< Néhémie 4 >

1 Lorsque Sanballat apprit que nous étions en train de rebâtir le mur, il en fut contrarié et entra dans une grande colère. II tourna en dérision les Judéens,
Sanbalati aliposikia kwamba tulikuwa tunajenga ukuta upya, alikasirika na akawa na uchungu sana. Aliwadhihaki Wayahudi
2 et dit devant ses frères et les gens de guerre de Samarie: "Que se proposent ces misérables Judéens? Les laissera-t-on faire? Offriront-ils des sacrifices? En viendront-ils à bout aujourd’hui? Rendront-ils la vie aux pierres tirées des tas de poussière et qui ont été brûlées?"
mbele ya rafiki zake na jeshi la Samaria, akisema, “Hawa Wayahudi wanyonge wanafanya nini? Je, wataweza kuurudishia ukuta wao? Je, watatoa dhabihu? Je, wataweza kumaliza kuujenga kwa siku moja? Je, wataweza kufufua mawe kutoka malundo ya vifusi yaliyoungua hivyo?”
3 Tobia l’Ammonite, à côté de lui, ajoutait: "Qu’ils bâtissent toujours: il suffira qu’un renard monte dessus pour renverser leur muraille de pierres!"
Tobia Mwamoni aliyekuwa upande wake akasema, “Wanachokijenga, hata kama mbweha angepanda juu yake, huo ukuta wao wa mawe angeliubomoa!”
4 Ecoute, ô notre Dieu, comme nous sommes devenus un objet de mépris; fais retomber leurs outrages sur leur tête, et livre-les au pillage sur une terre de captivité.
Ee Mungu wetu, utusikie, kwa kuwa tumedharauliwa. Warudishie matukano yao kwenye vichwa vyao wenyewe. Uwatoe ili wawe nyara katika nchi ya waliowateka.
5 Ne voile pas leur iniquité; que leur méfait ne s’efface point devant toi, puisqu’ils se sont déchaînés contre les travailleurs!
Usiusitiri uovu wao, wala usifute dhambi zao mbele zako, kwa kuwa wamewatukana wajenzi mbele.
6 Cependant, nous continuâmes à rebâtir le mur; et lorsque tout le mur fut bouché jusqu’à mi-hauteur, le peuple eut de nouveau du cœur à l’ouvrage.
Basi tuliujenga upya ukuta mpaka wote ukafikia nusu ya kimo chake, kwa kuwa watu walifanya kazi kwa moyo wote.
7 Lorsque Sanballat, Tobia, les Arabes, les Ammonites et les gens d’Asdod apprirent que la restauration des murs de Jérusalem allait bon train, que les brèches commençaient à se fermer, ils en furent très dépités.
Lakini wakati Sanbalati, Tobia, Waarabu, Waamoni na watu wa Ashdodi waliposikia kuwa ukarabati wa kuta za Yerusalemu ulikuwa umeendelea na mianya ilikuwa inazibwa, walikasirika sana.
8 Ils complotèrent tous ensemble d’aller attaquer Jérusalem et d’y jeter le désarroi.
Wote walifanya shauri pamoja kuja kupigana dhidi ya Yerusalemu, na kuchochea machafuko dhidi yake.
9 Nous implorâmes notre Dieu et, pour nous défendre contre eux, nous établîmes un service de faction chargé de les surveiller jour et nuit.
Lakini tulimwomba Mungu wetu, na tukaweka ulinzi usiku na mchana kupambana na tishio hili.
10 Juda disait: "Les forces des porteurs de charges sont à bout et les décombres sont considérables; nous sommes hors d’état de rebâtir la muraille."
Wakati ule ule, watu wa Yuda wakasema, “Nguvu za wafanyakazi zinapungua, nacho kifusi ni kingi mno, kiasi kwamba hatuwezi kuujenga upya ukuta.”
11 Et nos adversaires disaient: "Ils ne se douteront ni ne s’apercevront de rien jusqu’à ce que nous pénétrions au milieu d’eux pour les massacrer, et ainsi nous mettrons fin à ce travail."
Pia adui zetu walisema, “Kabla hawajajua au kutuona, tutakuwa palepale katikati yao, na tutawaua na kuikomesha hiyo kazi.”
12 Comme des Judéens établis parmi eux vinrent nous dire jusqu’à dix fois: "De quelque localité que vous soyez, il faut que-vous retourniez chez nous",
Kisha Wayahudi ambao waliishi karibu nao walikuja zaidi ya mara kumi na kutuambia, “Popote mtakapoelekea, watatushambulia.”
13 je plaçai en contrebas, derrière la muraille, sur des terrains secs, je plaçai, dis-je, le peuple par familles, avec leurs épées, leurs lances et leurs arcs.
Kwa hiyo nikaweka baadhi ya watu nyuma ya sehemu za chini za ukuta kwenye sehemu zilizo wazi, nikawaweka kufuatana na jamaa zao, wakiwa na panga, mikuki na pinde zao.
14 Ayant tout inspecté, je m’avançai et dis aux grands, aux chefs et au reste du peuple: "N’Ayez pas peur d’eux; pensez au Seigneur grand et redoutable et combattez pour vos frères, vos fils et vos filles, vos femmes et vos maisons."
Baada ya kuona hali ilivyo, nikasimama na kuwaambia wakuu, maafisa na wengine wote, “Msiwaogope. Mkumbukeni Bwana, ambaye ni mkuu mwenye kuogofya. Piganeni kwa ajili ya ndugu zenu, wana wenu na binti zenu, wake zenu na nyumba zenu.”
15 Quand nos ennemis eurent été informés que nous étions avertis et que Dieu avait ruiné leur plan, nous retournâmes tous à la muraille, chacun à son ouvrage.
Adui zetu waliposikia kwamba tumetambua hila yao, na kwamba Mungu amevuruga shauri lao, sote tulirudi kwenye ukuta, kila mmoja kwenye kazi yake.
16 A partir de ce jour, la moitié de mes gens s’occupait de l’ouvrage, et l’autre moitié était munie de lances, de boucliers, d’arcs et de cuirasses; les seigneurs se tenaient derrière toute la maison de Juda.
Kuanzia siku ile na kuendelea, nusu ya watu wangu walifanya kazi ya ujenzi, na nusu nyingine wakashika mikuki, ngao, pinde na dirii. Maafisa walijipanga nyuma ya watu wote wa Yuda
17 De ceux qui étaient occupés à la bâtisse, d’une part les manœuvres, porteurs de charges, faisaient leur besogne d’une main et tenaient l’épée de l’autre;
waliokuwa wakijenga ukuta. Wale waliobeba vifaa vya ujenzi walifanya kazi yao kwa mkono mmoja, na kushika silaha kwa mkono mwingine,
18 d’autre part, les maçons construisaient, ayant chacun son épée attachée aux reins, et celui qui sonnait de la trompette était à mes côtés.
na kila mjenzi alijifunga upanga wake upande mmoja akiwa anafanya kazi. Lakini mtu wa kupiga baragumu alikaa pamoja nami.
19 Et je dis aux nobles, aux chefs et au reste du peuple: "L’Ouvrage est considérable et s’étend sur un vaste espace, de sorte que nous sommes dispersés le long de la muraille, éloignés l’un de l’autre.
Kisha nikawaambia wakuu, maafisa na watu wengine wote, “Kazi hii ni kubwa na imeenea sehemu kubwa, nasi tumetawanyika kila mmoja akiwa mbali na mwenzake juu ya ukuta.
20 A l’endroit d’où vous parviendra le son de la trompette, là vous viendrez vous rallier à nous: Dieu combattra en notre faveur."
Popote mtakaposikia sauti ya baragumu, jiungeni nasi huko. Mungu wetu atatupigania!”
21 C’Est ainsi que nous nous occupions de l’ouvrage, la moitié des gens tenant les lances depuis le lever de l’aurore jusqu’à l’apparition des étoiles.
Basi tuliendelea na kazi, nusu ya watu wakishikilia mikuki, kuanzia mawio ya jua hadi nyota zilipoonekana.
22 En ce temps-là aussi, je demandai au peuple que chacun passât la nuit à Jérusalem avec son serviteur, pour nous servir de sentinelles pendant la nuit et consacrer le jour au travail.
Wakati huo pia niliwaambia watu, “Kila mtu na msaidizi wake wakae ndani ya Yerusalemu wakati wa usiku, ili waweze kutumika kama walinzi wakati wa usiku, na kufanya kazi wakati wa mchana.”
23 Quant à moi, à mes frères, à mes gens et aux hommes de garde qui me suivaient, nous ne quittions point nos vêtements: chacun gardait son épée dans la main droite.
Mimi, wala ndugu zangu, wala watu wangu, wala walinzi waliokuwa pamoja nami hatukuvua nguo zetu. Kila mmoja alikuwa na silaha yake, hata alipokwenda kuchota maji.

< Néhémie 4 >