< Josué 13 >

1 Or, Josué étant vieux, avancé en âge, l’Eternel lui dit: "Te voilà vieux, avancé en âge, et il reste encore une très grande partie du pays à conquérir.
Yoshua alipokuwa mzee na umri wake ukiwa umesogea sana, Bwana akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado kumesalia sehemu kubwa sana za nchi ambazo ni za kutwaliwa.
2 Voici ce qui reste à prendre: tous les districts des Philistins, et tout le canton de Guechour;
“Nchi iliyosalia ni hii: maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:
3 depuis Chihor, qui baigne l’Egypte, jusqu’au territoire d’Ekron au nord, qui est compté comme cananéen; les cinq principautés philistines de Gaza, d’Asdôd, d’Ascalon, de Gath et d’Ekron, et les Avéens;
kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani (maeneo yale matano ya watawala wa Kifilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni: ndiyo nchi ya Waavi);
4 en partant du midi: tout le pays des Cananéens, et Meara, qui est aux Sidoniens, jusqu’à Aphek, jusqu’à la frontière des Amorréens;
kuanzia kusini, nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,
5 la province des Ghiblites, toute la partie orientale du Liban, depuis Baal-Gad, au pied du mont Hermon, jusque vers Hamath;
eneo la Wagebali; Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
6 tout ce que possédaient les montagnards, du Liban jusqu’à Misrefot-Maïm, tout ce qui est aux Sidoniens: je les en déposséderai pour les enfants d’Israël. En attendant, lotis ce pays entre les Israélites, ainsi que je te l’ai ordonné.
“Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza watoke mbele ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,
7 Maintenant, tu as à le répartir comme possession entre les neuf tribus et la moitié de la tribu de Manassé."
sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”
8 Les Rubénites et les Gadites avaient, avec l’autre moitié, pris possession de l’héritage que Moïse leur avait donné du côté oriental du Jourdain, tel que Moïse, serviteur de Dieu, le leur avait attribué:
Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Mose aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Bwana alivyowagawia.
9 depuis Aroêr, située au bord du torrent d’Arnon, avec la ville qui est dans le bas-fond, et toute la plaine de Mêdeba jusqu’à Dibôn;
Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyoko ukingoni mwa Bonde la Arnoni kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba mpaka Diboni,
10 toutes les villes de Sihôn, roi des Amorréens, qui avait régné à Hesbon, jusqu’à la frontière des Ammonites;
nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.
11 le Galaad, le territoire de Guechour et de Maakha, toute la montagne de Hermon et tout le Basan jusqu’à Salka,
Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:
12 formant le royaume d’Og dans le Basan, lequel régnait à Astarot et à Edréi et était resté des derniers Rephaïm. Moïse avait vaincu et dépossédé ces deux rois.
yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Mose alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.
13 Toutefois, les Israélites ne dépossédèrent point les habitants de Guechour, ni ceux de Maakha, lesquels sont restés au milieu d’Israël jusqu’à ce jour.
Lakini Waisraeli hawakuwafukuza watu wa Geshuri na wa Maaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo hii.
14 A la seule tribu de Lévi l’on n’assigna pas de patrimoine: les sacrifices de l’Eternel, Dieu d’Israël, constituèrent son patrimoine, comme il le lui avait déclaré.
Lakini kwa kabila la Lawi, Mose hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Bwana, Mungu wa Israeli, ndizo zilizokuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.
15 Moïse donna donc sa part à la tribu des Rubénites, selon leurs familles.
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Reubeni ukoo kwa ukoo:
16 Et ils eurent pour territoire: Aroêr, au bord du torrent d’Arnon; la ville qui est dans le bas-fond, et toute la plaine vers Mêdeba;
Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba
17 Hesbon avec toutes ses bourgades qui sont dans la plaine: Dibôn, Bamoth-Baal, Beth-Baal Meôn;
hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,
18 Yahça, Kedêmoth, Méphaath;
Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,
19 Kiryathaïm, Sibma et Céreth-Hachahar sur le mont de la vallée;
Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,
20 Beth-Peor, les versants du Pisga, Beth-Hayechimoth,
Beth-Peori, materemko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:
21 enfin, toutes les villes de la plaine, tout le royaume de Sihôn, roi des Amorréens, qui avait régné à Hesbon et que Moïse avait battu, ainsi que les princes de Madian: Evi, Rékem Çour, Hour et Réba, vassaux de Sihôn occupant ce pays,
miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Mose alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.
22 et aussi Balaam, fils de Beor, le magicien, que les enfants d’Israël avaient fait périr, avec leurs autres victimes, par le glaive.
Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mchawi.
23 Le territoire des enfants de Ruben avait le Jourdain pour limite. Tel fut l’héritage des enfants de Ruben selon leurs familles, telles les villes et leurs dépendances.
Mpaka wa Wareubeni ulikuwa ni ukingo wa Mto Yordani. Miji hii na vijiji vyake ndiyo iliyokuwa urithi wa Wareubeni ukoo kwa ukoo.
24 Moïse donna aussi sa part à la tribu de Gad, aux enfants de Gad selon leurs familles,
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
25 et ils eurent pour territoire: Yazer et toutes les villes du Galaad, et la moitié du pays des Ammonites, jusqu’à Aroêr qui est en face de Rabba;
Nchi ya Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Amoni iliyoenea hadi Aroeri, karibu na Raba;
26 et depuis Hesbon jusqu’à Ramath-Miçpé et Betonim, et depuis Mahanaïm jusqu’à la frontière de Debir;
na kuanzia Heshboni mpaka Ramath-Mispa na Betonimu, na kutoka Mahanaimu hadi eneo la Debiri;
27 dans la vallée: Beth-Harâm, Beth-Nimra, Souccoth et Çaphôn, formant le surplus du royaume de Sihôn, roi de Hesbon, avec le Jourdain pour limite, jusqu’à l’extrémité du lac de Génésareth, au bord oriental du Jourdain.
na katika bonde, Beth-Haramu, Beth-Nimra, Sukothi na Safoni na sehemu iliyobaki ya eneo la utawala wa Sihoni mfalme wa Heshboni (upande wa mashariki mwa Mto Yordani, eneo inayoishia kwenye Bahari ya Kinerethi).
28 Tel fut l’héritage des enfants de Gad selon leurs familles, telles les villes et leurs dépendances.
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Gadi ukoo kwa ukoo.
29 Enfin, Moïse donna leur part aux membres de la demi-tribu de Manassé, répartis selon leurs familles,
Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa hiyo nusu ya kabila la Manase, yaani kwa nusu ya jamaa ya uzao wa Manase, ukoo kwa ukoo:
30 et ils eurent pour territoire, à partir de Mahanaïm, tout le Basan, le domaine entier d’Og, roi du Basan, et tous les Bourgs de Yaïr qui sont dans le Basan: soixante villes;
Eneo lililoenea kuanzia Mahanaimu, na kujumlisha Bashani yote, ufalme wote wa Ogu mfalme wa Bashani, makazi yote ya Yairi huko Bashani, miji sitini,
31 plus la moitié du Galaad, Astaroth et Edréi, les villes royales d’Og dans le Basan; ce fut la part des enfants de Makhir, fils de Manassé, dont la moitié y fut cantonnée selon ses familles.
nusu ya Gileadi, na Ashtarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Hii ilikuwa kwa ajili ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, kwa ajili ya nusu ya wana wa Makiri, ukoo kwa ukoo.
32 Telle fut la répartition faite par Moïse dans les plaines de Moab, du côté oriental du Jourdain vers Jéricho.
Huu ndio urithi alioupeana Mose wakati alipokuwa katika tambarare za Moabu, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
33 Mais à la tribu de Lévi Moïse n’assigna point de possession; c’est l’Eternel, Dieu d’Israël, qui était leur possession, comme il le leur avait déclaré.
Lakini kwa kabila la Walawi, Mose hakuwapa urithi; Bwana Mungu, Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.

< Josué 13 >