< Juges 18 >

1 En ce temps-là, Israël n’avait point de roi; et en ce même temps, la tribu des Danites se mettait en quête d’une possession pour s’y établir, car jusque-là elle n’avait pas obtenu en partage un territoire, comme les autres tribus d’Israël.
Katika siku hizo Israeli walikuwa hawana mfalme. Katika siku hizo kabila la Wadani walikuwa wanatafuta mahali pao wenyewe pa kuishi, kwa sababu walikuwa hawajafika kwenye urithi wao miongoni mwa makabila ya Israeli.
2 Les Danites choisirent donc parmi eux cinq hommes de leur famille, hommes résolus, et les envoyèrent de Çorea et d’Echtaol pour parcourir et explorer le pays, en leur disant: "Allez, explorez le pays." Ceux-ci arrivèrent dans la montagne d’Ephraïm, près de la maison de Micah, et y passèrent la nuit.
Hivyo Wadani wakatuma mashujaa watano kutoka Sora na Eshtaoli ili kupeleleza nchi na kuichunguza. Hawa watu waliwakilisha koo zao zote. Waliwaambia, “Nendeni mkaichunguze hiyo nchi.” Watu hao wakaingia katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao wakafika nyumba ya Mika, ambako walilala usiku huo.
3 Etant près de cette maison, ils reconnurent la voix du jeune lévite, le joignirent et lui dirent: "Qui t’a fait venir ici? que fais-tu céans, et qu’y possèdes-tu?"
Walipofika karibu na nyumba ya Mika, waliitambua sauti ya yule kijana Mlawi; hivyo wakaingia humo na kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta hapa? Unafanya nini mahali hapa? Kwa nini uko hapa?”
4 Il leur répondit: "Micah a fait pour moi telle et telle chose; il m’a engagé moyennant salaire, et je suis devenu son prêtre."
Akawaeleza yale Mika aliyomtendea, naye akasema, “Ameniajiri nami ni kuhani wake.”
5 "De grâce, lui dirent-ils, consulte Dieu pour que nous sachions si l’entreprise que nous tentons réussira."
Kisha wakamwambia, “Tafadhali tuulizie kwa Mungu kama safari yetu itafanikiwa.”
6 "Allez en paix, leur répondit le prêtre; l’Eternel voit d’un bon œil le voyage que vous faites."
Yule kuhani akawajibu, “Enendeni kwa amani. Safari yenu ina kibali cha Bwana.”
7 Les cinq hommes se remirent en route et atteignirent Laïs. Ils virent que le peuple habitant cette ville vivait en sécurité à la manière des Sidoniens, paisible et confiant; que rien ne ferait obstacle, dans le pays, à qui s’emparerait du pouvoir; qu’ils étaient loin des Sidoniens et sans rapports avec personne.
Basi hao watu watano wakaondoka na kufika Laishi, mahali ambapo waliwakuta watu wanaishi salama, kama Wasidoni, kwa utulivu na bila mashaka. Nchi yao haikupungukiwa na kitu chochote, hivyo wakawa tajiri. Pia walikaa mbali sana na Wasidoni, wala hawakushughulika na mtu yeyote.
8 Et de retour chez leurs frères, à Çorea et à Echtaol, quand ceux-ci leur dirent: "Que savez-vous?"
Waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli, ndugu zao wakawauliza, “Mlionaje mambo huko?”
9 ils répondirent: "Venez et marchons contre eux! Nous avons observé ce pays, il est excellent, et vous restez inactifs! N’Hésitez pas à vous mettre en marche, allez conquérir ce pays!
Wakajibu, “Twendeni, tukapigane nao! Tumeona kuwa nchi ni nzuri sana. Je, hamtafanya chochote? Msisite kupanda ili kuimiliki.
10 En y arrivant, vous arriverez chez un peuple plein de sécurité, dans un territoire spacieux, dont Dieu vous fait maîtres; une contrée où rien ne manque de ce que peut produire la terre."
Mtakapokwenda huko mtakuta watu waliotulia walio salama, nayo nchi hiyo ni kubwa na Mungu ameitia mikononi mwenu, nayo ni nchi ambayo haikupungukiwa na kitu chochote kilicho duniani.”
11 Aussitôt partirent de là, de Çorea et d’Echtaol, six cents hommes de la famille des Danites, armés en guerre.
Ndipo watu 600 toka ukoo wa Wadani, waliojifunga silaha za vita, wakaondoka Sora na Eshtaoli.
12 Puis, avançant, ils campèrent près de Kiryath-Yearim en Juda; c’est pourquoi ce lieu, situé derrière Kiryath-Yearim, s’appelle aujourd’hui encore Mahané-Dan.
Walipokuwa wakisafiri wakapiga kambi huko Kiriath-Yearimu katika Yuda. Hii ndiyo sababu sehemu ya magharibi ya Kiriath-Yearimu inaitwa Mahane-Dani mpaka leo.
13 De là ils se dirigèrent vers la montagne d’Ephraïm, et arrivèrent jusqu’à la maison de Micah.
Kutoka hapo wakaendelea mbele mpaka nchi ya vilima ya Efraimu na kufika katika nyumba ya Mika.
14 Les cinq hommes qui étaient allés explorer le pays jusqu’à Laïs prirent la parole, et dirent à leurs frères: "Savez-vous qu’il y a, dans une de ces maisons, un éphod, des pénates et une image taillée avec métal? Avisez maintenant à ce que vous devez faire."
Ndipo wale watu watano waliopeleleza nchi ya Laishi wakawaambia ndugu zao, “Je, mwajua kuwa mojawapo ya nyumba hizi kuna naivera, sanamu ndogo za nyumbani, sanamu ya kuchonga na sanamu ya kusubu? Sasa basi fikirini mtakalofanya.”
15 Ils se rendirent alors chez le jeune lévite, dans la demeure de Micah, et s’informèrent de son bien-être.
Basi wakaingia humo na kwenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi katika nyumba ya Mika na kumsalimu.
16 Tandis que les six cents hommes de la tribu de Dan, ceints de leurs armes, se tenaient au seuil de la porte,
Wale Wadani 600, waliovaa silaha za vita, wakasimama penye ingilio la lango.
17 les cinq autres, les explorateurs du pays, pénétrèrent dans l’intérieur et enlevèrent l’idole, l’éphod, les pénates et la garniture métallique; le prêtre était arrêté au seuil de la porte, avec les six cents hommes armés,
Wale watu watano waliokwenda kupeleleza nchi wakaingia ndani na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani pamoja na ile sanamu ya kusubu, wakati yule kuhani akiwa amesimama pale penye ingilio la lango pamoja na wale watu 600 waliokuwa wamejifunga silaha za vita.
18 tandis que les autres entraient chez Micah et s’emparaient de l’idole jointe à l’éphod, des pénates et du métal. Et le prêtre leur dit: "Que faites-vous?"
Hao watu walipoingia katika nyumba ya Mika na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, pamoja na ile sanamu ya kusubu, yule kuhani akawauliza, “Mnafanya nini?”
19 "Tais-toi! répondirent-ils, retiens ta langue et viens avec nous pour nous servir de père et de prêtre. Lequel vaut mieux, que tu desserves la maison d’un particulier, ou bien une famille et une tribu d’Israël?"
Wakamjibu, “Nyamaza kimya! Weka mkono wako juu ya kinywa chako na ufuatane nasi, uwe baba yetu na kuhani wetu. Si ni afadhali utumikie kabila na ukoo katika Israeli kama kuhani kuliko kumtumikia mtu mmoja na watu wa nyumbani mwake?”
20 Le prêtre en fut charmé dans son cœur; il prit éphod, pénates et idole, et entra dans les rangs de cette troupe.
Yule kuhani akafurahi. Akachukua ile naivera, zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, na sanamu ya kuchonga, naye akaenda pamoja na wale watu.
21 Alors ils se remirent en voyage, en faisant prendre les devants à la population faible, aux bestiaux et aux bagages.
Ndipo wakageuka na kuondoka wakiwatanguliza mbele watoto wao wadogo, wanyama wao wa kufugwa na mali zao.
22 Ils étaient déjà loin de la maison de Micah, lorsque les habitants des maisons qui avoisinaient celle de Micah s’ameutèrent, et se mirent à la poursuite des enfants de Dan.
Walipokuwa wamesafiri umbali kidogo toka nyumbani kwa Mika, watu walioishi karibu na Mika wakaitwa wakakusanyika pamoja, nao wakawafikia Wadani.
23 Comme ils criaient après eux, ceux-ci se retournèrent et dirent à Micah: "Qu’as-tu donc, pour te mettre ainsi en campagne?"
Walipofuatilia wakipiga kelele Wadani wakawageukia na kumwambia Mika, “Una nini wewe hata ukaja na kundi la watu namna hii ili kupigana?”
24 Il répondit: "Vous avez emporté les dieux que je m’étais faits, vous avez emmené mon prêtre, il ne me reste plus rien, et vous me demandez ce que j’ai!"
Akawajibu, “Mmechukua miungu yote niliyoitengeneza, mkachukua na kuhani wangu, nanyi mkaondoka. Nimebaki na nini kingine? Mnawezaje kuniuliza, ‘Una nini wewe?’”
25 Les Danites lui répliquèrent: "Ne nous obsède pas de tes plaintes; car quelques-uns, d’un caractère aigri, pourraient se jeter sur vous, et tu causerais ta perte et celle de ta famille."
Wadani wakamjibu, “Usibishane na sisi, la sivyo watu wenye hasira kali watakushambulia, nawe na watu wa nyumbani mwako mtapoteza maisha.”
26 Les Danites poursuivirent leur marche, tandis que Micah, voyant qu’ils étaient les plus forts, changeait de direction et rentrait chez lui.
Basi Wadani wakaenda zao, naye Mika alipoona kuwa wana nguvu kumliko yeye, akageuka na kurudi nyumbani kwake.
27 Pour eux, ils gardèrent et les objets qu’avait faits Micah et le prêtre qu’il avait eu; ils tombèrent sur Laïs, sur une population paisible et confiante, la passèrent au fil de l’épée et mirent le feu à la ville.
Kisha wakachukua vile Mika alivyokuwa ametengeneza, na kuhani wake, wakaendelea hadi Laishi, dhidi ya watu walio na amani, wasiokuwa na wasiwasi. Wakawashambulia kwa upanga na kuuteketeza mji wao kwa moto.
28 Nul ne la secourut, car elle était éloignée de Sidon et n’avait de relations avec personne; elle était située dans la vallée attenante à Beth-Rehob. Puis ils rebâtirent cette ville, s’y établirent,
Hapakuwa na yeyote wa kuwaokoa, kwa kuwa kulikuwa mbali sana na Sidoni na hawakuwa na ushirikiano na mtu mwingine yeyote. Mji ulikuwa kwenye bonde karibu na Beth-Rehobu. Wadani wakaujenga upya huo mji na kuishi humo.
29 et la nommèrent Dan, du nom de Dan leur père, l’un des fils d’Israël; mais la ville, antérieurement, avait nom Laïs.
Wakauita ule mji Dani kwa kufuata jina la baba yao aliyezaliwa na Israeli, ingawa mji huo ulikuwa ukiitwa Laishi hapo kwanza.
30 Les enfants de Dan érigèrent l’idole à leur usage; et Jonathan, fils de Gersom, fils de Manassé, ainsi que ses descendants, servirent de prêtres à cette tribu jusqu’au jour où elle fut exilée du pays.
Kisha Wadani wakajisimamishia sanamu ile ya kuchonga, naye Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Mose pamoja na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka nchi hiyo ilipotekwa.
31 Ils conservèrent donc l’idole fabriquée par Micah, tout le temps que la maison de Dieu resta à Silo.
Wakaisimamisha na kuiabudu hiyo sanamu ya kuchonga ya Mika aliyokuwa ameitengeneza, wakati wote ule nyumba ya Mungu ilipokuwa huko Shilo.

< Juges 18 >