< Josué 18 >
1 Toute la communauté des enfants d’Israël s’assembla à Silo et y installa la Tente d’assignation; le pays était conquis et à leur disposition.
Kusanyiko lote la Waisraeli likakusanyika huko Shilo na kusimamisha Hema la Kukutania. Nchi ikawa chini ya utawala wao,
2 Mais il restait, parmi les enfants d’Israël, sept tribus à qui on n’avait pas encore départi leur patrimoine.
lakini palikuwa bado makabila saba ya Israeli ambayo yalikuwa hayajapokea urithi wao.
3 Josué dit à ces Israélites: "Combien de temps encore négligerez-vous de prendre possession du pays que vous a donné l’Eternel, le Dieu de vos pères?
Hivyo Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtasubiri hata lini ili kuingia kumiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa?
4 Désignez vous-mêmes trois hommes par tribu, afin que je leur donne mission de parcourir le pays et d’en faire le plan selon les possessions à attribuer; après quoi, ils viendront me trouver.
Chagueni watu watatu kutoka kwenye kila kabila. Nitawatuma hao watu kukagua hiyo nchi na kuniandikia mapendekezo ya mgawanyo wa urithi wa kila kabila. Nao watanirudia.
5 Ils le diviseront en sept parts, Juda devant conserver sa frontière au midi, et la maison de Joseph devant garder la sienne au nord.
Mtaigawanya hiyo nchi katika sehemu saba. Yuda atabaki katika eneo lake upande wa kusini na nyumba ya Yosefu katika nchi yake upande wa kaskazini.
6 Vous ferez donc délimiter le pays en sept parts et m’apporterez le plan ici, où je les tirerai pour vous au sort devant l’Eternel, notre Dieu.
Baada ya kuandika maelezo ya hizo sehemu saba za nchi, yaleteni kwangu, nami nitawapigia kura kwa kura mbele za Bwana Mungu wetu.
7 Car, pour ce qui est des Lévites, ils n’ont point de part au milieu de vous, le ministère de l’Eternel étant leur apanage; quant à Gad, à Ruben et à la demi-tribu de Manassé, ils ont reçu leur patrimoine sur la rive orientale du Jourdain, telle que Moïse, serviteur de l’Eternel, le leur a attribué."
Hata hivyo, Walawi hawatakuwa na sehemu miongoni mwenu, kwa maana huduma ya ukuhani kwa Bwana ndio urithi wao. Nao Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapata urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, ambako Mose mtumishi wa Bwana aliwapa.”
8 Les délégués se disposant à partir pour lever le plan du pays, Josué leur donna cet ordre: "Allez, parcourez le pays, faites-en le plan et revenez auprès de moi, afin qu’ici, à Silo, je vous le répartisse au sort, en présence de l’Eternel."
Watu hao walipokuwa wanaondoka kwenda kuandika vizuri kuhusu hiyo nchi, Yoshua akawaagiza, “Nendeni mkakague hiyo nchi na mwandike maelezo kuihusu. Kisha mrudi kwangu, nami nitawapigia kura hapa Shilo mbele za Bwana.”
9 Les hommes partirent, traversèrent le pays, en dressèrent le plan par villes, en sept parties, sur un registre, et vinrent trouver Josué au camp, à Silo.
Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo.
10 Et Josué jeta le sort à Silo, devant l’Eternel, et il y répartit le pays entre les enfants d’Israël, selon leurs groupements.
Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele za Bwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.
11 Le premier lot échut à la tribu des enfants de Benjamin, selon leurs familles; les confins que leur attribua le sort se trouvaient entre les enfants de Juda et ceux de Joseph.
Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.
12 Leur limite, du côté du nord, partait du Jourdain, montait au côté nord de Jéricho, passait à l’ouest de la montagne, et aboutissait au désert de Beth-Avén.
Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni.
13 De là, elle gagnait le côté méridional de Louz, nommée aussi Béthel, et descendait vers Atrot-Addar, sur la montagne qui est au sud de Bethorôn-le-Bas.
Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.
14 Puis elle s’infléchissait et tournait du côté de l’ouest, au midi de la montagne qui fait face à Bethorôn, et se terminait à Kiryath-Baal ou Kiryath-Yearîm, ville de la tribu de Juda: voilà pour le côté occidental.
Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.
15 Le côté du midi partait de l’extrémité de Kiryath-Yearîm, et continuait dans la direction de la mer et atteignait la source de Mê-Nephtoah;
Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa.
16 puis la limite descendait à l’extrémité de la montagne faisant face à la vallée de Ben Hinnom, qui est au côté nord de la vallée des Rephaïm; suivait la vallée de Hinnom jusqu’au côté sud de Jébus et atteignait En-Roghel;
Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli.
17 tournait au nord vers En-Chémech, de là vers Gheliloth, en face de la montée d’Adoummim, et descendait vers la Pierre de Bohân-ben-Ruben;
Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni.
18 se poursuivait vers le côté nord de la Plaine, et atteignait Araba;
Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba.
19 de là, elle passait au côté nord de Beth-Hogla, et aboutissait à la pointe nord de la mer Salée, à l’extrémité sud du Jourdain: telle était la frontière méridionale.
Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.
20 Et le Jourdain formait la limite du côté de l’orient. Telle fut, dans tout son circuit, la possession des enfants de Benjamin selon leurs familles.
Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki. Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.
21 Les villes de cette tribu, réparties entre ses familles, étaient: Jéricho, Beth-Hogla, Emek-Keçis;
Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo: Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi,
22 Beth-Haaraba, Cemaraïm, Béthel;
Beth-Araba, Semaraimu, Betheli,
24 Kefar-Ammona, Ofni et Ghéba: douze villes, avec leurs bourgades.
Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
25 Plus Gabaon, Rama, Beërot;
Gibeoni, Rama na Beerothi,
27 Rékem, Yirpeël, Tareala;
Rekemu, Irpeeli, Tarala,
28 Cèla, Elef, Jébus, la même que Jérusalem, Ghibeath, Kiryath: quatorze villes, avec leurs bourgades. Tel fut le patrimoine des descendants de Benjamin, selon leurs familles.
Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake. Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.