< Nombres 26 >

1 Or, à la suite de cette mortalité, l’Éternel dit à Moïse et à Eléazar, fils d’Aaron le pontife, ce qui suit:
Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,
2 "Faites le relevé de la communauté entière des enfants d’Israël, depuis l’âge de vingt ans et au-delà, par familles paternelles; de tous ceux qui sont aptes au service en Israël."
“Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”
3 Moïse et Eléazar le pontife leur en firent part, dans les plaines de Moab, au bord du Jourdain faisant face à Jéricho, en disant:
Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,
4 "…Depuis l’âge de vingt ans et au-delà; ainsi que l’Éternel l’avait prescrit à Moïse et aux enfants d’Israël, lorsqu’ils furent sortis du pays d’Egypte."
“Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.” Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:
5 Ruben, premier-né d’Israël. Les fils de Ruben: Hénok, d’où la famille des Hénokites; de Pallou, la famille des Pallouïtes;
Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;
6 de Heçrôn, la famille des Heçronites; de Karmi, la famille des Karmites.
kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.
7 Telles sont les familles issues de Ruben; on y compta quarante-trois mille sept cent trente hommes.
Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.
8 Fils de Pallou: Eliab.
Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,
9 Fils d’Eliab: Nemouêl, Dathan et Abiram. C’Est ce Dathan et cet Abiram, dignitaires de la communauté, qui s’attaquèrent à Moïse et à Aaron avec la faction de Coré, lorsque celle-ci s’attaqua à l’Éternel.
nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.
10 Mais la terre ouvrit son sein et les engloutit avec Coré, pendant que périssait le reste du parti, que le feu consumait les deux cent cinquante hommes, frappés pour l’exemple.
Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.
11 Quant aux fils de Coré, ils ne périrent point.
Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.
12 Fils de Siméon, selon leurs familles: de Nemouêl, la famille des Nemouêlites; de Yamîn, la famille des Yaminites; de Yakhîn, la famille des Yakhinites;
Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;
13 de Zérah, la famille des Zarhites; de Chaoul, la famille des Chaoulites.
kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
14 Telles sont les familles issues de Siméon: vingt-deux mille deux cents hommes.
Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.
15 Fils de Gad, selon leurs familles: de Cefôn, la famille des Cefonites; de Hagghi, la famille des Hagghites; de Chouni, la famille des Chounites;
Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;
16 d’Ozni, la famille des Oznites; de Eri, la famille des Erites;
kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;
17 d’Arod, la famille des Arodites; d’Arêli, la famille des Arêlites.
kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.
18 Telles sont les familles des fils de Gad, selon leur dénombrement: quarante mille cinq cents hommes.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.
19 Fils de Juda: Er et Onân; mais Er et Onân moururent dans le pays de Canaan.
Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.
20 Les autres fils de Juda furent, selon leurs familles: Chêla, d’où la famille des Chêlanites; de Péreç, la famille des Parcites; de Zérah, la famille des Zarhites.
Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela; kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi; kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.
21 Les fils de Péreç furent: Heçrôn, d’où la famille des Heçronites; Hamoul, d’où la famille des Hamoulites.
Wazao wa Peresi walikuwa: kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
22 Telles sont les familles de Juda, selon leur dénombrement: soixante-seize mille cinq cents hommes.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.
23 Fils d’Issachar, selon leurs familles: Tola, d’où la famille des Tolaïtes; Pouvva, d’où la famille des Pounites;
Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;
24 de Yachoub, la famille des Yachoubites; de Chimrôn, la famille des Chimronites.
kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
25 Telles sont les familles d’Issachar, selon leur dénombrement: soixante-quatre mille trois cents hommes.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.
26 Fils de Zabulon, selon leurs familles: de Séred, la famille des Sardites; d’Elôn, la famille des Elonites; de Yahleêl, la famille des Yahleêlites.
Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.
27 Telles sont les familles issues de Zabulon, selon leur dénombrement: soixante mille cinq cents hommes.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.
28 Fils de Joseph, selon leurs familles: Manassé et Ephraïm.
Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:
29 Fils de Manassé: Makhir, d’où la famille des Makhirites. Makhir engendra Ghilad: de Ghilad, la famille des Ghiladites.
Wazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi); kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.
30 Suivent les fils de Ghllad: lézer, d’où la famille des lézrites; de Hêlek, la famille des Hélkites;
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi: kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;
31 puis Asriêl, d’où la famille des Asriêlites; Chékem, d’où la famille des Chikmites;
kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;
32 Chemida, d’où la famille des Chemidaïtes; de Héfer, la famille des Héfrites.
kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.
33 Celofhad, fils de Héfer, n’eut point de fils, mais seulement des filles. Les filles de Celofhad se nommaient: Mahla, Nos, Hogla, Milca et Tirça.
(Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)
34 Ce sont là les familles de Manassé: on y comptait cinquante-deux mille sept cents hommes.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.
35 Ceux-ci sont les fils d’Ephraïm, selon leurs familles: de Choutélah, la famille des Choutalhites; de Béker, la famille des Bakrites; de Tahân, la famille des Tahanites.
Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao: kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;
36 Et ceux-ci sont les descendants de Choutélah: Erân, d’où la famille des Eranites.
Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.
37 Telles sont les familles des fils d’Ephraïm, selon leur dénombrement: trente-deux mille cinq cents hommes. Tels sont les descendants de Joseph, selon leurs familles.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.
38 Fils de Benjamin, selon leurs familles: de Béla, la famille des Balites; d’Achbêl, la famille des Achbélites; d’Ahiram, la famille des Ahiramites;
Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;
39 de Chefoufam, la famille des Chefoufamites; de Houfam, la famille des Houfamites.
kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
40 Béla eut pour fils Ard' et Naamân: d’où la famille des Ardites, et de Naamân, la famille des Naamites.
Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa: kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.
41 Tels sont les descendants de Benjamin, selon leurs familles: on y compta quarante-cinq mille six cents hommes.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.
42 Voici les descendants de Dan, selon leurs familles: de Chouham, la famille des Chouhamites. Ce sont là les familles de Dan, compté selon ses familles.
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani:
43 Total des familles issues de Chouham, d’après leur dénombrement: soixante-quatre mille quatre cents hommes.
Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.
44 Fils d’Asher, selon leurs familles: de Yimna, la famille des Yimna; de Yichvi, la famille des Yichvites; de Berïa, la famille des Beriites.
Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;
45 Pour les fils de Berïa: de Héber, la famille des Hébrites; de Malkiêl, la famille des Malkiélites.
kutoka kwa wazao wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.
46 Puis la fille d’Asher, nommée Sérah.
(Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)
47 Telles sont les familles des fils d’Asher, selon leur dénombrement: cinquante-trois mille quatre cents hommes.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.
48 Fils de Nephtali, selon leurs familles: de Yahceêl, la famille des Yahceélites; de Gouni, la famille des Gounites;
Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;
49 de Yêcer, la famille des Yiçrites; de Chillem, la famille des Chillémites.
kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
50 Telles sont les familles de Nephtali, compté selon ses familles; leur dénombrement donna quarante-cinq mille quatre cents hommes.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.
51 Résultat du dénombrement des enfants d’Israël: six cent un mille sept cent trente hommes.
Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.
52 L’Éternel parla à Moïse en ces termes:
Bwana akamwambia Mose,
53 "C’Est entre ceux-là que le pays sera partagé comme héritage, selon le relevé des noms.
“Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.
54 Aux plus nombreux tu donneras une plus grande part, aux moins nombreux une part inférieure: chaque tribu recevra sa part selon le chiffre de sa population.
Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.
55 Toutefois, c’est au sort qu’on distribuera le pays; chacun aura son lot selon la désignation de sa tribu paternelle.
Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.
56 Ce lot sera attribué par la voie du sort, que la famille soit considérable ou non."
Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”
57 Voici maintenant le relevé des Lévites, selon leurs familles: pour Gerson, la famille des Gersonites; pour Kehath, la famille des Kehathites; pour Merari, la famille des Merarites.
Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
58 Voici les familles Issues de Lévi: la famille des Libnites, la famille des Hébronites, celle des Mahlites, celle des Mouchites, celle des Coréites. Kehath engendra Amram.
Hizi pia zilikuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni; ukoo wa Wahebroni; ukoo wa Wamahli; ukoo wa Wamushi; ukoo wa wana wa Kora. (Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu;
59 Et le nom de l’épouse d’Amram était Jocabed, fille de Lévi, laquelle naquit à Lévi en Egypte. Elle enfanta à Amram Aaron, Moïse et Miryam, leur sœur.
jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.
60 Aaron eut pour fils Nadab et Abihou, Eléazar et Ithamar;
Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
61 mais Nadab et Abihou moururent, pour avoir apporté un feu profane devant le Seigneur.
Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)
62 Or, leur population dénombrée se monta à vingt-trois mille mâles âgés d’un mois et au-dessus; car ils n’avaient point figuré dans le recensement des enfants d’Israël, n’ayant point reçu de patrimoine comme ceux-ci.
Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.
63 Tel fut le résultat du recensement opéré par Moïse, et le pontife Eléazar à l’égard des enfants d’Israël, dans les plaines de Moab, près du Jourdain, vers Jéricho.
Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
64 Parmi eux ne se trouvait pas un seul homme de ceux qu’avait recensés Moïse et le pontife Aaron, lorsqu’ils avaient dénombré les Israélites dans le désert de Sinaï.
Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.
65 Car l’Éternel avait déclaré, quant à ceux-là, qu’ils devaient mourir dans le désert; et aucun d’eux n’avait survécu, excepté Caleb, fils de Yefounné, et Josué, fils de Noun.
Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.

< Nombres 26 >