< 1 Chroniques 13 >
1 Et David tint conseil avec tous ses chefs, centeniers ou commandants de mille hommes.
Daudi alishauriana na kila afisa wake, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia.
2 Et David dit à toute l'Église d'Israël: Si cela vous paraît bon et agréable au Seigneur notre Dieu, envoyons chez nos frères qui sont restés en tout le territoire d'Israël, et chez les prêtres et les lévites, dans les villes où ils résident; qu'il se réunissent à nous,
Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote la Israeli, “Kama mkiona ni vyema, na kama ni mapenzi ya Bwana Mungu wetu, tupeleke ujumbe kwa ndugu zetu wengine walio mbali na walio karibu katika nchi yote ya Israeli, pia kwa makuhani na Walawi walio pamoja nao katika miji yao na katika sehemu zao za malisho yao, waje waungane na sisi.
3 Et amenons auprès de nous l'arche de notre Dieu; car, depuis l'avènement de Saül, on ne l'a point demandée.
Sisi na tulirudishe Sanduku la Mungu wetu kwetu kwa maana hatukujali wakati wa utawala wa Sauli.”
4 Et toute l'Église dit qu'il fallait faire ainsi; car ce discours avait plu à tout le peuple.
Kusanyiko lote likakubaliana kufanya hivyo, kwa sababu ilionekana vyema kwa watu wote.
5 Et David réunit tout Israël, depuis les confins de l'Égypte jusqu'aux défilés d'Emath, pour ramener l'arche de la ville d'Iarim.
Basi Daudi akawakusanya Waisraeli wote, kuanzia Mto Shihori ulioko Misri hadi Lebo-Hamathi, ili kulileta Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu.
6 Et David la ramena; et tout Israël entra dans la ville de David, qui est en Juda, pour y introduire l'arche du Seigneur Dieu assis sur les chérubins, où est invoqué son nom.
Daudi akiwa pamoja na Waisraeli wote wakaenda Baala ya Yuda (yaani Kiriath-Yearimu) kulipandisha Sanduku la Mungu Bwana, yeye anayeketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi: Sanduku linaloitwa kwa Jina lake, kutoka huko.
7 On avait posé l'arche de Dieu sur un chariot neuf de la maison d'Aminadab; Oza et ses frères conduisaient l'attelage.
Wakalisafirisha Sanduku la Mungu kwa gari jipya la kukokotwa na maksai kutoka nyumba ya Abinadabu, Uza na Ahio wakiliongoza gari hilo.
8 Et David et tout Israël jouaient de tout leur cœur de la flûte, de la lyre, du tambour, et des cymbales, et de la harpe, au milieu des cantiques.
Daudi pamoja na Waisraeli wote walikuwa wanasifu kwa nguvu zao zote mbele za Mungu, kwa nyimbo na kwa vinubi, zeze, matari, matoazi na tarumbeta.
9 Et ils vinrent jusqu'à l'aire; là, Oza étendit la main pour maintenir l'arche que le mouvement d'un bœuf avait fait pencher.
Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Kidoni, Uza akaunyoosha mkono wake ili kulizuia Sanduku, kwa sababu maksai walijikwaa.
10 Mais le Seigneur s'irrita contre Oza, et il le frappa en ce lieu même, parce qu'il avait porté la main sur l'arche; et il mourut là devant Dieu.
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza, akampiga kwa sababu aliuweka mkono wake kwenye Sanduku. Kwa hiyo akafa pale mbele za Mungu.
11 Et David fut abattu, parce que Dieu avait châtié Oza, et ce lieu fut appelé le Châtiment d'Oza, nom qu'il porte encore de nos jours.
Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, mahali pale pakaitwa Peres-Uza hadi leo.
12 Et, ce jour-là, David eut crainte du Seigneur, et il dit: Comment ferai- je entrer chez moi l'arche du Seigneur?
Siku ile Daudi akamwogopa Mungu naye akauliza. “Nitawezaje kulichukua Sanduku la Mungu kwangu?”
13 Et David ne ramena pas l'arche avec lui dans la ville de David; mais la fit placer en la maison d'Abdara le Géthéen.
Hakulichukua hilo Sanduku akae nalo katika Mji wa Daudi. Badala yake, akalipeleka nyumbani kwa Obed-Edomu, Mgiti.
14 Et l'arche du Seigneur resta trois mois en la maison d'Abdara le Géthéen, et le Seigneur bénit toute la maison d'Abdara et tout ce qui lui appartenait.
Sanduku la Mungu likabaki pamoja na jamaa ya Obed-Edomu, nyumbani kwake kwa miezi mitatu, naye Bwana akaibariki nyumba yake pamoja na kila kitu alichokuwa nacho.