< 1 Chroniques 16 >
1 Et ils introduisirent l'arche de Dieu, et la placèrent au milieu du tabernacle que David avait dressé pour elle, et l'on offrit devant Dieu des holocaustes et des hosties pacifiques.
Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
2 Quand David eut fait ses offrandes d'holocaustes et d'hosties pacifiques, il bénit le peuple au nom du Seigneur.
Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
3 Et il donna à chaque homme et à chaque femme d'Israël un pain de boulanger, et un pain pétri avec du miel.
Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
4 Et il institua devant l'arche de l'alliance du Seigneur ceux des lévites qui devaient y être employés, pour chanter et louer le Seigneur Dieu d'Israël, et lui rendre grâces.
Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
5 Asaph fut le chef, et il eut pour second Zacharie; puis, Jehiel, Semiramoth et Jehiel, Matthathias, Eliab, Banaïas et Abdedom: Jehiel jouait de la lyre et de la harpe, et Asaph faisait retentir des cymbales.
Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
6 Banaïas et Oziel les prêtres, sonnaient toujours de la trompette devant l'arche de l'alliance du Seigneur.
nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
7 Et ce jour-là, pour la première fois, David prescrivit que l'on chantât les louanges du Seigneur, sous la direction d'Asaph et de ses frères.
Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
8 Cantique. Rendez hommage au Seigneur, invoquez-le par son nom, faites connaître aux peuples ses désirs.
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
9 Chantez-le, chantez ses louanges; racontez à tous les merveilles qu'a faites le Seigneur.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
10 Louez son saint nom; le cœur qui cherche à lui âtre agréable sera réjoui.
Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
11 Cherchez le Seigneur et soyez forts; cherchez toujours son visage.
Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
12 Souvenez-vous des prodiges qu'il a faits, des merveilles et des jugements sortis de sa bouche.
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
13 Enfants d'Israël, ses serviteurs; fils de Jacob, ses élus;
enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14 Le Seigneur seul est notre Dieu; ses jugements sont sur toute la terre.
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
15 Souvenons-nous toujours de son alliance, de la loi qu'il nous a donnée pour des milliers de générations,
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
16 De son alliance avec Abraham; de son serment à Isaac,
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
17 Il l'a confirmé à Jacob comme un commandement, à Israël comme une alliance impérissable,
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
18 Disant: Je te donnerai la terre de Chanaan; c'est ta part d'héritage.
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
19 Alors, ils étaient en petit nombre, ils étaient humbles, et ils étaient passagers sur cette terre,
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
20 Et ils allèrent d'une nation à l'autre, et d'un royaume à un autre peuple,
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
21 Et à nul homme il ne permit de prévaloir sur eux, et à leur sujet il châtia des rois:
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
22 Ne touchez point à mes christs; ne maltraitez pas mes prophètes,
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
23 Chantez le Seigneur: que toute la terre le chante, proclamez chaque jour que lui seul est notre salut.
Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
24 [Racontez aux nations sa gloire, à tous les peuples ses merveilles.] Car le Seigneur est grand et digne de louanges infinies; il est redoutable plus que tous les dieux.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
25 [Racontez aux nations sa gloire, à tous les peuples ses merveilles.] Car le Seigneur est grand et digne de louanges infinies; il est redoutable plus que tous les dieux.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
26 Car, tous les dieux des nations sont des idoles, et notre Dieu a créé le ciel.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
27 Gloire et louange à lui face à face; force et joie au lieu où il réside.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
28 Tribus des nations, donnez au Seigneur, donnez au Seigneur force et gloire.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
29 Glorifiez le nom du Seigneur; prenez des dons et offrez-les au Seigneur en sa présence, et adorez le Seigneur dans ses demeures saintes.
mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
30 Que toute la terre ait crainte devant lui; que la terre s'affermisse et ne soit point ébranlée.
Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
31 Que le ciel se réjouisse, que la terre tressaille d'allégresse, et qu'ils disent aux nations: Le Seigneur règne.
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
32 La mer bruira dans sa plénitude, et l'arbre des champs avec tout ce qu'il porte se réjouira.
Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
33 Alors, les arbres de la forêt se réjouiront devant le Seigneur, parce qu'il est venu juger la terre.
Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
34 Rendez hommage au Seigneur, parce qu'il est bon et que sa miséricorde est éternelle.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
35 Et dites: Sauvez-nous, ô Dieu notre salut; recueillez-nous et séparez- nous des nations, afin que nous chantions les louanges de votre saint nom, et que noua mettions notre gloire à vous louer.
Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
36 Béni soit le nom du Seigneur Dieu d'Israël dans tous les siècles des siècles, et tout le peuple dira: Amen. Et ils louèrent le Seigneur.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
37 Et ils laissèrent là devant l'arche de l'alliance du Seigneur Asaph et ses frères, pour faire devant l'arche à perpétuité le service de chaque jour.
Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
38 Ils laissèrent aussi Abdedom et ses frères, au nombre de soixante-huit, et Abdedom, fils d'Idithun, et Osa pour être portiers.
Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
39 Et Sadoc le prêtre, avec ses frères les prêtres, fut laissé devant le tabernacle du Seigneur, sur le haut lieu de Gabaon,
Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
40 Afin d'offrir des holocaustes au Seigneur, sur l'autel des holocaustes à perpétuité, matin et soir, selon qu'il est écrit en la loi du Seigneur, qu'il a donnée aux fils d'Israël par la voix de Moïse, son serviteur.
ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
41 Et avec Sadoc étaient Hêman et Idithun, et le reste de ceux qu'on avait nominativement désignés pour louer le Seigneur, parce que sa miséricorde est éternelle.
Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
42 Et ils avaient avec eux des trompettes et des cymbales, pour les faire retentir, et les instruments accompagnant les cantiques de Dieu. Et les fils d'Idithun étaient gardiens des portes.
Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
43 Et le peuple s'en retourna chacun en sa demeure, et David s'en alla pour bénir sa maison.
Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.