethi na Anathothi, pamoja na maeneo yake ya malisho. Miji hii kumi na mitatu iligawanywa miongoni mwa koo za Wakohathi.
61 Et le sort assigna au reste des fils de Caath, par familles, dix villes de la demi-tribu de Manassé, en deçà du Jourdain.
Wazao waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za nusu ya kabila la Manase.
62 Et aux fils de Gerson, par familles, treize villes des tribus d'Issachar, d'Aser, de Nephthali et de la demi-tribu de Manassé en Hasan.
Wazao wa Gershoni, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na mitatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri na Naftali kutoka sehemu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 Et aux fils de Mérari, par familles, douze villes des tribus de Ruben, de Gad et de Zabulon.
Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
64 Et les fils d'Israël accordèrent aux lévites ces villes et leurs banlieues.
Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yake ya malisho.
65 Le sort désigna dans les tribus de Juda, de Siméon et de Benjamin, les villes auxquelles les lévites donnèrent leurs noms,
Kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini walipewa miji iliyotajwa hapo juu.
66 D'après les familles des fils de Caath. Et ils eurent aussi des villes du territoire d'Ephraïm,
Baadhi ya koo za Wakohathi walipewa kama nchi yao miji kutoka kabila la Efraimu.
67 Y compris les villes de refuge: Sichem et sa banlieue, dans la montagne d'Ephraïm, Gazer et sa banlieue,
Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji wa makimbilio) na Gezeri,
68 Jecmaan et sa banlieue, Béthoron et sa banlieue.
Yokmeamu, Beth-Horoni,
69 Et, en d'autres territoires, Aïlon et sa banlieue, Gethremmon et sa banlieue.
Aiyaloni na Gath-Rimoni, pamoja na maeneo yake ya malisho.
70 Et de la demi-tribu de Manassé: Anar et sa banlieue, Jemblaan et sa banlieue, selon les familles du reste des fils de Caath.
Kutoka nusu ya kabila la Manase, Waisraeli waliwapa koo za Wakohathi waliobaki miji ya Aneri na Bileamu pamoja na maeneo yake ya malisho.
71 Les fils de Gerson, par familles, eurent dans l'autre demi-tribu de Manassé, Golan en Basan et sa banlieue, Aseroth et sa banlieue.
Wagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho: Katika nusu ya kabila la Manase: walipewa Golani katika Bashani na pia Ashtarothi.
72 Et dans la tribu d'Issachar: Cédés et sa banlieue, Deberi et sa banlieue, Dabor et sa banlieue,
Kutoka kabila la Isakari walipokea Kedeshi, Daberathi,
73 Ramoth, Aïnan et sa banlieue.
Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
74 Et dans la tribu d'Aser: Maasal et sa banlieue, Abdon et sa banlieue,
Kutoka kabila la Asheri walipokea Mashali, Abdoni,
75 Acac et sa banlieue, Rhoob et sa banlieue.
Hukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
76 Et dans la tribu de Nephthali: Cédés en Gaulée et sa banlieue, Hamoth et sa banlieue, Cariathaïm et sa banlieue.
Kutoka kabila la Naftali walipokea Kedeshi katika Galilaya, Hamoni na Kiriathaimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
77 Et dans la tribu de Zabulon: le sort attribua au reste des fils de Mérari, Remmon et sa banlieue, Thabor et sa banlieue.
Wamerari (Walawi waliobakia) walipokea miji ifuatayo: kutoka kabila la Zabuloni walipokea Yokneamu, Karta, Rimoni na Tabori pamoja na maeneo yake ya malisho.
78 Et dans la vallée du Jourdain à l'occident du fleuve: Jéricho, et dans la tribu de Ruben: Bosor dans le désert et sa banlieue, Jasa et sa banlieue,
Kutoka kabila la Reubeni, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko walipokea Bezeri ulioko jangwani, Yahasa,
79 Cadmoth et sa banlieue, Maephla et sa banlieue.
Kedemothi na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
80 Dans la tribu de Gad: Ramoth-Galaad et sa banlieue, Maanaïm et sa banlieue,
Na kutoka kabila la Gadi walipokea Ramothi huko Gileadi, Mahanaimu,
81 Esébon et sa banlieue, Jazer et sa banlieue.
Heshboni na Yazeri, pamoja na maeneo yake ya malisho.

< 1 Chroniques 6 >