< Nombres 33 >

1 Voici l’itinéraire des enfants d’Israël, depuis qu’ils furent sortis du pays d’Egypte, selon leurs légions, sous la conduite de Moïse et d’Aaron.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Moïse inscrivit leurs départs et leurs stations sur l’ordre de l’Éternel; voici donc leurs stations et leurs départs:
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 ils partirent de Ramsès dans le premier mois, le quinzième jour du premier mois; le lendemain de la Pâque, les enfants d’Israël sortirent, triomphants, à la vue de toute l’Egypte,
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 tandis que les Egyptiens ensevelissaient ceux que l’Éternel avait frappés parmi eux, tous les premiers-nés, l’Éternel faisant ainsi justice de leurs divinités.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 Partis de Ramsès, les enfants d’Israël s’arrêtèrent à Soukkot.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Ils repartirent de Soukkot et se campèrent à Ethâm, situé sur la lisière du désert.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Puis ils partirent d’Ethâm, rebroussèrent vers Pi-Hahirot, qui fait face à Baal-Cefôn, et campèrent devant Migdol.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Ils partirent de devant Pi-Hahirot, se dirigèrent, en traversant la mer, vers le désert, et après une marche de trois journées dans le désert d’Ethâm, s’arrêtèrent à Mara.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Partis de Mara, ils arrivèrent à Elim. Or, à Elim étaient douze sources d’eau et soixante-dix palmiers, et ils s’y campèrent.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Puis ils repartirent d’Elim, et campèrent près de la mer des Joncs.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Ils repartirent de la mer des Joncs et campèrent dans le désert de Sîn.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Ils repartirent du désert de Sîn, et campèrent à Dofka.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 Ils repartirent de Dofka, et campèrent à Alouch.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 Ils repartirent d’Alouch, et campèrent à Rephidîm, où il n’y eut point d’eau à boire pour le peuple.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 IIs repartirent de Rephidîm, et campèrent dans le désert de Sinaï.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Ils repartirent du désert de Sinaï, et campèrent à Kibroth-Hattaava.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Ils repartirent de Kibroth-Hattaava, et campèrent à Hacêroth.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 Ils repartirent de Hacêroth, et campèrent à Rithma.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 Ils repartirent de Rithma, et campèrent à Rimmôn-Péreç.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 Ils repartirent de Rimmôn-Péreç, et campèrent à Libna,
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Ils repartirent de Libna, et campèrent à Rissa.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 Ils repartirent de Rissa, et campèrent à Kehêlatha.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 Ils repartirent de Kehêlatha, et campèrent au mont Chéfer.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Ils repartirent du mont Chéfer, et campèrent à Harada.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 Ils repartirent de Harada, et campèrent à Makhêloth.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 Ils repartirent de Makhêloth, et campèrent à Tahath.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Ils repartirent de Tahath, et campèrent à Térah.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 Ils repartirent de Térah, et campèrent à Mitka.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 Ils repartirent de Mitka, et campèrent à Haschmona.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 Ils repartirent de Haschmona, et campèrent à Mossêroth.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 Ils repartirent de Mossêroth, et campèrent à Benê-Yaakan.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 Ils repartirent de Benê-Yaakan, et campèrent à Hor-Haghidgad.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 Ils repartirent de Hor-Haghidgad, et campèrent à Yotbatha.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 IIs repartirent de Yotbatha, et campèrent à Abrona.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 Ils repartirent d’Abrona, et campèrent à Asiongaber.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 Ils repartirent d’Asiongaber, et campèrent au désert de Cîn, c’est-à-dire à Kadêch.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 Ils repartirent de Kadêch et campèrent à Hor-la-Montagne, à l’extrémité du pays d’Edom.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 Aaron, le pontife, monta sur cette montagne par ordre de l’Éternel, et y mourut. C’Était la quarantième année du départ des Israélites du pays d’Egypte, le premier jour du cinquième mois.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Aaron avait cent vingt-trois ans lorsqu’il mourut à Hor-la-Montagne.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 C’Est alors que le Cananéen, roi d’Arad, qui habitait au midi du pays de Canaan, apprit l’arrivée des enfants d’Israël.
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 Puis, ils partirent de Hor-la-Montagne, et vinrent camper à Çalmona.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Ils repartirent de Çalmona, et campèrent à Pounôn.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Ils repartirent de Pounôn, et campèrent à Oboth.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 Ils repartirent d’Oboth et campèrent à lyyê-Haabarîm, vers les confins de Moab.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Ils repartirent d’Iyyîm, et campèrent à Dibôn-Gad.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 Ils repartirent de Dibôn-Gad, et campèrent à Almôn-Diblathayim.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 Ils repartirent d’Almôn-Diblathayim et campèrent parmi les monts Abarim, en face de Nébo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 Ils repartirent des monts Abarîm et campèrent dans les plaines de Moab, près du Jourdain qui est vers Jéricho.
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 Ils occupaient la rive du Jourdain, depuis Bêth-Hayechimoth jusqu’à Abêl-Hachittîm, dans les plaines de Moab.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 L’Éternel parla ainsi à Moïse dans les plaines de Moab, près du Jourdain vers Jéricho:
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 "Parle aux enfants d’Israël en ces termes: Comme vous allez passer le Jourdain pour atteindre le pays de Canaan,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 quand vous aurez chassé devant vous tous les habitants de ce pays, vous anéantirez tous leurs symboles, toutes leurs idoles de métal, et ruinerez tous leurs hauts-lieux.
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 Vous conquerrez ainsi le pays et vous vous y établirez; car c’est à vous que je le donne à titre de possession.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 Vous lotirez ce pays, par la voie du sort, entre vos familles, donnant toutefois aux plus nombreux un plus grand patrimoine et aux moins nombreux un patrimoine moindre, chacun recevant ce que lui aura attribué le sort; c’est dans vos tribus paternelles que vous aurez vos lots respectifs.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 Or, si vous ne dépossédez pas à votre profit tous les habitants de ce pays, ceux que vous aurez épargnés seront comme des épines dans vos yeux et comme des aiguillons à vos flancs: ils vous harcèleront sur le territoire que vous occuperez;
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 et alors, ce que j’ai résolu de leur faire, je le ferai à vous-mêmes."
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< Nombres 33 >