< Psaumes 75 >

1 Au chef des chantres. Al tachhêt. Psaume d’Assaph. Cantique. Nous te rendons grâce, ô Dieu, nous te rendons grâce, ton nom est près de nous; qu’on proclame tes merveilles!
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 "Quand, dit Dieu, j’en aurai fixé l’heure, je rendrai mes arrêts avec équité.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 Que la terre en soit alarmée avec ses habitants, moi, je raffermirai ses colonnes." (Sélah)
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 Je dis aux insensés: "Trêve de folies!" Aux méchants: "Ne relevez point la tête!"
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 Ne relevez pas si haut la tête, ne vous rengorgez pas pour parler avec insolence;
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 car ni de l’orient, ni du couchant, ni du désert ne vient la grandeur.
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 C’Est Dieu qui est l’arbitre: il abaisse l’un, il élève l’autre.
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 Car l’Eternel tient une coupe en sa main, où écume un vin tout mêlé d’aromates; de ce vin il verse des rasades, mais la lie, ce sont tous les méchants de la terre qui l’aspirent et la boivent.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 Pour moi, je le proclamerai sans trêve, je chanterai le Dieu de Jacob.
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 J’Abattrai toutes les cornes des méchants; les cornes des justes se dresseront bien haut.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

< Psaumes 75 >