< 1 Chroniques 17 >

1 Et quand David eut pris possession de son palais, il dit à Nathan le prophète: Voilà que j'habite une maison de cèdre, tandis que l'arche de l'alliance du Seigneur repose sous des courtines de peaux.
Baada ya Daudi kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, akamwambia nabii Nathani, “Hebu tazama, mimi ninakaa kwenye nyumba nzuri iliyojengwa kwa mierezi, wakati Sanduku la Agano la Bwana liko ndani ya hema.”
2 Et Nathan dit à David: Tout ce qui est en ton cœur, fais-le, car Dieu est avec toi.
Nathani akamjibu Daudi, “Lolote ulilo nalo moyoni mwako litende, kwa maana Mungu yu pamoja nawe.”
3 Mais, cette nuit même, la parole du Seigneur vint à Nathan, et lui dit:
Usiku ule neno la Mungu likamjia Nathani, kusema:
4 Va, et dis à mon serviteur David; Voici ce que dit le Seigneur: Tu ne me bâtiras pas un temple pour que je l'habite,
“Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Wewe hutanijengea mimi nyumba ili nikae humo.
5 Parce que je n'ai point résidé dans un temple depuis que j'ai tiré de l'Égypte les fils d'Israël jusqu'à ce jour, et que je me suis tenu dans un tabernacle et sous un voile.
Mimi sijakaa ndani ya nyumba tangu siku ile niliyowatoa Israeli kutoka Misri mpaka leo. Nimehama kutoka hema moja hadi jingine na kutoka mahali pamoja hadi pengine.
6 En quelque lieu que j'aie passé avec tout Israël, ai-je jamais dit à celle des tribus que j'avais chargée de prendre soin de tout le peuple: Pourquoi ne m'avez-vous point bâti une maison de cèdre?
Je, popote nilipokwenda pamoja na Waisraeli wote, wakati wowote nilimwambia kiongozi yeyote niliyemwagiza kuwachunga watu wangu, kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?’
7 Dis encore à mon serviteur David: Voici ce que dit le Seigneur tout- puissant: Je t'ai tiré de la bergerie quand tu marchais derrière les troupeaux, pour que tu sois roi de mon peuple Israël.
“Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikuchukua machungani na kutoka kuandama kondoo ili uwatawale watu wangu Israeli.
8 Je t'ai accompagné partout où tu as marché, j'ai exterminé devant toi tous tes ennemis, et je t'ai rendu célèbre autant que les plus renommés des grands de la terre.
Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
9 Et j'adopterai un lieu pour mon peuple Israël; je l'y fixerai et il s'y abritera, chacun aura sa demeure, et il ne sentira plus d'inquiétudes, et le fils de l'iniquité ne l'affligera plus comme il a fait dès le commencement,
Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali na nitawapa ili wawe na mahali pao wenyewe pa kuishi na wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
10 Depuis les temps où j'ai donné des juges à mon peuple; j'ai humilié tous tes ennemis, et je t'augmenterai, et le Seigneur te fera une maison.
na ambavyo wamefanya siku zote tangu nilipowachagua viongozi kwa ajili ya watu wangu Israeli. Pia nitawatiisha adui zenu wote. “‘Pamoja na hayo ninakuambia kwamba Bwana atakujengea nyumba:
11 Et, quand tes jours seront remplis, quand tu te seras endormi avec tes pères, j'élèverai après toi ta race et celui qui sera issu de ton sang; et je préparerai son règne.
Wakati wako utakapokuwa umekwisha, nawe ukawa umekwenda kukaa na baba zako, nitamwinua mzao wako aingie mahali pako kuwa mfalme, mmoja wa wana wako mwenyewe, nami nitaufanya imara ufalme wake.
12 Celui-là me bâtira un temple, et je dresserai son trône pour toujours.
Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili yangu, nami nitakifanya imara kiti cha ufalme wake milele.
13 Je serai pour lui un père, et il sera pour moi un fils, et je ne lui retirerai point ma miséricorde, comme je l'ai retirée à ceux qui t'ont précédé.
Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Kamwe sitaondoa upendo wangu kwake, kama nilivyouondoa kwa yeye aliyekutangulia.
14 Et je l'établirai en mon temple, et en son royaume pour toujours; et son trône sera toujours debout.
Nitamweka juu ya nyumba yangu na ufalme wangu milele; kiti chake cha enzi nitakifanya imara milele.’”
15 Ainsi, Nathan répéta à David toutes ces paroles, que lui-même avait ouïes en sa vision.
Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
16 Alors, le roi David s'en alla; et il se plaça devant le Seigneur, et il dit: Qui suis-je, Seigneur mon Dieu, et qu'est ma maison pour que vous m'aimiez à jamais?
Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Mimi ni nani, Ee Bwana Mungu, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
17 Ce que vous en avez fait c'était à vos yeux peu de chose, ô mon Dieu, et vous avez parlé de la maison de votre serviteur pour un avenir lointain, et vous m'avez regardé comme on regarde un ami, et vous m'avez élevé, Seigneur mon Dieu.
Kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Mungu, umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Umeniangalia kama mtu aliyetukuka kuliko watu wote, Ee Bwana Mungu.
18 Que pourra faire encore David devant vous pour vous glorifier? Vous connaissez maintenant votre serviteur.
“Daudi aweza kukuambia nini zaidi kuhusu kumheshimu mtumishi wako? Kwa maana wewe unamjua mtumishi wako,
19 Vous avez opéré ces grandes choses au gré de votre cœur.
Ee Bwana Mungu. Kwa ajili ya mtumishi wako, tena sawasawa na mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa sana na kujulisha ahadi hizi zote zilizo kubwa sana.
20 Seigneur, nul ne vous ressemble, nul n'est Dieu que vous, et vous vous êtes révélé par toutes les merveilles que nous avons oui redire.
“Hakuna aliye kama wewe, Ee Bwana Mungu, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe.
21 Et il n'est point sur la terre de peuple qui ressemble à Israël votre peuple. Il n'en est point que Dieu. ait guidé pour le racheter et s'en faire un peuple pour lui-même, pour se faire à lui-même un grand et glorieux nom, et pour expulser les nations devant votre peuple que vous avez délivré de l'Égypte.
Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli: taifa pekee duniani ambalo Mungu wake alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe na kujifanyia jina kwa ajili yake mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
22 Vous vous êtes donné, en Israël, un peuple qui sera votre peuple à jamais; et vous, Seigneur, vous êtes son Dieu.
Uliwafanya watu wako Israeli kuwa watu wako wewe mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana Mungu, umekuwa Mungu wao.
23 Maintenant donc, Seigneur, que la promesse que vous avez faite à votre serviteur, concernant sa maison, soit à jamais confirmée; faites comme vous avez dit.
“Sasa basi, Bwana ahadi uliyoweka kuhusu mtumishi wako na nyumba yake na uithibitishe milele. Fanya kama ulivyoahidi,
24 Et que votre nom soit glorifié à jamais, et que l'on y ait foi, et que l'on dise: Seigneur, Seigneur tout-puissant, Dieu d'Israël, la maison de David votre serviteur est érigée devant vous.
ili ithibitike na jina lako litakuwa kuu milele. Kisha watu watasema, ‘Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu aliye juu ya Israeli, ndiye Mungu wa Israeli.’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itafanywa imara mbele zako.
25 Car, Seigneur Dieu, vous avez révélé vos desseins à votre serviteur, disant: Je te bâtirai une maison; c'est à ce sujet que votre serviteur a pensé à vous prier face à face.
“Wewe, Mungu wangu, umemfunulia mtumishi wako Daudi kwamba utamjengea yeye nyumba. Hivyo mtumishi wako amekuwa na ujasiri wa kukuomba maombi haya.
26 Et maintenant, Seigneur, vous seul êtes Dieu, et c'est vous qui avez fait à votre serviteur ces magnifiques promesses.
Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu! Umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
27 Commencez donc et bénissez la maison de votre serviteur, pour qu'elle subsiste toujours devant vous; car, Seigneur, vous l'avez déjà bénie, bénissez-la donc à jamais.
Basi imekupendeza kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu milele machoni pako; kwa ajili yako, Ee Bwana, umeibariki, nayo itabarikiwa milele.”

< 1 Chroniques 17 >