< Proverbes 25 >
1 Les proverbes qui suivent émanent également de Salomon et ont été colligés par les gens d’Ezéchias, roi de Juda.
Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
2 La gloire de l’Eternel, c’est de s’entourer de mystère; la gloire du roi est d’examiner les choses à fond.
Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
3 Tout comme les cieux en hauteur, la terre en profondeur, le cœur des rois est insondable.
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
4 Qu’on sépare les scories de l’argent, et l’orfèvre le travaillera en objet d’art.
Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
5 Qu’on éloigne le méchant de la présence du roi, et son trône se trouvera affermi par la justice.
Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
6 Ne te pavane pas devant le roi et n’occupe pas la place des grands.
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
7 Car mieux vaut pour toi qu’on te dise: "Monte là!" que si on t’abaissait devant les nobles, chose que tes yeux ont déjà pu voir.
ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
8 Ne t’engage pas inconsidérément dans les luttes: tu t’exposerais à ne plus savoir que faire à la fin, si ton prochain te couvrait de confusion.
usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
9 As-tu un procès avec, ton prochain, défends-le, mais sans dévoiler des secrets qui ne t’appartiennent pas:
Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
10 tu serais blâmé par ceux qui t’entendent et décrié sans retour.
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
11 Des pommes d’or dans des vases d’argent ajourés, telle une parole prononcée à propos.
Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
12 Un anneau d’or, un collier de perles, tel le sage qui fait la morale à une oreille attentive.
Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
13 Comme une fraîcheur de neige au temps de la moisson, tel le, messager, fidèle à son mandat: il restaure l’âme de son maître.
Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
14 Des nuages et du vent, mais de pluie point! Tel est l’homme qui fait grand bruit de ses dons illusoires.
Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
15 Par une patience inlassable, on capte la faveur d’un supérieur; un doux parler brise la plus dure résistance.
Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
16 As-tu trouvé du miel, manges-en à ta suffisance; mais évite de t’en bourrer: tu le rejetterais.
Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
17 Espace tes visites dans la maison de ton ami: il en aurait bientôt assez de toi et te prendrait en grippe.
Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
18 Une massue, un glaive, une flèche acérée, tel l’homme qui porte un faux témoignage contre son prochain.
Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
19 Une dent branlante, un pied chancelant, voilà ce que vaut au jour du malheur la confiance qu’on a dans un traître.
Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
20 Enlever son vêtement par un jour glacial, verser du vinaigre sur du nitre, ainsi fait celui qui entonne des chants pour un cœur affligé.
Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
21 Si ton ennemi a faim, donne lui à manger; s’il a soif, donne-lui à boire;
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
22 car ainsi tu attises des charbons sur sa tète, et le Seigneur t’en récompensera.
Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
23 Le vent du Nord produit la pluie, et la langue qui calomnie en secretles visages aigris.
Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
24 Mieux vaut habiter l’angle d’un toit que de partager un logis avec une femme acariâtre.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
25 De l’eau fraîche sur un corps fatigué, telle une bonne nouvelle venant d’un pays lointain.
Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 Une source boueuse, une fontaine aux eaux troubles, tel est le juste qui fléchit devant le méchant.
Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
27 Manger trop de miel ne vaut rien; mais étudier à fond les choses difficiles est un honneur.
Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
28 Une ville démantelée, sans remparts, tel est l’homme dont le tempérament ne connaît pas de frein.
Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.