< Néhémie 1 >
1 Paroles de Néhémie, fils de Hakhalia: "Au mois de Kislev, dans la vingtième année, alors que je me trouvais à Suse, la capitale,
Maneno ya Nehemia mwana wa Hakalia: Katika mwezi wa Kisleu katika mwaka wa ishirini, wakati nilikuwa ngomeni katika jumba la kifalme la Shushani,
2 il advint que Hanâni, un de mes frères, avec quelques autres hommes, arriva de Judée. Je les interrogeai sur les Judéens, ce groupe de libérés qui avaient été soustraits à la captivité, et sur Jérusalem.
Hanani, mmoja wa ndugu zangu, alikuja kutoka Yuda akiwa na watu wengine, nami nikawauliza kuhusu mabaki ya Wayahudi wale walionusurika kwenda uhamishoni na pia kuhusu Yerusalemu.
3 Ils me répondirent "Ceux qui, échappés à la captivité, se sont fixés là-bas, dans la province, sont dans une situation très mauvaise et humiliante; les murs de Jérusalem gisent écroulés et ses portes sont consumées par le feu."
Wakaniambia, “Wale walionusurika kwenda uhamishoni, wale ambao wamerudi kwenye lile jimbo, wako katika taabu kubwa na aibu. Ukuta wa Yerusalemu umebomoka, na malango yake yamechomwa moto.”
4 Quand j’entendis ces paroles, je m’affaissai en pleurant, et je fus dans la désolation pendant des jours. Je jeûnai et me répandis en prières devant le Dieu du ciel:
Niliposikia mambo haya, niliketi, nikalia. Kwa siku kadhaa niliomboleza na kufunga na kuomba mbele za Mungu wa mbinguni.
5 "De grâce, ô Eternel, dis-je, Dieu du ciel, Dieu grand et redoutable, qui gardes fidèlement le pacte de bienveillance à ceux qui t’aiment et obéissent à tes lois,
Kisha nikasema: “Ee Bwana, Mungu wa mbinguni, mkuu na mwenye kuogofya, ambaye hulishika agano lake la upendo na wale wampendao na kutii amri zake,
6 que ton oreille soit attentive et tes yeux ouverts pour entendre la prière de ton serviteur, qu’à présent j’élève vers toi jour et nuit en faveur de tes serviteurs, les enfants d’Israël, en confessant les péchés des enfants d’Israël que nous avons commis à ton égard; oui, moi aussi et la maison de mon père, nous avons péché.
tega masikio yako, na ufungue macho yako, ili usikie maombi ya mtumishi wako anayoomba mbele yako usiku na mchana kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli. Ninaungama dhambi zetu sisi Waisraeli, pamoja na zangu na za nyumba ya baba yangu, tulizotenda dhidi yako.
7 Nous t’avons gravement offensé, et nous n’avons pas observé les lois, les préceptes et les statuts que tu as prescrits à ton serviteur Moïse.
Tumetenda uovu sana mbele zako. Hatukutii amri, maagizo na sheria ulizompa Mose mtumishi wako.
8 Souviens-toi donc de la déclaration dont tu as chargé Moïse, ton serviteur, à savoir: Si vous, vous devenez infidèles, moi, je vous disperserai parmi les nations.
“Kumbuka agizo ulilompa Mose mtumishi wako, ukisema, ‘Kama mkikosa uaminifu, nitawatawanya miongoni mwa mataifa,
9 Que si alors vous revenez à moi, si vous observez mes lois et les exécutez, dussent vos proscrits être relégués aux confins des cieux, de là je les rassemblerai pour les ramener à l’endroit que j’ai choisi pour en faire la résidence de mon nom."
lakini mkinirudia na kutii amri zangu, ndipo hata kama watu wenu walio uhamishoni wako mbali sana katika miisho ya dunia, nitawakusanya kutoka huko na kuwaleta mahali ambapo nimepachagua kuwa makao kwa ajili ya Jina langu.’
10 Or, ils sont tes serviteurs et ton peuple, que tu as délivrés par ta grande force et ta main puissante.
“Hawa ni watumishi wako na watu wako, uliowakomboa kwa nguvu zako kuu na mkono wako wenye nguvu.
11 Ah! Seigneur, que ton oreille soit donc attentive à la prière de ton serviteur ainsi qu’à la prière de tes serviteurs, qui aspirent à révérer ton nom. De grâce, fais réussir ton serviteur en ce jour et concilie-lui la bienveillance de cet homme!" Je servais alors d’échanson au roi.
Ee Bwana, tega sikio lako na usikie maombi ya huyu mtumishi wako, na maombi ya watumishi wako wanaofurahia kuliheshimu Jina lako. Nipe leo, mimi mtumishi wako, mafanikio kwa kunipa kibali mbele ya mtu huyu.” Kwa maana nilikuwa mnyweshaji wa mfalme.