< Malachie 2 >
1 Et maintenant, à vous cette injonction, ô pontifes!
“Sasa onyo hili ni kwa ajili yenu, enyi makuhani.
2 Si vous n’écoutez point, et si vous ne prenez pas à cœur de faire honneur à mon nom, dit l’Eternel-Cebaot, je déchaînerai contre vous la malédiction, et je maudirai les biens dont je vous ai bénis; oui, je les maudirai, car vous ne le prenez point à cœur!
Kama hamtasikiliza, na kama hamtaki kuielekeza mioyo yenu kuheshimu Jina langu, nitatuma laana juu yenu, nami nitalaani baraka zenu. Naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamkuielekeza mioyo yenu kuniheshimu mimi,” Asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
3 Voici je défendrai à la semence de germer pour vous, je vous répandrai des excréments sur la figure, les excréments de vos victimes, et comme eux on vous enlèvera.
“Kwa sababu yenu nitawakatilia mbali wazao wenu. Nitazipaka nyuso zenu mavi, mavi ya dhabihu zenu. Nanyi mtafukuzwa pamoja nazo mtoke mbele zangu.
4 Vous reconnaîtrez alors que je vous avais commis cette tâche, pour établir mon pacte avec Lévi, dit l’Eternel-Cebaot.
Nanyi mtajua kuwa nimewapelekea onyo hili ili kwamba Agano langu na Lawi lipate kuendelea,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
5 Mon pacte avec lui a été un gage de vie et de paix; je les lui ai accordées comme condition de son respect, et il m’a révéré et s’est humilié sous mon nom.
“Agano langu lilikuwa pamoja naye, agano la uhai na amani, nami nilimpa yote, ili aniche na kuniheshimu, naye akaniheshimu na kusimama akilicha Jina langu.
6 Une doctrine de vérité s’est rencontrée dans sa bouche, aucune iniquité ne s’est trouvée sur ses lèvres; il a cheminé devant moi en paix et en droiture, et beaucoup, par lui, sont revenus du crime.
Fundisho la kweli lilikuwa kinywani mwake, wala hakuna uongo wowote uliopatikana katika midomo yake. Alitembea nami katika amani na unyofu, naye akawageuza wengi kutoka dhambini.
7 C’Est que les lèvres du pontife doivent conserver la science; c’est de sa bouche qu’on réclame la doctrine, car il est un mandataire de l’Eternel-Cebaot.
“Kwa maana yapasa midomo ya kuhani kuhifadhi maarifa. Tena kutoka kinywani mwake watu wangepaswa kutafuta mafundisho, kwa sababu yeye ni mjumbe wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
8 Vous, au contraire, vous avez déserté le bon chemin, vous en avez fait trébucher beaucoup par votre enseignement, vous avez dissous le pacte avec Lévi, dit l’Eternel-Cebaot.
Lakini mmegeuka mkaiacha njia, na kwa mafundisho yenu mmesababisha wengi kujikwaa. Mmevunja agano na Lawi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
9 En revanche, je vous ai rendus, moi, vils et méprisables aux yeux de tout le peuple, puisque vous n’observez pas mes voies et que vous faites preuve de partialité dans l’application de la Loi.
“Kwa hiyo nimewasababisha ninyi kudharauliwa na kufedheheshwa mbele ya watu wote, kwa sababu hamkufuata njia zangu, bali mmeonyesha upendeleo katika mambo ya sheria.”
10 N’Avons-nous pas tous un seul père? N’Est-ce pas un seul Dieu qui nous a créés? Pourquoi commettrions-nous une trahison l’un contre l’autre, de façon à déshonorer l’alliance de nos pères?
Je, sote hatuna Baba mmoja? Hatukuumbwa na Mungu mmoja? Kwa nini basi tunalinajisi Agano la baba zetu kwa kukosa uaminifu kila mmoja kwa mwenzake?
11 Juda a trahi, une abomination s’est perpétrée en Israël et à Jérusalem; oui, Juda a profané ce qui est sacré devant l’Eternel, ce qui lui est cher; il a épousé la fille d’un dieu étranger.
Yuda amevunja uaminifu. Jambo la kuchukiza limetendeka katika Israeli na katika Yerusalemu: Yuda amepanajisi mahali patakatifu apendapo Bwana, kwa kuoa binti wa mungu mgeni.
12 Puisse le Seigneur, à celui qui agit de la sorte, supprimer des tentes de Jacob tout être veillant et parlant, capable de présenter des offrandes à l’Eternel-Cebaot!
Kwa maana kwa mtu yeyote atendaye jambo hili, Bwana na amkatilie mbali kutoka hema za Yakobo, hata kama huwa anamletea Bwana Mwenye Nguvu Zote sadaka.
13 Et voici un autre méfait de votre part: vous êtes cause que l’autel du Seigneur est couvert de larmes, de pleurs et de sanglots, si bien que Dieu ne peut plus se complaire à vos offrandes ni accepter de présent de votre main.
Kitu kingine mnachokifanya: Mnaifurikisha madhabahu ya Bwana kwa machozi. Mnalia na kuugua kwa sababu yeye haziangalii tena sadaka zenu wala hazikubali kwa furaha kutoka mikononi mwenu.
14 Et vous dites: "Pourquoi cela? Parce que l’Eternel est témoin entre toi et la femme de ta jeunesse, que tu as trahie, elle qui est ta compagne, la femme unie à toi par un pacte.
Mnauliza, “Kwa nini?” Ni kwa sababu Bwana ni shahidi kati yako na mke wa ujana wako, kwa sababu umevunja uaminifu naye, ingawa yeye ni mwenzako, mke wa agano lako la ndoa.
15 Pas un ne l’eût fait, s’il lui restait quelque ombre de bon sens. Et que devrait-il souhaiter, même celui-là, si ce n’est une progéniture agréable à Dieu? Veillez donc sur vous-mêmes, et que personne ne trahisse la femme de sa jeunesse!
Je, Bwana hakuwafanya wao kuwa mmoja? Katika mwili na katika roho wao ni wa Mungu. Kwa nini wawe mmoja? Kwa sababu Mungu alikuwa akitafuta mzao mwenye kumcha Mungu. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, mtu asivunje uaminifu kwa mke wa ujana wake.
16 Car je hais la répudiation, dit l’Eternel, Dieu d’Israël, et celui qui couvre son vêtement de violence, dit l’Eternel-Cebaot. Surveillez donc vos sentiments et ne commettez pas de trahison!
“Ninachukia kuachana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli, “pia nachukia mtu anayejivika jeuri kama vazi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, wala msije mkavunja uaminifu.
17 Vous excédez l’Eternel par vos discours, et vous demandez: "En quoi t’excédons-nous? Parce que vous dites: "Tous ceux qui font le mal sont bien vus aux yeux de l’Eternel, et ce sont eux qui sont ses favoris!" ou bien encore: "Où est donc le Dieu du bon droit?"
Mmemchosha Bwana kwa maneno yenu. Nanyi mnauliza, “Tumemchosha kwa namna gani?” Mmemchosha kwa kusema, “Wote watendao mabaya ni wema machoni pa Bwana, naye anapendezwa nao” au “Mungu wa haki yuko wapi?”