< Psaumes 106 >

1 Alléluia! Rendez hommage à l’Eternel, car sa grâce dure à jamais.
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Qui saura dire la toute-puissance de l’Eternel, exprimer toute sa gloire?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Heureux ceux qui respectent le droit, pratiquent la justice en tout temps!
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Souviens-toi de moi, ô Eternel, dans ta bienveillance pour ton peuple, veille sur moi, par ta protection,
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 pour que je puisse voir le bonheur de tes élus, me réjouir de la joie de ton peuple, me glorifier de concert avec ton héritage.
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 Nous avons péché tout comme nos pères, nous avons mal agi, nous sommes coupables!
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Nos pères, en Egypte, n’ont pas compris tes miracles, ni gardé le souvenir de tes nombreux bienfaits! Ils se révoltèrent aux bords de la mer, de la mer des Joncs.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 Lui cependant les secourut à cause de son nom, pour faire connaître sa puissance.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 Il apostropha la mer des Joncs, et elle se dessécha, il leur fit traverser les flots comme une terre nue.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 Il leur porta secours contre l’oppresseur, les délivra de la main de l’ennemi.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 Les eaux recouvrirent leurs persécuteurs, pas un d’entre eux n’en réchappa.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 Alors ils eurent foi en ses paroles, et chantèrent ses louanges.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 Bien vite ils oublièrent ses œuvres; ils ne mirent pas leur attente dans ses desseins.
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 Ils furent pris d’ardentes convoitises dans le désert, et mirent Dieu à l’épreuve dans la solitude.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 Il leur accorda ce qu’ils réclamaient, mais envoya la consomption dans leurs organes.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 Ils furent jaloux de Moïse dans le camp, d’Aaron, le saint de l’Eternel.
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 La terre, s’entrouvrant, engloutit Dathan, elle se referma sur la bande d’Abirâm.
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 Un feu consuma leur troupe, une flamme embrasa les impies.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 Ils fabriquèrent un veau près du Horeb, et se prosternèrent devant une idole en fonte.
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 Ils troquèrent ainsi leur gloire contre l’effigie d’un bœuf qui broute l’herbe.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 Ils avaient oublié Dieu, leur sauveur, qui avait accompli de si grandes choses en Egypte,
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 des merveilles dans le pays de Cham, de formidables prodiges près de la mer des Joncs.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 Il parlait de les anéantir, si Moïse, son élu, ne se fût placé sur la brèche devant lui, pour détourner sa colère prête à tout détruire.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 Puis ils montrèrent du dédain pour un pays délicieux, n’ayant pas foi en sa parole.
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 Ils murmurèrent dans leurs tentes, n’écoutèrent point la voix de l’Eternel;
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 et il leva la main contre eux pour jurer qu’il les ferait succomber dans le désert,
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 qu’il rejetterait leurs descendants parmi les nations, et les disperserait dans leurs contrées.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 Ils se prostituèrent à Baal-Peor, et mangèrent des sacrifices offerts à des dieux inanimés.
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 Ils déchaînèrent la colère par leurs actes, et un fléau fit irruption parmi eux.
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 Mais Phinéas se leva pour faire justice, et le fléau cessa de sévir.
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 Cette action lui fut comptée comme un mérite, d’âge en âge, jusque dans l’éternité.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 Ils suscitèrent le courroux divin aux eaux de Meriba, et il advint du mal à Moïse à cause d’eux.
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 Car ils furent rebelles à l’esprit de Dieu, et ses lèvres prononcèrent l’arrêt.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 Ils n’exterminèrent point les nations que l’Eternel leur avait désignées.
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 Ils se mêlèrent aux peuples et s’inspirèrent de leurs coutumes,
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 adorant leurs idoles, qui devinrent pour eux un piège.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 Ils sacrifièrent leurs fils et leurs filles aux démons,
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 répandirent du sang innocent, le sang de leurs fils et de leurs filles, qu’ils immolaient aux idoles de Canaan, et le pays fut déshonoré par des flots de sang.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 Ils se souillèrent par leurs œuvres, et leurs actes furent une longue prostitution.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 La colère de l’Eternel s’alluma contre son peuple, et il prit en horreur son héritage.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 Il les livra au pouvoir des nations, ceux qui les haïssaient devinrent leurs maîtres.
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 Leurs ennemis les opprimèrent, et les firent plier sous leur joug.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Maintes fois Dieu les délivra, mais ils redevenaient rebelles de propos délibéré, et tombaient en décadence par leurs fautes.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 Il devenait attentif à leur détresse, quand il entendait leurs supplications,
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 se souvenant, pour leur bien, de son alliance, et se laissant fléchir dans son infinie miséricorde.
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 Il émouvait la pitié en leur faveur chez tous ceux qui les retenaient captifs.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Viens à notre secours, Eternel, notre Dieu, rassemble-nous d’entre les nations, pour que nous rendions hommage à ton saint nom, et cherchions notre gloire dans tes louanges.
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Béni soit l’Eternel, le Dieu d’Israël, d’éternité en éternité, et que le peuple tout entier dise: "Amen! Alléluia!"
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.

< Psaumes 106 >