< Psaumes 28 >
1 De David. C’Est vers toi que je crie, ô Seigneur! Mon Rocher, ne m’oppose pas ton silence, car si tu gardais le silence à mon égard, je serais pareil à ceux qui descendent au tombeau.
Zaburi ya Daudi. Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu; usiwe kwangu kama kiziwi. Kwa sababu ukinyamaza nitafanana na walioshuka shimoni.
2 Ecoute ma voix suppliante quand je t’invoque, quand j’élève les mains vers ton auguste sanctuaire.
Sikia kilio changu unihurumie ninapokuita kwa ajili ya msaada, niinuapo mikono yangu kuelekea Patakatifu pa Patakatifu pako.
3 Ne me confonds pas avec les méchants, avec les artisans d’iniquité, qui parlent paix à leurs proches, et n’ont que méchanceté au cœur.
Usiniburute pamoja na waovu, pamoja na hao watendao mabaya, ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri, lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
4 Donne-leur le prix de leur conduite, de leurs actes pervers, traite-les selon l’œuvre de leurs mains; paie-leur le salaire qu’ils méritent.
Walipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na matendo yao maovu; walipe sawasawa na kazi za mikono yao, uwalipe wanavyostahili.
5 Car ils ne prêtent aucune attention aux actes de l’Eternel, ni à l’œuvre de ses mains: qu’il les renverse pour ne plus les relever!
Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana, na yale ambayo mikono yake imetenda, atawabomoa na kamwe hatawajenga tena.
6 Béni soit le Seigneur, car il a entendu ma voix suppliante!
Bwana asifiwe, kwa maana amesikia kilio changu nikimwomba anihurumie.
7 L’Eternel est ma force, mon bouclier; en lui mon cœur s’est confié et j’ai été secouru. Aussi mon cœur est-il en joie. Par mon cantique, je vais lui rendre grâce.
Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
8 L’Eternel est une force pour son peuple, un rempart protecteur pour son oint.
Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
9 Prête assistance à ton peuple et bénis ton héritage: conduis-les comme un berger et soutiens-les jusque dans l’éternité.
Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.