< Josué 19 >

1 Le deuxième lot échut à Siméon, à la tribu des Siméonites selon leurs familles: ils eurent leur possession au milieu de celle des enfants de Juda.
Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
2 II leur échut comme possession: Bersabée, Chéba, Molada;
Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
3 Haçar-Choual, Bala, Ecem;
Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
4 Eltolad, Betoul, Horma;
Eltoladi, Bethuli, Horma,
5 Ciklag, Beth-Marcabot, Haçar-Souça;
Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
6 Beth-Lebaot et Charouhén: treize villes, avec leurs bourgades.
Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
7 Plus Ayîn-Rimmôn, Eter et Achân: quatre villes, avec leurs bourgades;
Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
8 et toutes les campagnes aux environs de ces villes, jusqu’à Baalat-Beér et Ramat-Négheb. Tel fut l’héritage de la tribu des Siméonites, selon leurs familles.
pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
9 C’Est sur la part mesurée aux descendants de Juda que fut pris l’héritage de ceux de Siméon; car la part des enfants de Juda était trop grande pour eux, de sorte que ceux de Siméon eurent leur héritage au milieu du leur.
Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
10 Le troisième lot échut aux enfants de Zabulon, selon leurs familles. La frontière de leur possession s’étendait jusqu’à Sarid.
Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
11 De là, elle montait à l’occident vers Mareala, touchait Dabbéchet et le torrent qui passe devant Yokneam;
Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
12 revenait de Sarid, vers l’orient, dans la direction du soleil levant, à la limite de Kislot-Thabor, ressortait vers Daberat et montait à Yaphïa;
Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
13 de là, elle passait à l’orient, vers Gat-Héfer, vers Et-Kacîn, aboutissait à Rimmôn-Metoar, à Néa,
Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
14 qu’elle contournait, par le nord, vers Hanatôn; et elle finissait la vallée de Yiftah-El.
Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
15 Plus, Kattat, Nahalal, Chimrôn, Yideala et Beth-Léhem: douze villes, avec leurs bourgades.
Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
16 Telle fut la possession des enfants de ZabuIon selon leurs familles, comprenant ces villes avec leurs bourgades.
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
17 C’Est à Issachar qu’échut le quatrième lot, aux enfants d’lssachar, selon leurs familles.
Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
18 Leur territoire comprenait: Jezreêl, Keçoullot, Chounêm;
Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
19 Hafaraïm, Chiôn, Anaharat,
Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
20 Rabbith, Kichyôn, Ebeç;
Rabithi, Kishioni, Ebesi,
21 Rémet, En-Gannim, En-Hadda, Beth-Paçêç;
Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
22 englobait encore Thabor, Chahacîm, Beth-Chémech, et avait pour limite le Jourdain: seize villes, ainsi que leurs bourgades.
Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 Telle fut la possession de la tribu d’lssachar, selon ses familles, telles les villes et leurs bourgades.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
24 Le cinquième lot échut à la tribu d’Aser, selon ses familles.
Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
25 Leur frontière comprenait: Helkat, Hall, Béten, Akhchaf;
Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
26 Allamélec, Amead, Micheal; atteignait le Carmel à l’ouest, ainsi que Chihor-Libnat;
Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
27 tournait à l’orient vers Beth-Dagôn, rencontrait Zabulon, la vallée de Yiftah-El au nord, Beth-Emek, Neïel; se dirigeait à gauche vers Caboul,
Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
28 Ebrôn, Rehob, Ham-môn, Kana, jusqu’à Sidon la Grande;
Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
29 de là elle passait à Rama, puis à la ville du Fort-de-Tyr; de là à Hossa, et elle se terminait à la mer par le canton d’Akhzib.
Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
30 De plus, Oumma, Aphek, Rehob: vingt-deux villes, avec leurs bourgades.
Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
31 Telle fut la possession de la tribu d’Aser, selon ses familles, telles les villes et leurs bourgades.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
32 Aux enfants de Nephtali échut le sixième lot, aux enfants de Nephtali selon leurs familles.
Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
33 Leur frontière allait de Hélef, du Chêne de Çaanannîm, par Adami-Hannékeb et Yabneêl, jusqu’à Lakkoum, et aboutissait au Jourdain;
Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
34 revenait à l’occident par Aznot-Thabor, passait de là à Houkkok, touchait Zabulon au midi, Aser à l’occident, et Juda, vers le Jourdain, à l’orient.
Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
35 Les villes fortes étaient: Ciddîm, Cêr, Hammat, Rakkat, Kinnéreth;
Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
36 Adam, Rama, Haçor;
Adama, Rama, Hazori,
37 Kédech, Edréi, En-Haçor;
Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
38 Yireôn, Migdal-El, Horem, Beth-Anat, Beth-Chémech: dix-neuf villes, avec leurs bourgades.
Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
39 Telle fut la possession de la tribu de Nephtali, selon ses familles, les villes et leurs bourgades.
Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
40 A la tribu de Dan, selon ses familles, échut le septième lot.
Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
41 La frontière de leur possession comprenait: Çorea, Echtaol, Ir-Chémech;
Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
42 Chaalabbîn, Ayyalôn, Yitla;
Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
43 Elôn, Timnatha, Ekron;
Eloni, Timna, Ekroni,
44 Elteké, Ghibetôn, Baalat;
Elteke, Gibethoni, Baalathi,
45 Yehoud, Bené-Berak, Gat-Rimmôn;
Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
46 Mê-Yarkôn et Rakkôn, avec le territoire devant Yapho.
Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
47 Mais le territoire des enfants de Dan dépassa ces limites: en effet, les enfants de Dan firent une expédition, attaquèrent Léchem, s’en emparèrent, la passèrent au fil de l’épée, en prirent possession et s’y établirent, remplaçant le nom de Léchem par celui de Dan, qui était le nom de leur père.
(Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
48 Telle fut la possession de la tribu de Dan, selon ses familles, telles les villes et leurs bourgades.
Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
49 Lorsqu’ils eurent achevé de partager le pays selon ses limites, les enfants d’Israël attribuèrent à Josué, fils de Noun, une possession au milieu d’eux.
Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
50 Sur l’ordre de l’Eternel, ils lui donnèrent la ville qu’il avait demandée: Timnat-Sérah, dans la montagne d’Ephraïm. II restaura cette ville et il s’y établit.
kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
51 Telles sont les possessions que le prêtre Eléazar, Josué, fils de Noun, et les chefs de famille des tribus des enfants d’Israël répartirent, par la voie du sort, à Silo, en présence de l’éternel, à l’entrée de la Tente d’assignation: on acheva ainsi le partage du pays.
Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.

< Josué 19 >