< Josué 3 >
1 Donc, de bon matin, Josué et tous les enfants d’Israël partirent de Chittîm et s’avancèrent jusqu’auprès du Jourdain; là ils passèrent la nuit avant d’effectuer le passage.
Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka.
2 Au bout de trois jours, les préposés parcoururent le camp
Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote,
3 et donnèrent cet ordre au peuple: "Quand vous verrez paraître l’arche d’alliance de l’Eternel, votre Dieu, portée par les prêtres, descendants de Lévi, vous quitterez votre emplacement et vous la suivrez;
wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata.
4 toutefois, vous maintiendrez entre elle et vous une distance de deux mille coudées environ; n’en approchez pas, de façon à connaître la route que vous devez suivre, car jamais encore vous n’avez fait ce trajet."
Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,000 kati yenu na Sanduku.”
5 Et Josué dit au peuple: "Sanctifiez-vous! Car, demain, l’Eternel accomplira au milieu de vous des merveilles."
Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”
6 Puis Josué dit aux prêtres: "Portez l’arche d’alliance et marchez en tête du peuple." Et ils portèrent l’arche d’alliance, et s’avancèrent en tête du peuple.
Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.
7 Et Dieu dit à Josué: "Dès aujourd’hui, je commencerai à te grandir aux yeux de tout Israël; je veux qu’ils sachent que, comme j’ai été avec Moïse, je serai avec toi.
Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose.
8 De ton côté, tu donneras cet ordre aux prêtres, chargés de porter l’arche d’alliance: "Quand vous aurez atteint les eaux qui baignent la rive du Jourdain, vous ferez halte dans le fleuve."
Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’”
9 Et Josué dit aux enfants d’Israël: "Approchez, et écoutez les paroles de l’Eternel, votre Dieu."
Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu.
10 Et il ajouta: "Voici qui vous prouvera que le Dieu vivant est au milieu de vous, et qu’il saura chasser de devant vous le Cananéen, le Héthéen, le Hévéen, le Phérizéen, le Ghirgachéen, l’Amorréen et le Jébuséen:
Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi.
11 voyez, l’arche d’alliance du Maître de toute la terre va, à votre tête, traverser le Jourdain.
Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia.
12 Et maintenant, vous allez choisir douze hommes parmi les tribus d’Israël, un homme par tribu.
Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila.
13 Aussitôt que les prêtres, portant l’arche de l’Eternel, Maître de toute la terre, poseront la plante de leurs pieds dans les eaux du Jourdain, les eaux du fleuve celles qui coulent en amont s’arrêteront net, et resteront droites comme un mur."
Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”
14 Ainsi arriva-t-il. Le peuple quitta ses tentes pour passer le Jourdain, et les prêtres porteurs de l’arche d’alliance marchaient en avant.
Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia.
15 Arrivés au Jourdain, sitôt que les prêtres porteurs de l’arche eurent trempé leurs pieds dans ses eaux, lesquelles couvraient toutes ses rives à cette époque de la moisson,
Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji,
16 les eaux d’amont s’arrêtèrent et formèrent comme un mur, à une grande distance, depuis Adâm, la ville voisine de Caretân, tandis que les eaux d’aval, dans la direction de la mer du Désert ou mer de Sel, achevaient de s’écouler; et le peuple effectua son passage en face de Jéricho.
maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.
17 Les prêtres, porteurs de l’arche d’alliance de l’Eternel, restèrent à pied sec au milieu du Jourdain, immobiles, pendant que tout Israël passait à pied sec, jusqu’à ce que la nation entière eût achevé de traverser le Jourdain.
Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.